Kiongozi, usiumize kichwa sana. Mara nyingi michango ya namna hii ni ya watu walioshindwa. Mwenye ndoa yenye afya hawezi kupinga kuwa kuheshimiana, kubebeana mizigo, kupendana na hata kuonyesha unyenyekevu ni sehemu ya maisha ya wanandoa( kunyenyekea ni pamoja na kujishusha pale unapoona ulimkosea mwenza, sio jambo baya). Mungu aliyesema "na mume ampende mke wake, nae mke amheshimu mume wake" alimaanisha mengi mno.
Shida kubwa tuliyonayo sasa ni kuchanganya tamaduni, tumekuwa na tamaduni za kimagharibi mno, tumepokea imani za "social activists" wanaotaka gender balance, kitu ambacho hakipo hata katika vitabu tunavyoviamini sana.