Serikali yasitisha mafunzo ya JKT

Serikali yasitisha mafunzo ya JKT

Niliposikia hii habari mwanzoni sikuiamini lakini kulingana na maelezo ninayoona hapa naanza kuamini!
Sikutegemea kama serikali yetu yenye maono na sikivu ingelianzisha projects ambazo hawawezi kuzisimamia hata kwa miaka miwili. Tulitegemea mipango ya serikali ione angalau miaka 10 mbele na sio kuishi au kupanga kwa kutegemea matukio.
 
Siku hizi taarifa rasmi za serikali huanzia JF? JKT ipo kwa mujibu wa sheria na kusitisha inabidi serikali warudi bungeni kubadilisha hiyo sheria.
 

Maoni yangu:

Mafunzo haya ya JKT yapigwe marufuku kabisa na yafutwe maana hayana faida yoyote wala tija katikaTaifa hili. Binafsi natamani serikali ifilisike kabisa ili isiweze kufadhili mafunzo hata tena.



Acha mawazo mgando, acha vijana wale kwata! We last year vijana wa jkt walitusaidia sana kukomesha wezi Mzumbe chuoni. Wezi walizoa kuiba na kuchoropoka wanajificha. Ikaja tokea mwizi kama kawaida yake akaja akaiba, vijana wa jkt wakasema ahaa ngoja, wakatumia mbinu za jkt, mbona walimdaka, na hawakumbakiza, hiyo tabia imekoma kabisa! Hivyo viva jkt
 
Kwa taarifa hii naona inaconclude maneno niliyokwisha yatamka ya kwamba wanatakiwa kutofanya lazima kwa vijana wote bali iwe kama moja ya vigezo vya kupata kazi katika sekta fulani watakazoona kuna haja ya kupita jkt kwanza, haya niliyasema sababu budget yetu ni ndogo sana hatuwezi kuinvest kwenye kukimbiza watu maporini tukaacha kununua dawa hospital. Ni upuuzi wa ccm na viongozi wake kutaka kuiba pesa kwa style ya kuweka mafunzo ya jkt sababu wanajua kule hakuna audit inayofanyika. Bilioni tisa budget ya mafunzo pekee its not a joke kwa nchi ya hovyo kama Tanzania halafu eti jkt lazima, nyerere mwenyewe ilimshinda hatujiulizi kwa nini?
 

Maoni yangu:

Mafunzo haya ya JKT yapigwe marufuku kabisa na yafutwe maana hayana faida yoyote wala tija katikaTaifa hili. Binafsi natamani serikali ifilisike kabisa ili isiweze kufadhili mafunzo hata tena.



Nimesoma uzi wote huu sijaona uthibitisho wa taarifa hii, sana sana ni wachangiaji wengi ni wale wenye hasira na ngariba za kijeshi. Nina wasiwasi iwapo nchi ikaingia vitani vijana wengi wataishia kwenye makambi ya wakimbizi badala ya kuwa msitari wa mbele.
 
Mafunzo ya JKT hayana tija hata kidogo walinawadhalilisha watoto wa kike na kuwaambukza tu. eti wanajenga uzalendo wapi na wapi wakati walioenda JKT ENZI HIZO NDO MAFISADI, WEZI WAKUBWA UPUUZI HUU HATA HAYANA HURUMA NA WALALA HOI. NDO HAO WATOA HUDUMA WENGINE KUJIONA TU ETI UZALENDO. UZALENDO NI MAPENZI MEMA KWA NCHI NA KWA RAIA.
 
Acha mawazo mgando, acha vijana wale kwata! We last year vijana wa jkt walitusaidia sana kukomesha wezi Mzumbe chuoni. Wezi walizoa kuiba na kuchoropoka wanajificha. Ikaja tokea mwizi kama kawaida yake akaja akaiba, vijana wa jkt wakasema ahaa ngoja, wakatumia mbinu za jkt, mbona walimdaka, na hawakumbakiza, hiyo tabia imekoma kabisa! Hivyo viva jkt

uonevu wakawa mahakama
 
Hiyo kazi ni ya polisi sasa tatizo polisi wako busy kula rushwa ndio maana mnaona jkt ndio suluhisho. Hapa kila mtu afanye kazi yake sio mwanasheria afanye kazi ya mwanajeshi mambo ya wapi haya?
 
Hongera kijana kwa kutengeneza habari ya kizushi. Tambua hii siyo fb au twiter ya kujadili habari za kipuuzi zisizo na mashiko na zilizojaa upotoshaji kwa umma. Mafunzo ya jkt yapo kama kawaida.
 
