Serikali yatangaza rasmi Mikoa mipya 4 na wilaya 19

hapo kuna mkoa wa magufuli,pinda,makinda,huo wa simiyu sababu za kisiasa!mkoloni alikua na majimbo tukaendelea kuliko
 
Gavana wa Kiingereza Tanganyika aliweza kuitawala koloni la Tanganyika ikiwa na mikoa michache na kwa ufanisi mkubwa kwa kutumia radio-calls, telegrams, barua, miundo-mbinu ya barabara za vumbi/reli/meli na Ma-DC.

Jambo la ajabu Tanganyika ya sasa ktk sanyansi na teknolojia za kisasa , miundo-mbinu bora zaidi na jeshi kubwa la ma-DC kujaribu kuwa na mikoa mingi iwezekanavyo bila kujali gharama za kuendesha mikoa mingi kupita kiasi ktk hii Tanganyiaka 'huru'.
 
Naona Katavi unaweza kuwa ni mkoa wa kwanza kuwa na wilaya 2 si angalau wangemega wilaya za Kigoma?
Naweza saidiwa vigezo vilivyotumika kama ni ukubwa wa eneo,idadi ya watu,natural resources etc.
 
Watu wanataharuki kutokana na mgomo wa madaktari wengine wanahangaika na mikoa na wilaya mpya! this country is very stupid
 
Iliyopo huduma duni sana, Kwa kuongeza hiyo kwani ndiyo itaboreka? Inachukua miaka zaidi ya mitano kwa Mikoa na Wilaya kusimama kwa miundo mbinu.
 
Na wilaya ya wanging'ombe ni Katibu Mkuu Mstaafu ndio kwao pale...yaani kwanza hakuna haata shughuli yeyote sijui wanajua wanachokifanya ??wanapoteza pesa bure kabisa....kila kitu wanategemea kutoka makambako....sijui wataishije pale jamani kutafuta legacy kazi sana duu
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



SERIKALI YATANGAZA RASMI MIKOA MIPYA MINNE NA WILAYA 19



SERIKALI imetoa matangazo rasmi ya Serikali (Government Notices) kuhusu uanzishaji wa mikoa mipya minne na wilaya mpya 19 ambayo yamechapishwa tangu Machi 2, mwaka huu.


Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema matangazo hayo ambayo yalisainiwa na Rais Jakaya Kikwete tangu Machi mosi, 2012, yanabainisha mikoa mipya kuwa ni Geita, Katavi, Njombe na Simiyu. Mikoa hii imechapishwa katika Tangazo la Serikali Na. 72.

Wilaya 19 ambazo zimeanzishwa na kuchapishwa katika Tangazo la Serikali Na.73 ni Buhigwe, Busega, Butiama, Chemba, Gairo, Ikungi na Itilima. Wilaya nyingine ni Kakonko, Kalambo, Kaliua, Kyerwa, Mbogwe, Mkalama na Mlele. Nyingine ni Momba, Nyang’hwale, Nyasa, Uvinza na Wanging’ombe.

Kwa mujibu wa matangazo hayo makao makuu ya mikoa hiyo mipya minne yatakuwa kama ifuatavyo: Geita (Geita), Simiyu (Bariadi) Njombe (Njombe) na Katavi (Mpanda).

Mikoa hiyo itakuwa na wilaya zifuatazo; Geita utakuwa na wilaya tano za Bukombe, Chato, Geita, Mbongwe na Nyang’hwale. Mkoa wa Katavi utakuwa na wilaya mbili za Mlele na Mpanda. Mkoa wa Njombe utakuwa na wilaya nne za Makete, Njombe, Ludewa na Wanging’ombe wakati mkoa wa Simiyu utakuwa na wilaya tano za Bariadi, Busega, Maswa, Meatu na Itilima.


Makao makuu ya wilaya mpya zilizoanzishwa ni kama ifuatavyo: Buhigwe (Buhigwe); Busega (Nyashimo); Butiama (Butiama); Chemba (Chemba); Gairo (Gairo); Ikungi (Ikungi) Itilima (Lagangabilili); Kakonko (Kakonko); Kalambo (Matai) na Kaliua (Kaliua).

