Serikali yashauriwa kuchukua hatua kali kudhibiti matumizi ya pombe kupita kiasi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Mtandao wa Wadau wanaopambana na unywaji wa pombe kupita kiasi nchini Tanzania {TAAnet} umeishauri serikali kuchukuwa hatua kali ili kudhibiti matumizi ya pombe kupita kiasi kwa kuridhia uwepo wa sera ya afya yenye kuweka katazo la matumizi mabaya ya pombe ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa muongozo wa kudhibiti utengenezaji, usambazaji na matumizi kinywaji chochote kile chenye kilevi nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo hii 02 October, 2022 na katibu wa mtandao huo Bi Gladness Hemedi Munuo, imeeleza kuwa Katika kuadhimisha ya siku ya ‘KUPINGA MATUMIZI YA POMBE KUPITA KIASI ULIMWENGUNI’ (NO ALCOHOL DAY) siku ambayo huadhimishwa kila siku ya tarehe 03 Octoba ya kila mwaka Matumizi ya pombe na athari zake ni tatizo linalozidi kukua nchini Tanzania, na linapaswa kudhibitiwa kwa haraka iwezekanavyo hasa wakati huu ambapo kuna aina nyingi za vilevi vyenye kileo kwa asilimia kubwa.

Aidha Taarifa hyo imeeleza kuwa Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Shirika la Kimataifa IOGT-NTO Movement, mwaka 2021 katika Mkoa wa Dodom,kata ya Iyumbu na Makulu,Mkoa wa Manyara wilaya ya Mbulu kata ya Dongobesh na Sanubara, Mkowa Iringa, Iringa Vijijini kata za Ifunda na Kalenga.

dha , katika Mkoa wa Arusha maeneo ya Arusha mjini kata ya Ngarenaro na Mkoa wa Kilimanjaro kata za Rombo na Tarakea umebaini kuwa asilimia 40 ya wanawake mpaka sasa ndiyo wanaotumia pombe nchini Tanzania kwa kiasi cha kunywa pombe mara mbili mpaka mara nne kwa wiki huku wanaume asilimia 51 hunywa pombe kwa kiasi cha zaidi ya mara tatu kwa wiki ambapo Utafiti huu ulidhihirisha kuwa haijalishi ni pombe ya aina gani.

Vilevile Bi Gladness katika taarifa hyo ameeleza kuwa Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Afya Duniani iliyotolewa tarehe 9 May, 2022,Inaonyesha kuwa Matumizi mabaya ya unywaji pombe ni moja wapo ya chanzo cha magonjwa takribani 200 zikiwepo ajali za barabarani.

Mbali na matatizo ya kiafya, matumizi ya pombe kupita kiasi madhara makubwa mengine katika Jamii ni ongezeko la ukatili wa kijinsia na kuyumba kiuchumi kunako sababishwa na matumizi ya pombe na utengengezaji wa pombe kupita kiasi kwa mujibu wa shirika la afya.

Hivyo basi kutokana na hayo yote Mtandao wa Wadau wanaopambana na unywaji wa pombe kupita kiasi nchini Tanzania {TAAnet} wametoa rai kwa serekali na wizara husika kupokea kilio hiki ambapo {TAAnet}inawakilisha mashirika mbalimbali nchini, kushughulikiwa kwa haraka.

Bi Gladness Munuo Amehitimisha kwa kueleza kuwa taarifa hii fupi, wana inaimani kubwa Tanzania inapokumbuka siku ya ‘KUTOKUNYWA POMBE DUNIANI’ kama ilivyotolewa kwa niaba ya Mtandao wa Asasi zinazopinga matumizi mabaya ya pombe nchini Tanzania TAAnet, Serikali Itaendelea kuchukuwa hatua Zaidi.

Source: Dira ya Maisha
 
Back
Top Bottom