Serikali yashusha bei ya sukari mpaka Tsh 1,800/=

Serikali yashusha bei ya sukari mpaka Tsh 1,800/=

Ok, imekaa vema. Hata hivyo makampuni wazalishaji wajitahidi kuisambaza. Isije ikatokea kukawa na upungufu kwa baadhi ya maeneo. Kwa mfano, bei ya sukari eneo lenye barabara inayopitika kwa shida kipindi cha masika inaweza kuwa na changamoto, na ukizingatia jografoa ya nchi
Jografoa?
 
Hivi tumeshaangalia ubora wa hii sukari? naona kama ina ladha ya sukari guru na nyingine ina kaharufu ka kiroba au ni mie tu naona hii hali. Na hili la bei linatia shaka, iweje mkazi wa kamachumu auziwe 1800 kwa kilo sawa na mtu wa kyela wakati yeye anaishi mita mia kutoka kiwandani? na anaweza enda nunua sukari kiwandani kwa miguu?
Kamachumu kuna kiwanda gani cha sukari?
 
Teh teh teh eeeee . Imenikumbusha mbali sana kuna babu yangu alikuwa anatumia sukari guru kwenye uji. Teh teh eeeee.
Siyo babu yako sema ni watanzania wengi miaka ya 80 tulikunywa sana chai ya sukari guru
 
Kwenye rangi nyekundu. Acha kukalili theory za kiuchumi!

Nani alikudanganya kama kufanya price capping kwenye market economy ni jipu?

Wewe nadhani unaamini open market ni open ambayo haina hata regulations!

Kumbuka price capping ni moja ya market regulation.

Lakini pia uzalishaji wa ndani uboreshwe kwa mikakati maalum lasivyo tukitegemea uzalishaji huu mdogo sukari itaadimika alafu tunarudi kulekule kurusu sukari kutoka nje.

Ambapo sasa ukichanganya na price capping ambayo haiendani na gharama za usafirishaji na kodi. Tutaishia kupokea sukari ambazo hazina viwango.
 
Nadhani umesoma heading pekee halafu uka comment!

Waraka umetoa maelezo yote!

Sisi Watanzania ni watu ajabu kweli. Tuko active sana kuongea au kuandika lakini ni wavivu linapokuja suala la kusoma kwa makini au maandiko marefu/mengi.
Tuna msongo wa mawazo sababu ya ugumu wa maisha
 
Bei elekezi za shule binafsi mpaka leo kizungumkuti,waache siasa kwenye mambo ya msingi...
 
Nani alikuambia kwenye open market hakuna price capping?

Hata hao waliotuletea market economy mpaka sasa wanafanya price capping.

Kuanzia Marekani mpaka Europe ukienda unakutana na price capping katika masoko yao.

Tuache kukalili theory za kiuchumi!

Price capping kwenye bidhaa zipi!!?

Kwenye open market economy sidhani kama inawezekana ukaweka same price across the whole country. Control measures unaweza kuweka kuzuia bei zisiwe beyond. Price capping kwenye services or utilities could be fine not on commodities. I am a Scientist but this one does not make sense to me!! I still stand to be corrected. I really have to check this before embarking on a serious discussion with any of you guys!! However, to me this would perhaps be a temporary measure ...... but what would be a permanent solution!!
 
Kwenye open market economy huwezi kufanya hivyo. Hayo maelekezo yataleta utata ............. bei ya sukari Morogoro, Moshi au Kagera kunakozalishwa sukari haiwezekani ikawa sawa na Mtwara, Mbeya au Kigoma!! Kama ni hivyo basi itabidi serikali ifidie gharama zingine.

Washushe pia bei za vifaa vya ujenzi!!
Mkuu hiyo inawezekana ili mradi tu kuwe na dhamila thabiti mbona bia na sigara v inauzwa bei ile ile tanzania mzima?
 
Tangazo la namna hii unalibeba na kwenda nalo dukani ukikomalia ni tangazo halali ukipigwa ngumi ya pua kwakweli huna pa kushtaki ni halali yako kabisa.
Unaenda kushitaki kwa mwijage
 
Safi sana magufuli hapa tumepata bonge la kiongozi viva jpm
 
Mkuu hiyo inawezekana ili mradi tu kuwe na dhamila thabiti mbona bia na sigara v inauzwa bei ile ile tanzania mzima?
Mkuu acha bangi sasa mambo ya sigara yanatuhusu nini sisi tunaangalia bidhaa muhimu kwa jamii sigara hata ikiuzwa elfu kumi moja poa tu.
 
Kwenye rangi nyekundu. Acha kukalili theory za kiuchumi!

Nani alikudanganya kama kufanya price capping kwenye market economy ni jipu?

Wewe nadhani unaamini open market ni open ambayo haina hata regulations!

Kumbuka price capping ni moja ya market regulation.
Kwa hiyo mmeshafanya price capping kwa bidhaa na huduma ngapi mpaka muda huu?
Na lengo lenu la kufanya price capping ni nini?
Ile price capping kwa elimu, shule mmeshaifanyia tathmini? Ilikuwa laki 3 na ushee? Tozo wanayolipa wazazi na wafadhili wao kama ada ya shule ikoje leo? Imeshuka au imeshushwa?
'Ujinga' wa Ikulu unarudi kwa kasi
Serikali yapiga ‘stop’ Shule binafsi kupandisha Ada
Serikali yapanga bei tiba hospitali binafsi
 
Hapo sawa sasa manake baada ya kuzuia ya nje wakapandisha bei kiholela
 
Mkuu hiyo inawezekana ili mradi tu kuwe na dhamila thabiti mbona bia na sigara v inauzwa bei ile ile tanzania mzima?

Mkuu, sina tatizo na hii kitu kwani ni faida kwa wananchi!! Nitafurahi wakisema hivi kwenye vifaa vya ujezi pia!!

Lakini ukumbuke kuwa marketing ya Bia au sigara ni tofauti na sukari. Bia TBL wanaipeleka kwa mteja wakati sukari mteja anaifuata kwa mzalishaji!!
 
Mkuu acha bangi sasa mambo ya sigara yanatuhusu nini sisi tunaangalia bidhaa muhimu kwa jamii sigara hata ikiuzwa elfu kumi moja poa tu.
Naona imekurupuka kujibu hujui logic ya post yangu
 
Lakini pia uzalishaji wa ndani uboreshwe kwa mikakati maalum lasivyo tukitegemea uzalishaji huu mdogo sukari itaadimika alafu tunarudi kulekule kurusu sukari kutoka nje.

Ambapo sasa ukichanganya na price capping ambayo haiendani na gharama za usafirishaji na kodi. Tutaishia kupokea sukari ambazo hazina viwango.
Nadhani Bodo ya Sukari watakuwa wamekokotoa gharama zote za uzalishaji na usambazaji kabla ya kufikia kiwango cha bei elekezi.

Uzalishaji utaboreka zaidi kama kutakuwa na viwanda vingi vya sukari. Hatuwezi kuwa na viwanda vingi vya sukari kama tutaendelea kupata sukari kutoka nje ambayo gharama yake ni ndogo kwa sababu viwanda vinavyozalisha vinapata government subsidy ukilinganisha na gharama za uzalishaji ndani ya nchi yetu.
 
Back
Top Bottom