Serikali ya Tanzania yatoa tamko, yamlilia Gaddafi

Ni lazima tufahamu kwamba historia haina reverse, kwa maana kwamba yaliyotokea yametokea lakini kwa vyovyote vile waliokuwa wakimpenda na wale wanaodhani kwamba walikuwa wakimchukia, wote watamkumbuka kama mtu aliye lipenda taifa lake pamoja na mapungufu yote aliyokuwa nayo kama binadamu.

Na kilichomponza ni nia yake ya kutaka kuunda USA ( Africa ). Hii iliyatisha sana mataifa ya ulaya kwa sababu Ulaya imefilisika na tegemeo la utajiri wa ulaya ni wizi unaofanywa sehemu mbali mbali za Africa uwe wa dhahiri au uliojificha. Wizi wa dhahiri ni kama iivyo kule Congo (RDC/DRC) na uliojificha ni kama huu wa hapa kwetu ambapo watu hujifanya hamnazo na kuingia mikataba mibovu kwa niaba ya nchi kwa makusudi.

Kwa wale watakaobisha kuhusu hili kwamba Gaddafi hakuwa na chochote kizuri kwa Libya watuambia kwa idadi na majina ni nchi gani duniani ambazo zinatoa huduma kwa wapiga kura wao kama alivyokuwa akifanya Gaddaffi.

Binafsi kama mtanzania ningefurahi kuwa na aina ya viongozi kama Gaddafi hapa kwetu na awe mwizi kwa kiwango cha Gaddafi ila pia atoe huduma za jamii kama alivyofanya Gaddaffi, hii watanzania wanaihitaji sana hasa katika gawio la keki ya taifa ili ifike kwa kila mwananchi bila kujali chama atokacho.

Tunapozungumzia demokrasia sijui tunamaanisha nini? Mfano kama hapa kwetu kiwango cha demokrasia ni kitu cha kufikirika kwa kuwa matokeo ambayo hutangazwa sio uamuzi wa wapiga kura ila tume ya uchaguzi ambayo ni ya chama tawala.

Mungu ibarika Africa yenye viongozi waoga ambao wanaweza kutochukua hatua yoyote mpaka kiongozi mwenzao akiuwawa na wakoloni ndipo huja na kulalamika wakati haina tija yoyote.


Rest In Peace my hero!
 
..................Tunapozungumzia demokrasia sijui tunamaanisha nini? Mfano kama hapa kwetu kiwango cha demokrasia ni kitu cha kufikirika kwa kuwa matokeo ambayo hutangazwa sio uamuzi wa wapiga kura ila tume ya uchaguzi ambayo ni ya chama tawala................

saw sawa kabisa Mkuu...........Wakati ule wa BCS and Economic Forum......hili suala ya demokrasia lilizungumziwa sana....na hasa Bob Mkandara alisema waafrika tunahitaji kuja/ku-taylor demokrasia model yetu.........hii ya kuiga iga......au mataifa makubwa ku-impose model zao za demokrasia............inatu-cost sana..........in my opinion......
 
Tanzania kwasasa atuna udikteta, dikteta mwalimu nyerere alishakufa kwani yeye alitunga sheria yake ya detention kuwakandamiza walie pminga, alafu leo tunamwita babab wa taifa, gadafi ni shujaa wa afrika na waarabu pia, Dr silaha ni kibaraka wa vatican na ujerumani
 
