Serikali: Shy-Rose hakupigana Kenya

Serikali: Shy-Rose hakupigana Kenya

Nderakindo amkana Samuel Sitta; Nderakindo amkana Samuel Sitta - Kitaifa - mwananchi.co.tz

Dodoma. Wakati Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta akisema ofisi yake imewakutanisha na kumaliza mgogoro baina ya wabunge wawili wa Bunge la Afrika Mashariki (Eala), mmoja wa wabunge hao, Dk Nderakindo Kessy amesema hakuna kitu kama hicho.
 
Sasa kilicho mpelekea kulala rumande ni kitu gani? Ai alikosa nyumba ya wageni? Kila kitu hata ambavyo vinaonekana Nyie ni kikanusha tuu. Vijikaratasi vya kufunga maandazi vinaibomoa serikali yaCcm. Aibuuu

Ni wapi serikali imsema alilala rumande? Mtu umeambiwa hakupigana tena kwa tamko la serikali.Sasa kama hakupigana ulitegemea serikali ya Kenya imuweke rumande?
 
Ni wapi serikali imsema alilala rumande? Mtu umeambiwa hakupigana tena kwa tamko la serikali.Sasa kama hakupigana ulitegemea serikali ya Kenya imuweke rumande?

Wewe mtetee tu...

Nairobi.

Kenyan police are investigating an incident in which a Tanzanian member of the East African Legislative Assembly (Eala) allegedly assaulted a fellow lawmaker and compatriot in Nairobi on Tuesday.

Ms Shy-Rose Bhanji allegedly confronted and hit Dr Nderakindo Kessy outside the debating chamber. Ms Bhanji could not be reached for comment yesterday.


Eala insiders linked the incident with the dispute pitting members who want to oust Eala Speaker Margaret Zziwa against those supporting the embattled Ugandan head of the assembly.


Ms Zziwa, who was elected in 2012, has since earlier this year been battling accusations of incompetence, nepotism and intimidation of lawmakers and staff.


Dr Kessy said in the statement she recorded at Parliament Police Station that Ms Bhanji attacked her shortly after the assembly was adjourned following its official opening on Tuesday.


Eyewitnesses, including some Eala MPs, said Ms Bhanji first elbowed Dr Kessy as they filed out of the hall.

Dr Kessy told The Citizen by telephone yesterday that was treated at a nearby hospital and her back was still painful.


On Monday, Dr Kessy read out a resolution in which some MPs vowed to continue with their push to remove the Speaker and punish Ms Bhanji for alleged misconduct.

Dr Kessy is the secretary of the “Crisis Committee” formed by some Eala MPs in Kigali last month to push for the removal of Ms Zziwa as speaker and Ms Bhanji from the Eala Commission.


Tanzanian MPs are required to reach a consensus on the leadership crisis and the pending motion to remove Ms Bhanji as a commission member.


Ms Bhanji was accused, among other things, of being drunk and disorderly, on a flight to Brussels last month, but she said in Dar last week that her detractors had not put the accusations in writing and were just engaging in “gossip”.



“If indeed I was drunk and violent on the plane, I would have been arrested and charged in accordance with international air safety regulations. This did not happen…these allegations are false. This is part of a character assassination plot that is now in top gear following my refusal to be part of the group that wants to impeach Zziwa,” she said.

Nation Publishers
 
kwa hiyo kama ni jembe, ndio afanye hayo madudu? au unataka kutuaminisha huwa wanamfuata chumbani na kumpeleka kituo cha polisi? Kama ni jembe hebu nipe hoja moja tu amabayo aliitoa na ikaleta manufaa kwenye nchi hizi za afrika mashariki, isiwe kupinga kila hoja ndio ujasiri tu.
alipinga hoja ya suala la ardhi kuwa la Afrika Mashariki na siyo nchi washirika, na mpaka leo ni hivyo. Mkenya hawezi kuja kumiliki eneo huku Bongo, ila anaweza kulitumia kwa shughuli za kiuchumi tu na ni kwa mda maalum tu! Hivyo basi nampongeza sana mama huyu, anaweka maslahi ya taifa mbele halafu ya EAC baadaye!
 
Nderakilo-Kessy--November21-2014.jpg

Mbunge wa bunge la Afrika Mashariki Nderakindo Kessy

Serikali imetoa kauli bungeni, ikisema Mbunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Shyrose Bhanji, hakumpiga Mbunge mwenzake Nderakindo Kessy (pichani), bali Bunge hilo lina mgogoro ambao, kiini chake ni Spika wa Bunge hilo,Magreth Zziwa.

Hayo yalielezwa jana na Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, akitoa taarifa bungeni baada ya Khatib Said Haji (Konde-CUF), kuomba mwongozo wa Spika, kuhusu kinachoendelea kwenye Bunge hilo.

