Kibanga Ampiga Mkoloni
JF-Expert Member
- Aug 9, 2007
- 18,697
- 8,843
Kuna watu wa ajabu sana humu jf, suala la kupigwa shekh ponda si la kufurahisha kwa mtu yeyote, hata kama ana makosa si sawa kuchukua sheria mkononi dhidi yake.
Sasa mnaokuja na suala la CHADEMA na UDINI mnahusisha vipi na tukio hili? Ni CHADEMA wamemdhuru au ni DINI flani?
Hata kama tunatumwa kutetea maslahi ya watu flani na kupotosha ukweli yatupasa muda mwingine kutumia ubinadamu.
Yamkini mnakua mmetumwa ili kupotosha mada, watu waache kujadili dhima kuu ya habari na wajadili kile mnachopindisha, siku moja mtakosa wa kupindisha maana habari itawahusu ninyi. Ritz, FaizaFoxy
Mbona mapovu mengi huku Hoja huna.
Last edited by a moderator: