ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 79,084
- 84,976
My Take
Samia ataendelea kusalia kama Rais aliyefanikiwa sana kwenye nyanja ya Uchumi na biashara hapa Tanzania.
Mageuzi aliyoyafanya kwenye mashirika haya ya Umma yamefaulu ,hatutegemei tena hasara huko tuendko.
Bado mashirika machache sana mfano Air Tanzania na TTCL.
Pia soma Ojambi Masaburi: Rais Samia amebadili historia mbaya ya Tanesco kutoka kuleta hasara hadi kuingiza na kutoa gawio kwa Serikali | JamiiForums Ojambi Masaburi: Rais Samia amebadili historia mbaya ya Tanesco kutoka kuleta hasara hadi kuingiza na kutoa gawio kwa Serikali
================
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imesema imeridhishwa na hali ya uzalishaji wa umeme , ambapo sasa nchi ina uwezo wa kuzalisha jumla ya megawati 4,400 huku matumizi yakiwa ni megawati 2,071 hatua ambayo imeendelea kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme.
Hayo yamejiri Februari 20,2026 baada ya Kamati hiyo kufanya ziara ya kukagua miradi ya umeme katika Mkoa wa Dar es Salaam, ambapo imetembelea Kituo cha Kusafirisha Umeme kwenda Zanzibar cha Ras Kilomoni na Kituo cha kuzalisha Umeme kwa Gesi Asilia cha Kinyerezi I na II.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Subira Mgalu, amesema kumekuwa na maendeleo makubwa katika eneo la uzalishaji wa umeme, na sasa TANESCO inaendelea na jitihada za kujenga njia za kusafirisha umeme, ikiwemo ya kutoka Bwawa la Julius Nyerere hadi Chalinze, kisha Kinyerezi hadi Mkuranga, eneo lenye viwanda vingi vya uzalishaji.
“Tunaipongeza sana TANESCO kwa utekelezaji wa miradi ya umeme. Ile hali ya kukatika kwa umeme imepungua, na sasa hakuna mgao. Kamati inashauri kuwa nguvu kubwa sasa itumike katika kuhakikisha umeme unamfikia mlaji wa mwisho, hususani katika maeneo ya viwanda na migodi,” alifafanua Subira.
Samia ataendelea kusalia kama Rais aliyefanikiwa sana kwenye nyanja ya Uchumi na biashara hapa Tanzania.
Mageuzi aliyoyafanya kwenye mashirika haya ya Umma yamefaulu ,hatutegemei tena hasara huko tuendko.
Bado mashirika machache sana mfano Air Tanzania na TTCL.
Pia soma Ojambi Masaburi: Rais Samia amebadili historia mbaya ya Tanesco kutoka kuleta hasara hadi kuingiza na kutoa gawio kwa Serikali | JamiiForums Ojambi Masaburi: Rais Samia amebadili historia mbaya ya Tanesco kutoka kuleta hasara hadi kuingiza na kutoa gawio kwa Serikali
================
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imesema imeridhishwa na hali ya uzalishaji wa umeme , ambapo sasa nchi ina uwezo wa kuzalisha jumla ya megawati 4,400 huku matumizi yakiwa ni megawati 2,071 hatua ambayo imeendelea kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme.
Hayo yamejiri Februari 20,2026 baada ya Kamati hiyo kufanya ziara ya kukagua miradi ya umeme katika Mkoa wa Dar es Salaam, ambapo imetembelea Kituo cha Kusafirisha Umeme kwenda Zanzibar cha Ras Kilomoni na Kituo cha kuzalisha Umeme kwa Gesi Asilia cha Kinyerezi I na II.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Subira Mgalu, amesema kumekuwa na maendeleo makubwa katika eneo la uzalishaji wa umeme, na sasa TANESCO inaendelea na jitihada za kujenga njia za kusafirisha umeme, ikiwemo ya kutoka Bwawa la Julius Nyerere hadi Chalinze, kisha Kinyerezi hadi Mkuranga, eneo lenye viwanda vingi vya uzalishaji.
“Tunaipongeza sana TANESCO kwa utekelezaji wa miradi ya umeme. Ile hali ya kukatika kwa umeme imepungua, na sasa hakuna mgao. Kamati inashauri kuwa nguvu kubwa sasa itumike katika kuhakikisha umeme unamfikia mlaji wa mwisho, hususani katika maeneo ya viwanda na migodi,” alifafanua Subira.