wa afrika tunatakiwa kujikomboa upya kutoka kwa mabeberu haya kama ambavyo walifanya mababu zetu, tulisoma kwenye historia na tukawasifu lakini sasa tunaitaji wajukuu zetu waje watusifu kama ambavyo sasa tunawasifu kina mkwawa, isiki, abushiri, kinjekitile na wanginewe, awa walichoshwa na ukoloni wakaamua kutumia mbinu zote walizoweza hatimaye wakoloni wakasalimu amri wakautoa uhuru, leo hii wamekuja na propaganda za kueneza demokrasia duniani, hawa ni waongo wakutupwa kabisa kama auamini hili jikumbushe wapalestina walivyofanya uchaguzi wao kwa amani na uhuru na kukichagua chama cha hamasi kuwaongozi wakaja juju na kuwaita magaidi ,hata kama magaidi sindio hao waliochaguliwa kwa demokrasia, au demokrasia gani waliokuwa wanaitaka, ivi inawezekana vipi watu wanabeba silaha alafu gadafi awaache eti tukaambiwa wanaandamana kwa amani ila gadafi anawauwa, ivi leo wanafunzi wa UD Washike silaha waandamane alafu serikali iwaachie eti demokrasia ni kweli tutakuwa na serilkali apo, KWA WALE AMBAO WALIKUWA AWAJUI NA WAKAAMINISHWA UONGO WA ALJAZEERA, CNN NA BBC eti libya wanamaisha ya taabu sana basi wakumbuke makala ambayo ilikuwa inarushwa na ITV karibu wiki nzima kabla ya uasi wa kijambazi ikionyesha libya ilivopata maendeleo na maisha yasivokuwa ghari kupita nchiu zote za mashariki ya kati na afrika kwa ujumla leo hii unawezaje kumwita gadafi dikteta, dikteta kwa kuwapa maisha mazuri watu wake, wazungu waliogopa hata pale mwanae gadafi alitangaza kuwa wapo tayari kufanya uchaguzi wa haraka kwa kujua kuwa gadafi angeshinda kwakuwa aliungwa mkona na asilimia 90% ya walibya
 
jmushi1,

..inafika mahali wananchi hawaridhiki na handouts[elimu,afya,makazi,..] anymore.

..mwanasiasa lazima uwe na uwezo wa kusoma psychology ya wananchi unaowatawala/ongoza.

..once ppl have access to free education, healthcare,and housing, they will start demanding other things like freedom of expression, worshiping, rights to organize, etc etc.

..binafsi nadhani viongozi kama Gaddafi alishindwa kwenda na wakati, na kutambua mahitaji[matamanio] ya wananchi wake, haswa vijana.

..upeo wa KIMASIKINI wa WATANZANIA ndiyo unaotufanya tuwashangae wananchi wa Libya kwa kumkataa Raisi "anayewapatia" elimu bure,afya bure, etc etc.

..tena kitu cha ajabu zaidi wapiga kura wa Tanzania walimkataa mgombea Uraisi, na chama, kilichotoa ahadi ya kutoa elimu hapa Tanzania. badala yake wananchi wakamchagua mgombea aliyekuwa akigawa T-shirt na pilau.

..inawezekana ndugu zetu wa vijijini nao wanatushangaa[JF members] jinsi tunavyoilaumu serikali, na chama tawala, wakati wao kila msimu wa uchaguzi hupewa pilau, sukari, huletewa bendi za muziki etc etc.
Psychology ya wengi wa watanzania ni kuondoa mafisadi.Sema hawajapata msaada wa NATO.

Ukisaidiwa na NATO kuna nani atakayekuzuia?

Wenye kupiga kura ni wachache.Ila wenye kuichukia serikali ni wengi.
 
Tatizo la Membe haamini katika nguvu ya umma, anaamini vifaru na mizinga! Historia inatamka wazi "PEOPLE CAN DEFEAT THE STRONG ARMY". Tanzania ina Defence Force haina ARMY, kwa hiyo wananchi tukiamua tunaweza kumtoa fisadi kwa marungu na mishare tu siyo Pick-up tena. Aibu imrudie Mende kwa kutotambua Nguvu ya Umma iliyomkimbiza Quaddafi Tripoli.
Sidhani iwapo hiyo ni kauli ya baraza la mawaziri; na wala si kauli ya bunge! Kauli hiyo ya Membe ni shinikizo toka kwa kikwete! Huyo anayeliliwa ni Ghaddafi yule aliyeungana na Iddi Amini kuivamia Tanzania mwaka 1978 - 1980? Au ndio wanadhani watanzania wamesahau historia? Hizo ni porojo tu zikiongozwa na hisia za udini. Hebu basi wafunge ubalozi wa Libya tuone!
 
