Blessed Tajiri
JF-Expert Member
- Dec 16, 2023
- 221
- 659
Sheikh Ponda kanyooka kama Kitima, ni mwendo wa kupiga kwenye mshono mpaka kieleweke.
====
Katibu wa Shura ya Maimamu Tanzania ambaye pia ni mwanachama mpya wa Chama cha ACT Wazalendo, Sheikh Ponda Issa Ponda, ameungana na Askofu Mkuu wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania (Ufufuo na Uzima) na Mbunge wa Kawe kupitia CCM, Bishop Dr. Josephat Gwajima, katika kulaani vitendo vya utekaji wa raia vinavyoripotiwa nchini.
Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara wa chama cha ACT Wazalendo uliofanyika katika viwanja vya Mwembeyanga, jijini Dar es Salaam, Sheikh Ponda alisema kuwa serikali imeshindwa kuwalinda raia wake dhidi ya vitendo vya kihalifu ikiwemo utekaji na vitisho. Alisema hali hiyo inaiweka serikali kwenye nafasi ya kuhojiwa kuhusu uhalali wake wa kuendelea kubaki madarakani.
====
Katibu wa Shura ya Maimamu Tanzania ambaye pia ni mwanachama mpya wa Chama cha ACT Wazalendo, Sheikh Ponda Issa Ponda, ameungana na Askofu Mkuu wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania (Ufufuo na Uzima) na Mbunge wa Kawe kupitia CCM, Bishop Dr. Josephat Gwajima, katika kulaani vitendo vya utekaji wa raia vinavyoripotiwa nchini.
Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara wa chama cha ACT Wazalendo uliofanyika katika viwanja vya Mwembeyanga, jijini Dar es Salaam, Sheikh Ponda alisema kuwa serikali imeshindwa kuwalinda raia wake dhidi ya vitendo vya kihalifu ikiwemo utekaji na vitisho. Alisema hali hiyo inaiweka serikali kwenye nafasi ya kuhojiwa kuhusu uhalali wake wa kuendelea kubaki madarakani.