Serikali yashusha bei ya sukari mpaka Tsh 1,800/=

Serikali yashusha bei ya sukari mpaka Tsh 1,800/=

kama ya nje ilikuwa bei hiyo sasa ya ndani wana maana gani kutuuzia bei ya kenya na jinsi watanzania tunavyopenda mahumashi wanaweza kuifanywa iwe adimu tuinunue kama vipodozi vile vya magendo ambayo vimejaa kila mahali wenye kuviuza wanauza kama vibaka wanavyouza simu pale ubungo na pengine this country buanaaaaaa


ccm imeambukiza watanzania wizi wa kila namna
 
Duuh mbona dawa ni ndogo.saana.. kuanzia leo naacha kufanya biashara ya sukari.. tuone sasa..
 
mkuu nimewaza tu ndugu zangu wa kule Kakonko Yaeda Chini, Gamboshi n.k hii bei itawafikia kweli..kwanini wasitoe kama bei ya mafuta?
Kama umesoma vizuri utagundua kuwa kuna watu wanatakiwa kufatilia
 
Mtu wa Kilombero, Mtibwa, Moshi - TPC na Kagera - Sugar naye atanunua kwa bei hiyohiyo wakati production imo ndani ya miji husika, nadhani bei inatakiwa kuwa reviewed kwa maeneo hayo

ungeanza na mbunge wa dodoma, kwa nini apewe mkopo wa gari , wakati hata kwa miguu anaweza fika bungeni
 
Serikali leo imetangaza viwango vipya vya bei ya sukari nchini vinavyoanza kutumika kuanzia sasa. Kwa mujibu Mkurugenzi wa bodi ya sukari Tanzania Henry Semwanza bei ya rejareja ya sukari sasa itakuwa sh. 1,800 kwa kilo moja


20160308_113718-1.jpg
 
Du afazali maana huku kwetu mbeya sukari katoni ni arobaini thelasin na tisa wafanya biashara waliweka dili kutuumiza walaji hapa katikati ya mwez wa pili
 
ungeanza na mbunge wa dodoma, kwa nini apewe mkopo wa gari , wakati hata kwa miguu anaweza fika bungeni

Kwenye suala la sukari nimefikiria
  • gharama za uzalishaji - hapa gharama ni sawa iwe sukari hiyo itatumika Moshi au Songea
  • usafirishaji - hapa kuna gharama inaongezeka kulingana na umbali inakokwenda kuuzwa mfano mzuri ni bei za mafuta zinavyoongezeka kadiri unavyozidi kwenda mbali zaidi toka bandarini
Kwa mantiki hiyo mwananchi wa Moshi au Kagera Mtibwa na Kilombero alitakiwa apate sukari kwa bei nafuu zaidi kwasababu gharama za usafirishaji ni ndogo sana - almost negligible ukilinganisha na yule wa Songea, Rukwa, Mtwara, Mara na Kigoma

Huyu Mbunge wa Dodoma siwezi kumzungumzia, labda unisaidie
 
Je bei hiyo ni kila mkoa na mji au kwa mikoa jirani na Kilimanjaro, Morogoro na Kagera tu? Bei elekezi haijafafanua jambo hilo?
 
Ok, imekaa vema. Hata hivyo makampuni wazalishaji wajitahidi kuisambaza. Isije ikatokea kukawa na upungufu kwa baadhi ya maeneo. Kwa mfano, bei ya sukari eneo lenye barabara inayopitika kwa shida kipindi cha masika inaweza kuwa na changamoto, na ukizingatia jografoa ya nchi
 
Hivi tumeshaangalia ubora wa hii sukari? naona kama ina ladha ya sukari guru na nyingine ina kaharufu ka kiroba au ni mie tu naona hii hali. Na hili la bei linatia shaka, iweje mkazi wa kamachumu auziwe 1800 kwa kilo sawa na mtu wa kyela wakati yeye anaishi mita mia kutoka kiwandani? na anaweza enda nunua sukari kiwandani kwa miguu?
 
Back
Top Bottom