Sheikh Ponda amua moja ueleweke!

Sheikh Ponda amua moja ueleweke!

Aksante sana mkongwe mohamedi saidi kwa mchango wako hoja yangu ipo hapa ndio maana nimesema wasije wakampa kesi ya udini kwa maana ya kuambiwa ni gaidi,ila achukuliwe kama mwanasiasa maana ukiwa mwanasiasa upo huru kusema chochote, ukiwa sheikh na ukauvaa usiasa muda wowote unaweza kuwa katika orodha ya magaidi!
Kipara...
Toka zimeanza kesi za ugaidi hakuna hata kesi moja sheikh yeyote
amekutwa ha hatia ya ugaidi huu sasa mwaka wa 15.

Kesi mashuhuri ya masheikh wa Uamsho huu mwaka wa 4 ushahidi
bado haujapatikana kuwatia hatiani kwa ugaidi.

Ama kuhusu suala la udini ikiwa Sheikh Ponda atashtakiwa kwa hilo
sijui itakuwa katika kipengele gani cha sheria.

Lakini hebu tujaaiie kuwa atashitakiwa kwa kosa la, ''udini,'' basi hiyo
itakuwa kesi ya karne na mengi ambayo hayajasemwa hadharani hapo
yatasikika mahakamani Sheikh Ponda atakaposimama kujitetea.
 
Kwa maelezo ya Mzee M. Said tuseme kujitosa kwa Sheikh Ponda ina maanisha sasa tunaingia kwenye matatizo makubwa ya kisiasa? Kiasi kwamba waTz wenye uelewa tujiandae kuingia kwenye utawala wa ki-imla?
Je siasa hizi zina manufaa na hasara gani kwa sababu naona kuna nchi kama Rwanda ina mfumo huo na inaonekana kusonga mbele.
Sheik ametuamsha siyo kuupinga utawala bali tukemee aina hii ya siasa je kwa mzee kama M. Said ana maoni gani?
Mimi naona tusipo kemea hasa tabia ya kuwadhuru wakosoaji itazalisha watawala wa kudumu madarakani kwa sababu watakuwa wamejijengea maadui wengi na wataogopa kuachia madaraka.
 
Jamani huyo mpendwa analo tatizo litokanalo na jina lake alilolirithi. Tumuombee tu kwa kuachilia damu ya Yesu Kristo iweze kumfunğua ufahamu wake. Hiyo ndiyo njia sahihi ya kumjulisha ili kuepukana na noah nyeusiiii na Nissan patrol nyeupe. Basi
 
Sheikh Ponda ni muda mrefu anajulikana kama mwanaharakati na kiongozi wa kupigania mali za waislamu,Ponda ana historia ndefu na amepatwa na misukosuko mingi katika kuendesha harakati zake na wengi walijitokeza kumtetea kwa sababu ya kuvaa kofia ya kuonyesha kuwa anatetea imani fulani,lakini hili linalotokea sasa ni dhahiri sasa Ponda anajipambanua kuwa ni mwanasiasa na yupo tayari kisiasa na tumkaribishe rasmi katika ulingo wa siasa na asihukumiwe kidini aonekane ni mwanasiasa kama wengine tu

Ponda asiogope mbona dkt Slaa alikuwa ni askofu akaamua moja,mchungaji Msigwa na bado wanafanya siasa za uwazi bila ya kujificha kwenye kivuli cha dini.

Ponda hukuzungumzia msikitini habari zako umezungumzia ukumbini,wakili ni Safari makamu mwenyekiti CHADEMA hivyo umekamatwa kama mwanachadema.

Pesa ya chadema haikuwahi kuwaacha watu salama

Ponda umevalishwa mkenge!

Siasa mpaka 2020!
Mleta mada nipunguani kweli kweli yaliompata lisu nayeye aliwahikupatwa viongozi wengine wakidini huenda wanafaidika nahali hivyo yeye kamaraia na kiongozi wataasisi yadini hayupo tayari kuona uhai wamtu unakatishwa ndio maana serekali huwatumia viongozi wadini kuhubiri amani lakini amani inaweza kuvurgwa hata naserekali pia lakini watu wengi huokopa kuiambia serekali ndio wanajitokeza viongozi kama shekh ponda nakusema ukweli sasa wewe ulivyo kilaza uelewi hivyo nadhani umefundishwa kusema ndiooooo
 
Prof. Safari kwa kuwa ni mwanachama wa CHADEMA, kwa hiyo haruhusiwi kufanya kazi yake ya uwakili? Tuna watu ambao wanadhani kujifanya wajinga ni sifa.
Sio wanajifanya, ni wajinga kwelikweli tena IQ ya kifaranga
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom