Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,468
- 113,583
Wanabodi,
Wakati inajitahidi kujikoa kwa Barrick ili isinunuliwe kwa bei ya kutupa siku ya Ijumaa hii ambayo ndio deadline ya mwisho ya PUSU ya Barrick kutangaza dau, masikini Acacia, mambo yake yazidi kuwa magumu baada ya Baraza la Usimamizi wa Mazingira, NEMC, kusitisha shughuli zote za mgodi wa North Mara, kwa hoja za kimazingira. Yaani ng'ombe yako mnadani, unajaribu kumnenepesha ili apate bei nzuri, mara anateguka mguu!. Na kwa wasiojua, kati ya migodi yote mitatu ya Acacia, North Mara ndio cash cow wake, ng'ombe wa maziwa akichinjwa, nyumbani ni mwendo wa chai ya rangi.
Hivyo sasa, ili Acacia kujarabu kujinasua, isinunuliwe kwa bei ya kutupa na Barrick, leo imeamua kusalimu amri kwa serikali, yaomba kusitisha mashauri yote kwenye mahakama za usuluhishi, iwapo serikali ya Tanzania itakubali kuendelea na mazungumzo na Barrick, ili kujaribu kujikoa na PUSU ya mwisho kutoka Barrick ambayo itarajajiwa kutangazwa keshokutwa siku ya Ijumaa ambayo ndio itaashiria kifo rasmi cha Acacia.
Jisomee mwenyewe hapa.
Kwa msiojua PUSU ni "Put Up or Shut Up"
Wakati inajitahidi kujikoa kwa Barrick ili isinunuliwe kwa bei ya kutupa siku ya Ijumaa hii ambayo ndio deadline ya mwisho ya PUSU ya Barrick kutangaza dau, masikini Acacia, mambo yake yazidi kuwa magumu baada ya Baraza la Usimamizi wa Mazingira, NEMC, kusitisha shughuli zote za mgodi wa North Mara, kwa hoja za kimazingira. Yaani ng'ombe yako mnadani, unajaribu kumnenepesha ili apate bei nzuri, mara anateguka mguu!. Na kwa wasiojua, kati ya migodi yote mitatu ya Acacia, North Mara ndio cash cow wake, ng'ombe wa maziwa akichinjwa, nyumbani ni mwendo wa chai ya rangi.
Hivyo sasa, ili Acacia kujarabu kujinasua, isinunuliwe kwa bei ya kutupa na Barrick, leo imeamua kusalimu amri kwa serikali, yaomba kusitisha mashauri yote kwenye mahakama za usuluhishi, iwapo serikali ya Tanzania itakubali kuendelea na mazungumzo na Barrick, ili kujaribu kujikoa na PUSU ya mwisho kutoka Barrick ambayo itarajajiwa kutangazwa keshokutwa siku ya Ijumaa ambayo ndio itaashiria kifo rasmi cha Acacia.
Jisomee mwenyewe hapa.
Barrick Gold Corporation - Home
www.acaciamining.com
- Serikali iliisha iandikia migodi yote mitatu ya Acacia kuwa haiitambui Acacia.
- Barrick akaamua kuingilia kati kwa kutoa offer ya kuinunua Acacia kwa hostile takeover kwa kutoa dau dogo kwa sababu Acacia haina thamani kivile na too risky. Wakikubali wafe na kupokea kidogodogo, wakigoma wafe kwa kujinyonga wenyewe mazima kupitia kitu kinachoitwa PUSU yaani "Put Up or Shut Up"
- Acacia akagomea offer kiduchu ya Barrick kutoa extention time Barrick ajifikirie kuongeza dau, ambayo hutolewa kwa siku kumi kumi toka deadline ya PUSU.
- Acacia akaanza kujitutumua jinsi alivyo na thamani, deadline ya kwanza ya PUSU ikafika Barrick kagoma kuongeza hata senti moja.
- Acacia akaongeza muda na kujieleza alivyo na thamani, Barrick bado akagoma, PUSU deadline ya pili ikapita, muda ukaongezwa.
- Acacia akatoa financial statement yake na projections za faida kubwa, Barrick akagoma na kusema nothing new. PUSU dealine ya tatu ikaongezwa for 10 days kwa mara ya tatu ambayo sasa ni keshokutwa tarehe 19. hizi PUSU mwisho ni tatu, hii ya keshokutwa ndio ya mwisho.
- Sasa leo huyu ng'ombe yuko mnadani, zinakuja taarifa ngombe wetu ana tatizo la maini!. Atauzika kweli kwenye mnada wa keshokutwa?. Barrick ataongeza dau au anaweza kulipunguza?.
- Tangazo la leo ni Acacia kutaka kuihonga serikali yetu hongo ya kufuta mashauri ili serikali ikubali mazungumzo na Barrick yaendelee kubla ya PUSU ya Ijumaa hii.
- Kama Acacia imekataliwa, ni imekataliwa!, inatoa conditions kwa nani?!.
- Watu tunasubiria hiyo PUSU ya keshokutwa hii biashara iishe.