Sitta alisema: "Kinachotokea katika AELA kwa kiasi kikubwa kinahusu mgogoro wa Spika mwenyewe, ndiye chanzo cha matatizo mengi ambayo yamegawa bunge hilo katika makundi makuu mawili."

Alitaja makundi hayo kuwa ni linalotaka spika huyo aondolewe kwa madai kwamba hafai, huku lingine likimtetea abaki.

Alisema Tanzania inaonekana kuwa kikwazo katika mkakati wa kumuondoa Zziwa.

Alisema ili Bunge hilo liamue jambo lolote, lazima akidi ipatikane katika kila nchi na kwamba awali Tanzania waliunga mkono aondolewe, lakini sasa, wamekuwa na msimamo tofauti na kusababisha kuwapo aina fulani ya chuki.

"Kilichotokea kati ya Bhanji na Kessy, siyo kinavyoelezwa kwani Bhanji anahesabika kuwa ni shabiki mkubwa wa Spika, kiasi cha wenzake kumuona kama kibaraka vile," alieleza Sitta.

Alielezea kuwa madai ya Kessy kupigwa yalitokana na Bhanji kugongana naye kwa bahati mbaya wakati akiwahi usafiri, akipita katikati ya wabunge wenzake,Alisema mgongano huo ulitafsiriwa na Kessy kuwa ni shambulio, ambaye alihamaki na kwa kusaidiwa na baadhi ya Wabunge wa Uganda, akaenda polisi na kumtuhumu Bhanji kwamba amemtendea kosa la jinai.

Alisema hata hivyo, kwa jitihada za uongozi wa EALA, mpaka jana suala hilo halimo mikononi mwa polisi tena bali limemalizwa ndani ya Bunge.

Sitta alizungumzia madai mengine dhidi ya Shyrose kwamba alifanya mambo ya ‘ovyo' takriban miezi miwili iliyopita kwamba bado yapo mikononi mwa Tume ya EALA, itakapomaliza kulishughulikia litatolewa taarifa.

"Kwa sasa hatuwezi kufanya lolote, mpaka tutakapopata taarifa kutoka EALA, nikizipata nitaziwasilisha kwa Spika wetu na hapo ndipo sisi kama jimbo la uchaguzi tutakapojadili kuona ukweli ni upi na kuamua hatua za kuchukua," alieleza Sitta.

Chanzo
:Nipashe
 
alipinga hoja ya suala la ardhi kuwa la Afrika Mashariki na siyo nchi washirika, na mpaka leo ni hivyo. Mkenya hawezi kuja kumiliki eneo huku Bongo, ila anaweza kulitumia kwa shughuli za kiuchumi tu na ni kwa mda maalum tu! Hivyo basi nampongeza sana mama huyu, anaweka maslahi ya taifa mbele halafu ya EAC baadaye!
Hiyo hoja haiwezi kuzuia mtu anaetaka kumiliki ardhi ashindwe, wapo wengi tu wamenunua ardhi kwa pesa zao na wamejenga mpaka hoteli huko meserani Arusha tunawajua, ukiwa na hela nchi hii hakuna kinachoshindikana, mradi watanzania hatuna vitambulisho, na ukinunua ardhi huulizwi umezaliwa wapi.
 
Kwa nini kila siku anasemwa Shyrose Bhanji na sio wabunge wengine kutoka Tanzania. Mimi ninaamini kuna tatizo hapo japo wakubwa wanalitetea.
 

Mimi sio Pro SHYROSE... Lakini hapo inaonyesha hawa Wabunge wa nchi JIRANI i.e UGANDA; RWANDA; KENYA wanatafuta sababu za kutuondolea Umoja wetu...

Ni Wabunge 7 tu kati ya 9 wa TANZANIA ndio wanaomkubali Madame Speaker.. Sasa wanatafuta visa kuwachafua baadhi na wanaona SHYROSE being not 100% ndio wa ku attach hana nguvu... hawakujua kuwa Tanzania NYERERE alituelimisha BILA MATABAKA kama hizo nchi zao...
 
Kwa nini kila siku anasemwa Shyrose Bhanji na sio wabunge wengine kutoka Tanzania. Mimi ninaamini kuna tatizo hapo japo wakubwa wanalitetea.

Hao waafrika wa UGANDA RWANDA na KENYA wana ule UKOLONI kuwa BIAS na ku attach a weakest point yao ni Rangi ya SHYROSE sababu wabunge 7 wa Tanzania wako Upande wa SPEAKER
Shakidinkili
 
Kama unaweza kuwa pigisha kura watu waliokufa utashindwa kuja kuongea utumbo kama huu... Sitta angejikali kimya, ni mtu mzima lakini ni mkosa akili sana, kwa ulaghai aliofanya katika kura za katiba pendekezwa kwa sasa angekuwa ananya debe kwa nchi zenye utawala wa kisheria ... kajishushia sana heshima yake, hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kumsiliza huyu ....
 