The most lasting legacy from the death of Gaddafi is that dictators often begin to believe their own narratives... Were he not completely blinded by his own sense of power and omnipotence, Gaddafi might have realized that the rats and cockroaches were winning, and perhaps, that he needed to negotiate his exit from power, or even arrange exile in a neighbouring nation. He did neither... The upturned face of a dead Gaddafi boils down to one thing only - dictators everywhere should be afraid, very afraid
 
Naungana na Membe kuwa si utamaduni wa Watanzania kushangilia kifo hata kama ni cha adui wao (lakini haimaanishi kuwa watanzania hawafurahii vifo vya maadui wao) kiukweli lugha ya Membe ni ya Kidiplomasia zaidi kuliko ukweli wa kuhusu Watanzania nitatoa mifano mitatu

I/ Chama cha wananchi CUF kilifanya maandamano huko Zanzibar ya kupinga matokeo ya uchaguzi wakapata kichapo na idadi kubwa ya watu kuuwawa CUF inadai waliokufa walikuwa 75 lakini serikali inadai waliokucha 12 cha msingi hapo watu(watanzania walikufa bila kujali idadi yao). Nini maoni yaliyotolewa na Rais wetu Mkapa na wana CCM kipindi hicho? ninachokumbuka kukisiakia ni kuwa wanaCuf hao walivamia kituo cha polisi na kumchinja polisi sasa walitegemea nini kiwapate? wapo waliosema kilichowapata ndio stahili yao warudie tena waone, wengine walisema serikali haijalala itapambana na wachochezi na wavuruga amani ya nchi kwa nguvu zote. Hakuna kiongozi wa nchi aliyelaani mauaji hayo bali CUF walikemewa na kudhihakiwa sana na serikali. Kama nchi kupitia serikali yetu hatukuonyesha utamaduni wa mtanzania kuhuzunika kifo kikitokea bali tulilazimisha watanzania waelewe kuwa wafuasi wale wa CUF walistahili mauti yaliyowakutaa. Kama tulishindwa kuonyesha utamaduni wetu wa kuhuzunika kifo cha adui yako kikitokea kwanini watu walazimishwe kuonyesha hisia za huzuni kwa kifo cha Gaddafi?

II/ Waislam waliuwawa na Polisi pale Msikiti wa mwembechai magomeni lakini hakuna si Rais ,serikali yake wala CCM iliyopinga mauaji yale, ni ukweli uliom;wazi maana nilishuhudia tukio hilo la mauaji kupitia kituo cha tv cha itv kiongozi wa polisi akimuelekeza polisi wa ngazi ya chini akimwambia mpige yule pale (aliyeangalia itv wakati wa tukio hilo atakuwa shahidi yangu)Lakini kama nchi kupitia serikali yetu hatukuonyesha utamaduni wa mtanzania kuhudhunika kifo kikitokea bali tulilazimisha watanzania waelewe kuwa waislam wale walistahili mauti yaliyowakuta

III/Miezi michache ilizopita CHADEMA waliandamana mkoani Arusha kilicho wapata ni kama cha CUF kule Zanzibar hila huko Arusha walifariki/uwawa watu wa 3, hadi leo ni maneno ya dhihaka na kejeli yanatolewa na viongozi wa CCM na serikali yake kuhusu kilichowapata marehemu na majeruhi wa maandamano ya Arusha.Hakuna kuhuzunika bali wanasisitiza kilicho wapata kiwefunzo kwa wasiotii amri za polisi na sheria ( usipotii amri ya polisi na sheria wewe kifo ni haki yako) Lakini kama nchi kupitia serikali yetu hatukuonyesha utamaduni wa mtanzania kuhudhunika kifo kikitokea bali tulilazimisha watanzania waelewe kuwa wafuasi wale wa CHADEMA walistahili mauti yaliyowakuta.