Nyingine ni Kyerwa (Rubwera); Mbogwe (Mbogwe); Mkalama (Nduguti); Mlele (Inyonga); Momba (Chitete); Nyang’hwale (Kharumwa); Nyasa (Mbamba Bay); Uvinza (Lugufu) na Igwachanya (Wanging’ombe).

Julai 2010, kabla Rais Kikwete hajatoa hotuba ya kulivunja Bunge, Serikali ilitoa uamuzi wa kuunda mikoa mipya minne na wilaya mpya 21. Hata hivyo, baada ya kuhakiki mipaka ya maeneo hayo yote na kuandaa maelezo ya mipaka hiyo vizuri (boundary descriptions),wilaya zilipunguzwa na kubakia 19.


(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 3021,
DAR ES SALAAM.
ALHAMISI, MACHI 8, 2012.

==================================================

My Yake: Je kuna umuhimu wa lazima kuwa na mikoa mipya?

Kuna watu muhimu wanastaafu wanahitaji kuendelea kupokea posho za Serikali. Nabashiri Luhanjo atapewa ukuu wa mkoa wa Njombe
 
Naamini kuna taratibu ndani ya mamlaka ( Executive Branch ) ambazo zimefuatwa na kwamba wanachosubiri ni maendeleo na kuboreshwa kwa hali zao za maisha.
 
Ni zamu ya walio dondokea pua uchuguzi mkuu kupendelewa vyeo sasa na wao wale washibe na kuvimba matumbo
 
Namkumbuka Kawegere Fortunatus na kitabu chake SHAMBA LA WANYAMA ikiwa ni tafsiri ya THE ANIMAL FARM by George Orwell....ndio Tanzania yetu INAFANANIA KWA SASA
 
Mkoa wa Katavi utakuwa na Wilaya 2 Mlele na Mpanda?!
This is sickening?! Mimi nafikiri mwandishi amekosea labda alimaanisha 12 SIO 2?
If it is true now where moving in Zanzibar Style ambako huko TARAFA ni MKOA.

Hii yote imefanyika kum please Pinda na Pia kuwatafutia mahawala zao nafasi za U-DCs na RCs.

Bora katiba mpya ije tufutilie mbali hivi vyeo vya RCs & DCs. No wonder zaidi ya miongo 3 bado wanaimba
Serikali kuhamia Dodoma?!
 

Mkoa wa Katavi utakuwa na wilaya mbili za Mlele na Mpanda.......hii sasa ndio nini mkoa kuwa na wilaya mbili tu?.......halafu mikoa yote mipya ni kama kuwapendelea viongozi fulani....Geita(Magufuli).....Simiyu(Chenge).....Katavi(Pinda)......Njombe(Makinda)...

huu ndo Ujinga na upuuzi wa serikali yetu kuwatukuza viongozi wake
1. Hatimaye ombi ya Magufuli lakubaliwa
2. Hatimaye ombi ya Chenge lakubaliwa
3.Hatimaye ombi ya MAkinda lakubaliwa
4.Hatimaye ombi ya Pinda lakubaliwa

This is all Rubbish:A S embarassed:
 
Naona Katavi unaweza kuwa ni mkoa wa kwanza kuwa na wilaya 2. S angalau wangemega wilaya za Kigoma?.

Mkuu Njowepo,
Baada ya haya mabadiliko hata Mkoa wa Rukwa nao utabaki kuwa na Wilaya mbili tu (Sumbawanga na Nkasi)! Ni maajabu!

 
VIGEZO GANI VIMETUMIKA KUPATA HII MIKOA?????

WATU WANAKUFA NJAA serikali unajiongeze gharama katika uendeshaji( nani think tanker wa serikali?))
 
hapa sasa ukuu wa wilaya ingekuwa unagombea ningesema nikachukue fomu japo nijiliwaze na ukuu wa wilaya,

lakini ndo yale yale, mahawara na watoto wao waliowazaa nje ya ndoa zao ndo watapewa nafasi za uongozi ambao hakuna wanachokifanya, me sielewi hii serikali inachofanya ni nini?

its about time tuigawe hii nchi, maana itoshe sasa kugawa mikoa na kuongeza mzigo kwa serikali moja ambayo haina uwezo wa kuihudumia si tu mikoa iliyopo, achilia mbali mikoa mitatu tu.

