HAYA NI MAKADILIO YA KIMATAIFA KWA WATU WALIOSOMA RESEARCH WATANIELEWA. Si lazima Kumfuata Mtu na Kumuuliza..
WE TAKE SAMPLE
Sensa ya 1967
Takwimu ya dini nchini Tanzania kwa sasa haipatikani kwa sababu maswali kuhusu dini yaliondolewa na serikali katika sensa baada ya
mwaka 1967. Sensa ile ya tarehe 27 Agosti ilihesabu wafuasi wa dini za jadi kuwa 34.3%, Wakristo 33.5% na Waislamu 31.4%, mbali na wengineo 0.8%.[1]
BAADA YA HAPO
"World Christian Encyclopedia" (toleo la pili, Oxford 2001) imekadiria kwa mwaka 2000 Wakristo kuwa 50.4 % (Wakatoliki 24.7%, Waprotestanti mbalimbali 16.5%, Waanglikana 7.9%, wasio na madhehebu maalumu 3.5%, madhehebu huru 1.9%, madhehebu yasiyokubali imani ya msingi ya Wakristo wengine wote 0.1%, wenye kufuata madhehebu mawili kwa wakati mmoja 4.2%),
Waislamu 31.8%, wafuasi wa dini za jadi 16.1% na wengineo 1.8%.
Pia imetabiria kwa mwaka 2025 uwiano kuwa 56.1, 32.8, 8.9 na 2.1%, na kwamba kufikia mwaka 2050 Wakristo na Waislamu watakuwa karibu 65 na 35% kati ya wakazi wa nchi.
Taarifa ya "International Religious Freedom Report 2009" kutoka Marekani Bureau of Democracy, Human Rights, and Labor
kwa mwaka 2009 unaotaja 62% ya Watanzania kuwa Wakristo, 35% Waislamu na 3% wafuasi wa dini nyingine.[4]