ROHO za watanzania hawa zilizopotezwa THAMANI YAKE NI NDOGO ukilinganisha na  ROHO moja ya GADDAFI? AU kwa kuwa GADDAFI alikuwa kiongozi? au kwa sababu alikuwa na ukwasi ambao aliwafadhili viongozi wa Afrika? Damu za watu zilizomwagwa na GADDAFI zikiwemo za Watanzania hazina thamani kuliko Damu ya GADDAFI?
GADDAFI ni muuaji kama wauaji wengine, ni mbaka Demokrasia kama wabakaji wengine na ni king'ang'anizi wa madaraka kama viongozi wengi wa Afrika, Dhambi za GADDAFI wanazijua zaidi Walibya kuliko sisi waTanzania, waache wafurahie kifo chake maana roho na nafsi zao zinzfuraha tusiwarazimishe wapi pa kufurahi na wapi pa kuhuzunika.MEMBE akumbuke GADDAFI alishilikiana na NDULI IDDI AMINI kuuwa watanzania wenzetu wakati wa vita ya KAGERA sasa usiwaladhimishe waliopoteza ndugu zao ktk vita hiyo wasifurahie kifo cha GADDAFI. GADDAFI kapata haki yake UKIUA KWA UPANGA NAWE UTAUWAWA KWA UPANGA.MEMBE na SERIKALI acheni unafiki ktk suala hili kama nchi tungepinga wazi wazi uvamizi wa NATO na UASI wa Baraza la mpito la LIBYA, kama nchi tungeonyesha msimamo wetu wazi bila kificho wala kumung'unya maneno tungekemea uvamizi ule (Wakati wa mwl Nyerere tulikuwa tunaonyesha wazi misimamo yaetu kama nchi ktk dunia hii) Lakini tusijifanye wasemaji baada ya GADDAFI kuuwawa.NAWAHAKIKISHIA WANA JF BAADA YA MUDA TUTALITAMBUA BARAZA LA MPITO NA KUSHIRIKIANA NAO KIDIPLOMASIA NA KTK SHUGHULI ZA MAENDELEO. Huo ndio UNAFIKI wa serikali na viongozi wetu wa sasa.

Dini nyingi zinakataza kushangilia tatizo au kifo cha jirani yako lakini silka ya Ubinadamu haikatazi kuonyesha hisia zako kwa jambo lililokufurahisha au kukusikitisha, KWA UPANDE WANGU WENYE KUFURAHI NAWAFURAHI NA WENYE KUHUZUNIKA NA WAUZUNIKE, Si MEMBE wala serikali wasituamulie ktk hili, maana walipouwawa watanzania wenzetu na serikali hihi hihi HAWAKUTUAMBIA TUSIKITIKE NA TUSHUSHE BENDERA, KAUWAWA MTU WANAEKAA NAE VIKAONI NA KUFANYA NAE MAAMUZI YA BARA LA AFRIKA( YAANI KIONGOZI MWENZAO)BILA KUJALI UBAYA WAKE NA ROHO MBAYA YAKE NA KUWA ALISHIRIKI KTK UVAMIZI WA NCHI YETU NA KUSABABISHA ROHO ZA WATZ ZIPOTEE WANATUTAKA TUUDHUNIKE NASEMA HAPANA TUACHE UNAFIKI wenye furaha na afurahi na wenye huzuni na auzunike Si MEMBE wala SERIKALI wenye haki ya kutuamulia wapi tufurahi na wapi tuuzunike.
 
Naloli,
Hili sii swla la silka ya binadamu, tunazungumzia sheria na UTU wa mwanadamu..Ghadaff ailikuwa na makosa yake na ndio maana kaondolewa madarakani. Kuondolewa kwake ni swala la Walibya kama lilivyo swala hili lakini kwa nini wewe unashangilia mahala ambapo sheria haikutumika maana kinachoweza kutuunganisha sisi na Walibya ktk swala hili ni kuzama sheria zinasema nini?
Hivyo kwa mtu yeyote anayekiuka sheria iwe Ghadaff au NTC hatuwezi kumuunga mkono tu kwa sababu hatumpendi mtu wa upande wa pili kama wanavyofanya Marekani na nchi za magharibi. Na afadhali wao wanafanya Urafiki na nchi hizi kwa maslahi yao wakati wewe na mimi urafiki wa maslahi hatuoni sababu..