Suluhisho la pekee sasa ni kuigawa hii nchi zitoke nchi tatu kila mmoja kivyake au tuwe na serikali ya majimbo japo manne ambayo kila mmoja ata manage jimbo lake kama usa.

Aaaaah me nimechoka sasa jamani.



Hii kitu inanichanganya sana, sijui kama hawa jamaa wana chembe ya uzalendo. Hata mtoto mdogo wa primary ukimwuliza hii atakushangaa, nenda sehemu yoyote katika hii dunia huwezikuta Mkoa wenye wiliya mbili ni Tanzania tu. Unajua kwa uwezo na ufanisi wa nchi yetu ilitakiwa tuwe na Mikoa kama kumi tu............. Few but manageable! Siku moj nilikuwa na jamaa yangu wa Kiholanzi akaniambia "Tanzania can't achieve development just because of the structure of administration" sikumwelewa. Now I realise what the guy meant... Mungu aingilie kati, haiwezekani watu wakawa wanagawana nchi yetu kuhunihuni tu,
 
Hapa ndipo ninapoishangaa serkali ya ccm, kwa mtu anaejua ramani na jiografia ya mkoa wa Mara, atacheka na kushangaa jinsi upendeleo na ubaguzi wa kikabila ulivyo hapa mkoani kwetu. Tunaambiwa hakuna ubaguzi wa kikabila, lugha wala dini lakini hapa Mara ubaguzi wa Kabila unaofanywa na ccm pamoja na serkali yake umevuka mipaka ya kibinadamu.
Angalia mwenyewe Bunda, Kiabakari (makao makuu ya Musoma V) na sasa Butiama ni vitongoji vitatu vilivyo jirani sana vyenye kukaliwa na watu wa jamii moja. Sehemu kubwa ya wilaya ya Musoma V iko maeneo ya Majita, uruli na ukwaya lakini chuki za kikabila na serkali ya ccm kutokuwa makini inashindwa kutenda haki kwa raia wa maeneo hayo. Kama ni kuienzi familia ya Nyerere basi Kiabakari na Butiama iwe wilaya moja na makao makuu yawe Butiama na wilaya ingine iwe ya majita yenye makao makuu Mugango au Suguti. Pale walipoanzisha wilaya ya Musoma V, katikati ya wilaya ilikuwa Mugango, makao makuu yalitakiwa yawe pale na maandalizi yalikuwa tayari yamefanyika lakini mkabila mmoja au genge la ukabila wakatumia nafasi zao huko ccm na serkalini wakachakachua uamuzi wa makao makuu kutoka Mugango hadi Kiabakari. na sasa wamemega kaeneo kadogo ka wilaya na kukafanya wilaya ingine. Jamani hizi dhuluma za kikabila huku Musoma mpaka lini?? Angalia hali halisi ya maisha ya watu huku ujitani, uruli na ukwayani, hakuna barabara, hakuna maji ya bomba ingawaje vijiji vingi vimejipanga kandokando ya ziwa victoria, hakuna muundo mbinu wowote kutoka serkali ya ccm tangu uhuru, kila kitu kilicho huku ni kile kilichoachwa na mkoloni!!!!! Je sisi siyo raia kama wengine?? Kosa letu nini?
Kwenye miaka ya 1980's mashine ya kusukumia maji kwenda Butiama ilifungwa maeneo ya Mgango lakini cha ajabu wananchi wa Mgango hawakupata hayo maji ya bomba hadi vijana machachari walipoamua kulisabotage bomba kwa kulipasua ndo ccm na serkali yake wagagundua kuwa kumbe pale Mgango pia pana watu na ndo wakasambaza vibomba vichache kuzuia hasira. Inabidi wana Mara wanaoguswa na hizi dhuluma za wazi tujipange kuikabili hii serkali dhalimu ya ccm na wakabila wake ili tupate haki zetu za kiraia bila kupigiana magoti
 
Back
Top Bottom