Sherehe ya kumbukumbu ya Nyerere lakini tunaenda Chato?

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Wakuu,

Sijui kama kuna kitu sijaelewa ila naona kama taifa ni kama tumechanganyikiwa hivi au niseme tumepoteza muelekeo au ufahamu fulani.

Siku inapotengwa kitaifa kumuenzi mtu fulani maana yake siku ile inatakiwa kutumia kutafakari, kujadiliana na kuenzi mafundisho mema ya yule tunayemuenzi.

Sasa nashangaa kuona msururu wa viongozi ukienda Chato badala ya Butiama. Sioni viongozi na taasisi mbalimbali zikiandaa mijadala ya kuhusu mafundisho ya Nyerere.

Hii haitakiwi kuwa siku ya kwenda beach tu au kuangalia tu mpira. Kama fikra za Nyerere zinaonekana zimepitwa na wakati, au viongozi wanaona haya kumuenzi basi hii sikukuu ifutiliwe mbali. Wanaotaka kumuenzi watafanya hivyo kwa namna yao.

Kingine, siku ya kumuenzi ilitakiwa iwe siku yake ya kuzaliwa na si siku ya kufa maana alikufa kifo cha kawaida (tunavyofahamu sisi) ila hilo nitaliacha kwa mjadala mwingine.
 
Labda Kama chato ni marekani..
Swala siyo Chato. Swala kwa nini wanaitumia siku hii kumuenzi mtu mwingine? Siku ya Bwana Yesu unaenda kumuenzi Mtume Paulo? Au wanaogopa kivuli cha Nyerere maana wamezitupilia mbali falsafa zake kwa hiyo wanatuchanganya na mauzauza haya?

Nchi hii tuna ombwe kubwa sana la uongozi hadi inatisha kwa kweli.
 
Wakati Viongozi wote wa kitaifa pamoja na wale wa ccm wakijazana Chato kumuenzi Nyerere lakini kwa kupamba kaburi la Magufuli, BAVICHA watinga butiama kuweka mashada kwenye kaburi la mwalimu nyerere

3642A19D-0CE1-4AFC-A913-67A35BEDD93A.jpeg
 
Wakuu,

Sijui kama kuna kitu sijaelewa ila naona kama taifa ni kama tumechanganyikiwa hivi au niseme tumepoteza muelekeo au ufahamu fulani.

Siku inapotengwa kitaifa kumuenzi mtu fulani maana yake siku ile inatakiwa kutumia kutafakari, kujadiliana na kuenzi mafundisho mema ya yule tunayemuenzi.

Sasa nashangaa kuona msururu wa viongozi ukienda Chato badala ya Butiama. Sioni viongozi na taasisi mbalimbali zikiandaa mijadala ya kuhusu mafundisho ya Nyerere.

Hii haitakiwi kuwa siku ya kwenda beach tu au kuangalia tu mpira. Kama fikra za Nyerere zinaonekana zimepitwa na wakati, au viongozi wanaona haya kumuenzi basi hii sikukuu ifutiliwe mbali. Wanaotaka kumuenzi watafanya hivyo kwa namna yao.

Kingine, siku ya kumuenzi ilitakiwa iwe siku yake ya kuzaliwa na si siku ya kufa maana alikufa kifo cha kawaida (tunavyofahamu sisi) ila hilo nitaliacha kwa mjadala mwingine.

2FC90921-98B8-4A44-8DAB-3BE98821A95D.jpeg
 
Wakati Viongozi wote wa kitaifa pamoja na wale wa ccm wakijazana Chato kumuenzi Nyerere lakini kwa kupamba kaburi la Magufuli, BAVICHA watinga butiama kuweka mashada kwenye kaburi la mwalimu nyerere

View attachment 1974124
Mimi sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa ila naamini kabisa CHADEMA itaenda kuongoza nchi hii. Na siku hiyo ipo karibu kuliko tunavyodhani.
 
Back
Top Bottom