Ni mtu mwoga na mjinga pekee ndiye asiyependa mafunzo ya JKT. wale wote waliochangia kuunga mkono kuwa yafutwe hakika wameonyesha ujinga uliobobea. Wakati vijana wengi wanatamani kwenda huko na wana ari ya kuendelea kubaki huko ninyi mnakuja na uzi wa kutaka mafunzo yasitishwe....:confused3::confused3::confused3:

wewe ndio uache kusema vitu bila reason.kina watu wanaishi maisha magumu huku chuo .hawana mikopo.na wengine wanamikopo nusu bado hawawezi kujilipia.sasa yaanini serijaliifanye allocation JKT wakati haohao wanafunzi wakitoka jkt wanapata shida chuo?ni bora hizo hela zitumike kuwapa mikopo wanafunzi.pia jkt kwa sasa tumekurupuka.maana matatizo y kielimu bado ni makubwa .na uzalendo ni jukumu la mmojaa.mbona wazee wetu walikaa jkt mwaka mzima lakino hao ndio mafisadi wengi wao.
jenga taifa lenye elimu kwanza.ifuatiww na kuimarisha sasa /jkt.
 
kwan yamesitishwa yapi yale ya vijana wa waliohitimu kidato cha sita au wale wanakuja kuajiriwa kua wanajeshi ?
 
Shida ya serikali yetu ni kufanya kazi kama ¬`Fire Department¬¬ yani kuibuka tu na kuanzisha kitu kama ¬¬reaction¬¬ ya jambo jingine. mambo mengi yanayoanzishwa na serikali yetu yanaishia au kutumia tu hela za watanzania, au kufutwa kwa vile inagundulika kuwa hayana tija kwa taifa. Tukumbuke tu mkakati wa kilimo kwanza ulivyaokuja kwa kasi na kuwafanya wananchi waamini kuwa kilimo ndio mkombozi wa maisha yao. Tutakumbuka kuwa serikali imetumia fedha nyingi sana kutoa kwa wananchi ili ziwasaidie kuboresha kilimo. Lakini tunachoshuhudia sasa, ni uzalishwaji mkubwa wa mahindi wakati hakuna soko. Uhalisia ule ule wa hali ya serikali unawakumba wananchi, kwani wanatumia gharama kubwa kuzalisha mazao ambayo hayawapi tija. Najiuliza, serikali haikuweza kufikiria kuandaa soko la uhakika la mazao ambayo yameongezewa uwezo ili kuboresha uzalishaji? Sasa mahindi ya wakulima yanaozea magurioni, au wengine wamekopwa na serikali hadi sasa hawajalipwa, na hao ni wananchi ambao wanategemea kilimo ili wasomeshe watoto, wanunue pembejeo mpya za kilimo na wajikimu katika maisha yao. Najiuliza, kama kweli kulikuwa na mikakati madhubuti ya kuboresha kilimo, kwanini nyanda za juu kusini mikoa kama ile ya Mbeya Njombe, Iringa na Ruvuma ambako kunazalishwa mahindi kwa wingi hakuna kiwanda kilichojengwa cha kuzalisha sembe? Soko la mahindi linapungua kwa sababu zao lenyewe halijaboreshwa. Baadala ya kuuza mahindi watu walitegemea kuona sokoni mazao ya mahindi, ambayo kiuhalisia yangeingia katika soko la ndani ya Tanzania na hata masoko ya nje, kama tungeongeza ubora.
Naunganisha suala hili na lile la kufutwa kwa JKT kwa hoja ya kwamba, bila shaka serikali iliamua kurudisha tena JKT kwa ilipata ushauri toka upande fulani, na sio kwa sababu iliona hitaji hilo. Pengine hata fungu lilitoka mahala fulani, ndio maana lilipoisha ikabidi kufuta JKT. Je hatuoni kama tumesababisha usumbufu mkubwa kwa vijana poezawetu na kuwapotezea muda bila sababu? Tujipange watanzania, ili tuje kuwapata viongozi ambao watakuwa na mwono stahiki ¬¬ Mission¬¬ ambao watakuwa na mikakati mathubuti``Strategic Leaders`` ambao watakuwa ``proactive`` na sio ``reactive`` watakaoweza kuona mbali na kuzuia madhara yasitokee na siyo kusubiri yatokee kisha kuhangaika kutafuta mbinu ya kuyazuia. Ni sisi watanzana tutaibadili nchi yetu tukiwa makini katika kuwahakiki watu tunaowapa madaraka. Pamoja sana ndugu zangu katika kutetea maslahi ya taifa letu.
 
Sasa si unajua wezi pale mzumbe walikuwa kama wachawi vile, yaani anaweza iba hapa akaenda kuiba na pale wala hamumuoni, ila vijana wa jkt wakafanya kazi yao!

Hawahawa unaowapongeza watakuja kudhibiti wizi wa kura kwenye Uchaguzi Mkuu maana hawaogopi Risasi.Nadhani hii italeta taabu kwenye Chama chetu.
 
This government can't ran such nationalistic move because of lack of funds and seriousness.
 
Back
Top Bottom