Viongozi wa kiislamu wanatakiwa wawashauri waumini wao kupenda maendeleo na ushindani wa kiuchumi. Wakati waarabu (ambao ni waislamu) wanapenda maendeleo kwa kusoma, kuwekeza, kushirikiana na wenzao, hawa weusi kama mimi wanalilia wingi wa namba ili serikali iwape mkate kila siku na vyeo serikalini bila ya kujituma.
Hii hulka ya kujiona wanaonewa ni dalili za kutojituma na kukosa matumaini katika nchi ambayo imeongozwa na waislamu kwa miaka 20 ya miaka 50 ya uhuru wake. Kikwete alimweka Hawa Ghasia utumishi ili waislamu wengi waajiriwe matokeo yake hata upendeleo haukutosha hawako wengi qualified na hili ni tatizo la waislamu wenyewe na siyo JMT wala vatican, wala nchi za Magharibi.
Tanzania ni nchi huru waislamu wanatakiwa kuacha chuki na kushirikiana na wasiokua waislamu katika nyanja mbali mbali za kimaendeleo na vile vile kujifunza toka kwa wengine kama wanavyofanya waislamu wa arabuni, uturuki, indonesia n.k
Kuna mnigeria mmoja nilikua naongea nae na akaniambia kitu kizuri sana kuhusu suala la waislamu na wakristo hapa afrika kwa ujumla; alisema wakati Nigeria wakristo wanatumia bidii kutafuta maendeleo binafsi kwa kupata elimu nzuri, uhuru, kufanya kazi kwa bidii na kujituma, waislamu wanawaza siasa na filosofia ya kuifanya Nigeria kua nchi ya kiislamu huku wakisahau maendeleo yao wenyewe kwa kufikria kila mara kua wana jukumu la kuisafisha Nigeria na kuitawala kiislamu.
Najua sheikh Ponda hajafikia hatua ya kutaka "kuisafisha" tanzania ili itawalike kiislamu, nafikiri anachotaka kusema ni kua serikali iwape zaidi mkate mkubwa kwa kua wao ni wengi, sasa sheikh wangu mkate mkubwa bila kushirikiana, bila elimu, bila kua na akili ya kimaendeleo ya kuwekeza na kujiendeleza si utakua ni bure. Nigeria katika viongozi wake toka huru wamekua na viongozi wakuu wa kitaifa 13 kati ya wote hawa watatu tu ndiyo wamekua wakristo, lakini waislamu pamoja na mkate mkubwa wamebaki maskini huko Kano, kaduna, katsina kwa sababu za kutojiendeleza, na utajiri umebaki bado kusini kwa sababu hela haikai bure, hela inaenda kwenye uzalishaji na wazalishaji. Matajiri wote wakubwa Nigeria ni Waislamu, lakini hawakai Kaskazini kwao, wako kusini na hawawekezi kwao wanaweka hela kusini na Ulaya wakiwaacha watu wao maskini wa kutupwa.
Sheikh Ponda hata waislamu wakiwa 60% bado hii haijalishi lazima wanafunzi 6 kati ya 10 lazima wa elimu ya juu lazima wawe waislamu, au serikalini kati ya watumishi 10 lazima 6 wawe waislamu. duniani kote affirmative action inatumika kwa minority na siyo majority.
Mharakati,