Watu wengi hapa JF wametumia sababu ya Membe kumpenda Ghadaff ni kwa sababu ya misaada alotupa na interest zetu lakini wanashindwa kuelewa kwamba kama Ghadaff huyo huyo angeweza kukidhi interest za nchi za magharibi angeendelea kutawala kwa mika amingine na pengine hata kumwachia mwanaye kwani sii wa kwanza kufanya hivyo kinyume cha fikra tulopandikizwa..

Maneno yako ya kwamba ukiua kwa upanga nawe utauawa kwa upanga ni maneno mazito sana! na siodhani kama unayazungumza kwa kutumia sheria ama hisia zako lakini kama kweli unaamini aliyeua kwa Upanga anatakiwa kuuawa kwa upanga bila kufuata taratibu za kisheria, basi ya nini tunakuwa na mahakama? ya nini watu mnasomea sheria ili hali mwanadamu anaweza kufanya maamuzi haya pale inapompendeza...
 
Pasco, nimeisoma kwa umakini sana thread iliyopo hapo juu. Kwanza umeanza kwa kumshambulia Membe kuwa ameumbuka. Naweka maneno uliyoyaandika mwenyewe "Benard Membe leo umeumbuka. Alisema nchi haiwezi kutetwa kwa PICK UP. Libya imetekwa sasa kwa PICK UP. God bless libya"
Pili, ukatuhabarisha kuwa Waziri huyo ametoa msimamo wa nchi kuhusu kifo cha Gaddafi. Ukanukuu baadhi ya maneno aliyotamka wakati anatoa msimamo huo. (soma kuanzia 1-5 hapo juu).
Ukaendelea kumnukuu Mhe. Membe kwa sifa mbali mbali alizozitoa kwa marehemu Col. Muammar Gaddafi, na baada ya hapo ukatuambia yale ya kutoka moyoni mwako (soma MY TAKE hapo juu). Mwishoni ukaungana na Mhe. Membe kutofurahishwa na kifo cha Col. Gaddafi.

Wamejitokeza wachangiaji kadhaa ktk thread hii. Nitayachambua mawazo ya kila mmoja, na hasa wale wanaoona kuwa ilikuwa ni sahihi kwa Col. Gaddafi kuuliwa, na pili kwa wale wenye mawazo ya tofauti na msimamo aliyouweka Mhe. Membe.

Nikianza na wewe mtoa hoja, naomba utuambie kwanza, ktk kutoa hoja hii, lengo lako hasa lilikuwa nini????? Nauliza hivi kwa sababu sentensi yako ya kwanza hailingani na zile zinazofuatia.
Chechetuka, asante kwa agalizo hilo, hiyo sentensi ya kwanza siyo yangu, ni mode ameunganisha threads bila attribution, na kwa kweli hakunitendea haki, haswa kwa kuzingatia, najipanga niwe mmoja wa wapiga debe la 'Membe for Presidency' 2015. Hiyo sentensi ya kwanza, itaniharibia!
 
Wakulu........ jmushi1, Nyamgluu (wee Mkuu usipotee namna hii), Ben, 1954, Bob Mkandara na Pasco....asanteni sana kwa fikra zenu kwenye huu mjadala..........mnanikumbusha mbali sana kwenye mijadala ya JF........keep it up!

Pamoja sana comrade Ogah!
 
Tatizo la Membe haamini katika nguvu ya umma, anaamini vifaru na mizinga! Historia inatamka wazi "PEOPLE CAN DEFEAT THE STRONG ARMY". Tanzania ina Defence Force haina ARMY, kwa hiyo wananchi tukiamua tunaweza kumtoa fisadi kwa marungu na mishare tu siyo Pick-up tena. Aibu imrudie Mende kwa kutotambua Nguvu ya Umma iliyomkimbiza Quaddafi Tripoli.
aake dafi alikuwa baba y

yaani membe analia lia as if Gadafi aikuwa babake..hovyo sana hili lizee..yaani we jitu lilikuwa dikteta unalitetea..kwanza MTC wameniudhi gadafi alikuwa wa kutoa utumbo na kuutundika barabarani mainzi yale
 
hata sisi hapa wananchi nawagawiwa vyandarua vya bure lakini wanaichukia serikari (ref. Igunga as a sample), nami pia nauona mwanga katika mawazo ya Mzee Mwanakijiji
Nimeipenda. Yaani hapo sina swali. Ndiyo maana nami nilitoa mfano wa wanawake wanaomshangaa mwenzao anayedai talaka wakati anabadilisha magari ya kutembelea siku zote saba za wiki na huvaa dhahabu mwili mzima za gharama kubwa.. Asante mzee mwanakijiji..
 
