Serikali yaajiri walimu hewa(?) Ushahidi huu hapa...

Serikali yaajiri walimu hewa(?) Ushahidi huu hapa...

Mkuu haya majina ni Ajira ya mwaka gani?
Mbona hao walio ajiriwa week iliyopita majina ya A yanaishia 296.
Fuatilia vizuri mkuu,Hayo majina ni kweli yamejirudia. Nje ya Hao watu hewa pia kuna mtu kapangiwa kufundisha Mathematics na Book keeping, Mathematics na Account au Biology na Home economic. Hivyo vitu havipo kabisa. Kuna jamaa anasomo moja lakini kajaza mawili na kaenda. Ukifuatilia hizo ajira yamejaa madudu ya kutisha sana.

Shida huu uzi utakosa nguvu coz haumpondi jiwe au kiongoz yyt direct. Lkn ni uzi moja makini sana na kama ni userious Wazira anaweza wajibika kupitia hili.
 
Huwa wanapika Data vibaya sana. Ndio maana wakatunga sheria ya takwimu ili zisitolewe Data za kweli bali za kwao za kupika tu.
Mkuu mwenyewe niligundua ajira nyingi sana ni HEWA na kama zipo basi waliopewa sio waliostahili. Nina Uthibitisho wa vitu vingi sana kuhusu uozo wa hizi ajira.
 
Kwahyo hapo Jafo kapgwa Chenga bla kujua au Naye anatuzuga tu
 
Duuh!!!
IMG-20190501-WA0002.jpeg
 
Naomba ninene kidogo kwenye hizi ajira.

Kwanza kabisa niunge mkono hoja ya mwanzilishi wa huu uzi kwa kuchangia kama ifuatavyo

Hizi ajira zimetoka kwa namna ambayo kiasi kwamba ukiamua ufuatilie kiundani utapata maswali mengi kuliko majibu. Tumeona kuna watu mbali mbali wameajiriwa mara mbili tena katika vituo viwili tofauti na wengine wameajiriwa nje ya vigezo vilivyokuwa vimewekwa kwenye tangazo la ajira.

Ninachojiuliza je hawa wanaopangiwa vituo mara mbili ni hewa nyongine inaingia serikalini??

Je ni wale ambao wameajiriwa kwa michongo ndo maana imepelekea majina yao kuajirika mara mbili??

Ni kwanini katika awamu hii kipengele cha vyuo walivyosoma hakijawekwa tukajua na miaka yao ya kumaliza?? Kwanini wafiche wakati mara kadhaa wamekuwa wakikiweka hiki kipengele??

Hii yote inadhihirisha ni kwa namna gani kuna madudu kwenye hizi ajira ambayo yamefanyika.

Hapa pichani ni mmoja kati ya waliopangiwa vituo mara mbili ambapo kituo cha kwanza kapangiwa iringa kingine kigoma. Kilichofanyika wameacha majina yale yale, center number yake ya shule (O level) ile ile isipokuwa wamebadili mwaka wake wa kuhitimu masomo ambapo mwanzoni inaonyesha kamaliza kidato cha nne 2012 na kamaliza kidato tena cha nne mwaka 2013 NOTE:majina ni yale yale. Nimewawekea picha hapa ili muweze kuitazama
Naomba mrejee kwenye jina namba 3244 na 3245 kwenye ajira za waliopangiwa kwenda sekondari. Naomba pia mrejee katika jina namba 3251 alafu mje tujuzane hapa maana mhusika tajwa kwenye hiyo namba amemaliza kidato cha nne 1994 je kwa sasa atakuwa na umri gani na ataitumikia serikali kwa miaka mingapi(ikumbukwe watu wa zamani walikuwa wanasoma wakiwa wakubwa kidogo)
Screenshot_20190430-172550.jpeg
 
Mkuu haya majina ni Ajira ya mwaka gani?
Mbona hao walio ajiriwa week iliyopita majina ya A yanaishia 296.
Pole sana! Watanzania wengi ukiwemo wewe si wapenzi wasomaji bali ni wapenzi watazamaji.

Hapo kuna ajira za aina mbili yaani msingi na sekondari na inaanza list ya msingi A mpaka Z halafu ya sekondari A mpaka Z na yanaanzia namba 3089
 
Mtoa huu uzi nimetafakari sana lengo na nia ya ww kutumia hiyo Avatar !! Nimejifunza mambo mengi mojawapo ni kwamba jina huumba!! Hakika "Trust None" narudia tena " kweli kabisa Trust None" huyu ni mwanajf kwa jina lake ambalo hakika analiishi hana imani na mtu au taasisi yoyote ndio maana kafanya hiki alichokifanya !!! Hakika trust none!

Hii ndio Jf , am proud of it ! Hongera sana sana ,,,hii ndio maana tunasema humu jf ni kwa ma greatthinkers!!

Thanks !!
Anastahili pongezi mtoa uzi
 
Njia ya muongo ni fupi .

Uwezi wadanganya watu milele.

Ipo siku mauti itaumbua upupu wote huu.
 
nacheka kama mazuri vile

kwanza nacheka huo hayo mambo niliyoyasoma kwa thread na kisha ninasikitika

pili nacheka jinsi watu walivyo na muda daaaaah
Kuna watu wanalipwa kadri wanavyotumia internet na kumbukuka uchunguzi/ufukunyuzi ni kazi na inaingiza pesa
 
Sin maana kwamba napinga mkuu punguza jazba mimi nimeuliza.
Sababu hiyo takwimu ya A nimeangalia hii ajira ya April. Huku kwengine ni sawa ila hiyo ya A sijayaona. Labda kama sio Ajira ya April.

Nikatika hali ya kutaka kujiridhisha tu.
Tazama kuanzia jina namba 3089
 
Back
Top Bottom