Mwanzo » Habari


NA MWANDISHI WETU



21st November 2014


Nderakilo-Kessy--November21-2014.jpg

Mbunge wa bunge la Afrika Mashariki Nderakindo Kessy


Serikali imetoa kauli bungeni, ikisema Mbunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Shyrose Bhanji, hakumpiga Mbunge mwenzake Nderakindo Kessy (pichani), bali Bunge hilo lina mgogoro ambao, kiini chake ni Spika wa Bunge hilo,Magreth Zziwa.


Hayo yalielezwa jana na Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, akitoa taarifa bungeni baada ya Khatib Said Haji (Konde-CUF), kuomba mwongozo wa Spika, kuhusu kinachoendelea kwenye Bunge hilo.


Sitta alisema: “Kinachotokea katika AELA kwa kiasi kikubwa kinahusu mgogoro wa Spika mwenyewe, ndiye chanzo cha matatizo mengi ambayo yamegawa bunge hilo katika makundi makuu mawili.”


Alitaja makundi hayo kuwa ni linalotaka spika huyo aondolewe kwa madai kwamba hafai, huku lingine likimtetea abaki.


Alisema Tanzania inaonekana kuwa kikwazo katika mkakati wa kumuondoa Zziwa.


Alisema ili Bunge hilo liamue jambo lolote, lazima akidi ipatikane katika kila nchi na kwamba awali Tanzania waliunga mkono aondolewe, lakini sasa, wamekuwa na msimamo tofauti na kusababisha kuwapo aina fulani ya chuki.


“Kilichotokea kati ya Bhanji na Kessy, siyo kinavyoelezwa kwani Bhanji anahesabika kuwa ni shabiki mkubwa wa Spika, kiasi cha wenzake kumuona kama kibaraka vile,” alieleza Sitta.


Alielezea kuwa madai ya Kessy kupigwa yalitokana na Bhanji kugongana naye kwa bahati mbaya wakati akiwahi usafiri, akipita katikati ya wabunge wenzake,Alisema mgongano huo ulitafsiriwa na Kessy kuwa ni shambulio, ambaye alihamaki na kwa kusaidiwa na baadhi ya Wabunge wa Uganda, akaenda polisi na kumtuhumu Bhanji kwamba amemtendea kosa la jinai.


Alisema hata hivyo, kwa jitihada za uongozi wa EALA, mpaka jana suala hilo halimo mikononi mwa polisi tena bali limemalizwa ndani ya Bunge.


Sitta alizungumzia madai mengine dhidi ya Shyrose kwamba alifanya mambo ya ‘ovyo’ takriban miezi miwili iliyopita kwamba bado yapo mikononi mwa Tume ya EALA, itakapomaliza kulishughulikia litatolewa taarifa.


“Kwa sasa hatuwezi kufanya lolote, mpaka tutakapopata taarifa kutoka EALA, nikizipata nitaziwasilisha kwa Spika wetu na hapo ndipo sisi kama jimbo la uchaguzi tutakapojadili kuona ukweli ni upi na kuamua hatua za kuchukua,” alieleza Sitta.






CHANZO: NIPASHE




Kumbe pia alifanya mambo ya hovyo takribani miezi michache iliyopita!Hivi kwa akili ya darasa la kwanza,inakuwaje apite katikati ya wabunge wengine alafu amgonge adui wake?eti alikuwa anawahi usafiri kwa hiyo alikuwa anakimbia?alikuwa anakimbilia hiace?mimi ninaona huyo Shyrose anafaa zaidi kuwa mhudumu wa baha awe anashikwa makalio.
 
Hiyo hoja haiwezi kuzuia mtu anaetaka kumiliki ardhi ashindwe, wapo wengi tu wamenunua ardhi kwa pesa zao na wamejenga mpaka hoteli huko meserani Arusha tunawajua, ukiwa na hela nchi hii hakuna kinachoshindikana, mradi watanzania hatuna vitambulisho, na ukinunua ardhi huulizwi umezaliwa wapi.

Kama hilo halitekelezeki basi siyo kosa lake Shy Rose. Ni uzembe wetu sisi watanzania. Yeye kama mbunge wa Tanzania huko EALA ameshafanya part yake!
 
kwa hiyo kama ni jembe, ndio afanye hayo madudu? au unataka kutuaminisha huwa wanamfuata chumbani na kumpeleka kituo cha polisi? Kama ni jembe hebu nipe hoja moja tu amabayo aliitoa na ikaleta manufaa kwenye nchi hizi za afrika mashariki, isiwe kupinga kila hoja ndio ujasiri tu.

Wewe personally una evidence kuwa kafanya hayo madudu? au unasikia tu na kulipuka.
 
Ngoja ije ithibitike kuwa alipigana sijui huyu mwendawazimu Sita ataficha wapi uso wake.
 
Back
Top Bottom