Serikali: Shy-Rose hakupigana Kenya

Serikali: Shy-Rose hakupigana Kenya

msemakweli

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2014
Posts
1,627
Reaction score
880
SERIKALI imesema Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Shy-Rose Bhanji hajapigana nchini Kenya, na wanasubiri Tume ya EALA ili kujua ukweli wa tuhuma zinazoelekezwa kwake.

Kwa muda sasa, Shy-Rose amekuwa katika mzozo na wabunge wenzake wa EALA, kwanza akituhumiwa kuwatukana wakiwa safarini Ubelgiji na juzi akituhumiwa kupigana na mwenzake kutoka Tanzania, Dk Nderakindo Kessy.

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta awali alilieleza Bunge jana mjini hapa kuwa kiini cha mzozo wote ni mgogoro dhidi ya Spika wa EALA, Margaret Zziwa wa Uganda.

Sitta alisema yapo makundi mawili sasa ndani ya Bunge hilo, moja likitaka kumng'oa Spika huyo na lingine likimkingia kifua kwamba hapaswi kuondolewa.

"Katika hili (la kumng'oa Spika), Tanzania ni kikwazo, kwa sababu ili Spika aondolewe ni lazima akidi itimie, na akidi hiyo ni kupata kuungwa mkono kwa idadi fulani ya wajumbe wa kila nchi. "Sasa Tanzania wamefuta hoja ya kutaka Spika huyo aondolewe na hii ndiyo imesababisha chuki yote," alieleza Sitta kabla ya kujibu hoja kuhusu Shy-Rose.

Sitta alisema Shy-Rose hakupigana au kumpiga mbunge mwenzake kama ilivyoandikwa katika magazeti jana.

Nderakilo-Kessy--November21-2014.jpg

Mbunge wa bunge la Afrika Mashariki Nderakindo Kessy

Serikali imetoa kauli bungeni, ikisema Mbunge wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Shyrose Bhanji, hakumpiga Mbunge mwenzake Nderakindo Kessy (pichani), bali Bunge hilo lina mgogoro ambao, kiini chake ni Spika wa Bunge hilo,Magreth Zziwa.

Hayo yalielezwa jana na Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, akitoa taarifa bungeni baada ya Khatib Said Haji (Konde-CUF), kuomba mwongozo wa Spika, kuhusu kinachoendelea kwenye Bunge hilo.

Sitta alisema: "Kinachotokea katika AELA kwa kiasi kikubwa kinahusu mgogoro wa Spika mwenyewe, ndiye chanzo cha matatizo mengi ambayo yamegawa bunge hilo katika makundi makuu mawili."

Alitaja makundi hayo kuwa ni linalotaka spika huyo aondolewe kwa madai kwamba hafai, huku lingine likimtetea abaki.

Alisema Tanzania inaonekana kuwa kikwazo katika mkakati wa kumuondoa Zziwa.

Alisema ili Bunge hilo liamue jambo lolote, lazima akidi ipatikane katika kila nchi na kwamba awali Tanzania waliunga mkono aondolewe, lakini sasa, wamekuwa na msimamo tofauti na kusababisha kuwapo aina fulani ya chuki.

"Kilichotokea kati ya Bhanji na Kessy, siyo kinavyoelezwa kwani Bhanji anahesabika kuwa ni shabiki mkubwa wa Spika, kiasi cha wenzake kumuona kama kibaraka vile," alieleza Sitta.

Alielezea kuwa madai ya Kessy kupigwa yalitokana na Bhanji kugongana naye kwa bahati mbaya wakati akiwahi usafiri, akipita katikati ya wabunge wenzake,Alisema mgongano huo ulitafsiriwa na Kessy kuwa ni shambulio, ambaye alihamaki na kwa kusaidiwa na baadhi ya Wabunge wa Uganda, akaenda polisi na kumtuhumu Bhanji kwamba amemtendea kosa la jinai.

Alisema hata hivyo, kwa jitihada za uongozi wa EALA, mpaka jana suala hilo halimo mikononi mwa polisi tena bali limemalizwa ndani ya Bunge.

Sitta alizungumzia madai mengine dhidi ya Shyrose kwamba alifanya mambo ya ‘ovyo' takriban miezi miwili iliyopita kwamba bado yapo mikononi mwa Tume ya EALA, itakapomaliza kulishughulikia litatolewa taarifa.

"Kwa sasa hatuwezi kufanya lolote, mpaka tutakapopata taarifa kutoka EALA, nikizipata nitaziwasilisha kwa Spika wetu na hapo ndipo sisi kama jimbo la uchaguzi tutakapojadili kuona ukweli ni upi na kuamua hatua za kuchukua," alieleza Sitta.