Watanzania wanaomlilia zaidi Gaddafi ni wa CCM na BAKWATA na sababu ni dhahiri..........kukinga bakuli
 
Hivi Pasco mwaka ule tunapigana vita na Nduli Amin Gaddaf unajua nini ulilkuwa mchango wake kwenye ile vita ? Kweli wenye njaa hawaoni aibu .Mbele ya Mwalimu Gaddafi si kitu we all know ubafya wa Gaddafi sijaona ushujaa wake .
Membe mnafiki hawafurahii damu kila siku polisi wanaua watu Tanzania huko migodini na kwingineko hadi Kombe na watu wameachiwa .Aseme wageni wakifa yeye anaumia kana Gaddafi na Mchina wa juzi .
Mkuu Lunyungu, mtu anahukumiwa kwa aliyoyafanya kale ama alivyotubu kabla ya mauti kumkuta?.
A friend in need is a friend in deed!. 1978-79 Ghadafi ilikuwa rafiki na Amin, na kama true friend, alimsaidia na huu ndio urafiki wa kweli.
Jee unajua baada ya vita Ghadafi alimuomba vipi msamaha Mwalimu?, jee mnajua ni Libya ndio iliyolipia reparations za vita ile?.
Kwenye politics, hakuna permanent friends or permanent enemies, kuna only common interest, hivyo Ghadafi ilikuja kuwa rafiki mwema mara 100 ya hawa wazungu ambao tunawalamba miguu kila kukicha!.

Nilicomment kwa Mzee Mwanakijiji kuhusu the true reasons behind ambazo naamini hata wewe Mkuu Lunyungu naamini unazijua.

Sijasema ghadafi ni malaika, bali nimemuunga mkono Waziri Membe just kwa kumrecognize Ghadaf kwa wema aliotutendea, japo recognition hiyo imekuja too late!.

Mzee Lunyungu, mimi nimefanya kazi na wazungu hawa, tena kazi nyingine za jikoni kabisa agains us uli tuu mkono uende kinywani, amini nawaambie, wazungu hawa sii wema kwetu, hawako genuine, wana agenda zao!. Ghadafi was a true African patriot for African cause. Alijipanga kuukomesha ukiritimba wa IMF na World Bank kucontrol uchumi wa dunia kwa kuanzisha AMF na AB.

Naunga mkono kuwa watu wa kusamehe na kutokuweka kumbukumbu ya mabaya, na badala yake kuwa watu wa shukrani kwa kuweka kumbukumbu ya mema.

RIP Ghadafi.

Pascal.
 
Membe yeye alituambi kwamba kila mwezi alikuwa anakwenda Tripol! hivyo alichokisema pale sio msimamo wa Tanzania bali ni hisia zake ambazo zilikuwa zinasukumwa na chochote alichokuwa akipewa na Mh. Col. M.G!
 
izekomedioct2411.jpg
 
@ Jayfour_King unasema Gaddafi ameponzwa na kutaka kuundwa kwa United States of Africa,ili wazungu wasiweze kirahisi kuchukua rasilimali za Afrika,unaamini kitu kama hicho kwa moyo na dhati kabisa? Kama muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni matatizo matupu,kama shirikisho la kisiasa la EAC sisi Watanzania ndiyo tunaongoza kulipinga kwasababu za msingi na nyingine za uwoga tu,itakua eti Afrika kuwa na serikali moja? Kama yeye alishindwa washawishi majirani zake hata mmoja kuungana nae,utanishawishi vipi kwamba angeweza hiyo ndoto ya USA? Huu ni mfano tu wa ulevi wa madaraka na fedha za Walibya aliokua nao Gaddafi. Wewe mwenyewe moyoni unajua tofauti zetu kubwa tulizonazo hiyo haiwezekani!
 
Back
Top Bottom