Chanzo
:Nipashe
 
SIASA BWANA UONGO HUWA KWELI NA KWELI HUWA UONGO
Ndugu zangu mnaotaka kujiingiza kwenye siasa kigezo cha kwanza ni kutokuwa na soni
 
SERIKALI imesema Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Shy-Rose Bhanji hajapigana nchini Kenya, na wanasubiri Tume ya EALA ili kujua ukweli

Sasa wakisema hakupigana(maana yake wana uhakika) na wanasubiri kujua ukweli,(maana yake hawajui kilichotokea), TZ viongozi wanakurupuka sana
 
Kama tanzania imekataa kuungana na wenzao kwa nini kila siku ni shyrose tu? kwani yeye ndio mbunge pekee wa kutoka tanzania? ficheni maovu yenu humu ndani, ila nje yatafichuliwa tu.
 
We bwana mdogo sita,watu hatu iman kabisaaa na hii serikali,hata Mr.tezi dume anajua hilo.
 
Mti wenye maembe ndio unaotupiwa mawe.Shyrose ni jembe.Usifanye mchezo.Ni mbunge anayejua kazi yake.Na hatishwi wala kutetereka.

kwa hiyo kama ni jembe, ndio afanye hayo madudu? au unataka kutuaminisha huwa wanamfuata chumbani na kumpeleka kituo cha polisi? Kama ni jembe hebu nipe hoja moja tu amabayo aliitoa na ikaleta manufaa kwenye nchi hizi za afrika mashariki, isiwe kupinga kila hoja ndio ujasiri tu.
 
SERIKALI imesema Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Shy-Rose Bhanji hajapigana nchini Kenya, na wanasubiri Tume ya EALA ili kujua ukweli wa tuhuma zinazoelekezwa kwake.....
Anasema hakupigana, ila pia anasubiri taarifa kujua ukweli!! Sasa kama anasubiri taarifa, iweje afanye ruling kwamba hakupigana?
 
SERIKALI imesema Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Shy-Rose Bhanji hajapigana nchini Kenya, na wanasubiri Tume ya EALA ili kujua ukweli wa tuhuma zinazoelekezwa kwake.
Ndio umekanusha nini sasa ikiwa hujui na kwamba unasubiri nawe uelezwe na waliokuwepo? Kwanini usisubiri hiyo tume kwanza ndipo uhitimishe? Hata hivyo hii sio habari tena. Habari ya mujini ni Escrow ya Tegeta.
 
Tumtazame kwa umakini Shujaa huyu Shai Rose, isije kuwa ana ushujaa unaowatisha maadui wa Utanzaniauliotukuka kizalendo zaidi. Tumsapoti hadi pale tutakapo dhibitisha kuwa ana kosa.
 
Huyu ndiye mzuri wa kuolewa , unakuwa ufungi milango kwani ni ulinzi tosha, akija mwizi unasema shy, shy shy miji, miji. Mwizi anatimka.
 
Ndio umekanusha nini sasa ikiwa hujui na kwamba unasubiri nawe uelezwe na waliokuwepo? Kwanini usisubiri hiyo tume kwanza ndipo uhitimishe? Hata hivyo hii sio habari tena. Habari ya mujini ni Escrow ya Tegeta.
Mh. Zitto anasema tena bungeni kuwa wizi wa escrow ac unaweza kutokea tu kwenye nchi isiyo na serikali mfano Somalia au Congo DRC. Sasa ni kweli umetokea Tanzania tayari na hiyo serikali iliyosimamia wizi huo ndio inatoa hili 'kanusho' ...unataka kithibitisho gani kuyaamini maneno ya Zitto!?

 
Sasa kilicho mpelekea kulala rumande ni kitu gani? Ai alikosa nyumba ya wageni? Kila kitu hata ambavyo vinaonekana Nyie ni kikanusha tuu. Vijikaratasi vya kufunga maandazi vinaibomoa serikali yaCcm. Aibuuu
 
huyu 6 nae anataka ku2fanya cc wajinga, kasema shy-rose hakupgana, sasa wanasubiri ripot ya nn wakat kasha conclude, duh
 
Mh. Zitto anasema tena bungeni kuwa wizi wa escrow ac unaweza kutokea tu kwenye nchi isiyo na serikali mfano Somalia au Congo DRC. Sasa ni kweli umetokea Tanzania tayari na hiyo serikali iliyosimamia wizi huo ndio inatoa hili 'kanusho' ...unataka kithibitisho gani kuyaamini maneno ya Zitto!?


Mkuu kwenye post yangu sidhani kama niliungana na mkanushaji, na wala sidhani kama nilihitaji uthibitisho zaidi ya kumtaka mkanushaji asubiri taarifa kwanza ndipo afanye ruling. May be you misquoted me Sir.
 
The government need to stick on principles rather than favouritism. The statement shows that government stands with Shyrose and it has issued a historic background to support its stance. That tell every one that rule of law, leadership principles and standards are not to be abided by some people. This amount to impunity and rise of "mafia" law in our society
 
Back
Top Bottom