PostGE2025 Serikali yatoa ufafanuzi uteuzi wa Angela Kizigha kuwa Mbunge, yadai taarifa ya LHRC ni potofu

PostGE2025 Serikali yatoa ufafanuzi uteuzi wa Angela Kizigha kuwa Mbunge, yadai taarifa ya LHRC ni potofu

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,665
Reaction score
15,554
Serikali imetoa ufafanuzi kwa umma kufuatia taarifa iliyoelezwa kuwa potofu iliyotolewa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kuhusu uteuzi wa Mbunge uliofanywa na Rais Samia Aprili 2, 2026 chini ya Ibara ya 66(1)(e) ya Katiba.

KIZIGHA JF.jpg
Katika ufafanuzi huo, Serikali imeeleza kuwa ni kweli kwamba kabla ya uteuzi huo, Angela Kizigha alikuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA). Hata hivyo, imefafanua kuwa kwa mujibu wa Ibara ya 51(3)(c) ya Mkataba wa Kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mbunge wa EALA hukoma kushika nafasi hiyo pindi anapoteuliwa kuwa Mbunge wa Bunge la nchi mwanachama.

Soma: LHRC: Uteuzi wa Angela Kizigha kuwa Mbunge unavunja masharti ya mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Kutokana na masharti hayo ya kisheria, Serikali imebainisha kuwa ubunge wa EALA kwa Mheshimiwa Angela Kizigha, pamoja na Waheshimiwa Dkt. Ngwaru Maghembe na James Milya, ulikoma mara baada ya kuteuliwa au kuchaguliwa kuwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Serikali imeeleza kuwa kwa mujibu wa Ibara ya 50 ikisomwa pamoja na Ibara ya 52 ya Mkataba huo, Bunge la nchi mwanachama lina mamlaka ya kujaza nafasi zilizo wazi katika Bunge la Afrika Mashariki kulingana na ratiba zake na taratibu husika.

Tazama alivyoapishwa: Angela Kizigha na Dkt. Evaline Munisi waapishwa kuwa Wabunge wa Bunge la Tanzania, Aprili 9, 2026

Kwa msingi huo, Bunge la Tanzania linatarajiwa kujaza nafasi tatu zilizoachwa wazi, kwa kuzingatia ratiba ya shughuli za Bunge. Serikali imeongeza kuwa mchakato huo utaanzia katika vyama vya siasa ili kukidhi matakwa ya Ibara ya 50(1) ya Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Serikali imesisitiza kuwa hakuna mgongano wowote kati ya uteuzi uliofanywa chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na masharti ya Mkataba wa Kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Hivyo basi, wananchi wamehimizwa kupuuza taarifa iliyotolewa na LHRC kuhusu suala hilo, kwa kuwa si tafsiri sahihi ya masharti ya Mkataba huo.

1775801649509.png
 
Serikali imetoa ufafanuzi kwa umma kufuatia taarifa iliyoelezwa kuwa potofu iliyotolewa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kuhusu uteuzi wa Mbunge uliofanywa na Rais Samia Aprili 2, 2026 chini ya Ibara ya 66(1)(e) ya Katiba.

Katika ufafanuzi huo, Serikali imeeleza kuwa ni kweli kwamba kabla ya uteuzi huo, Angela Kizigha alikuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA). Hata hivyo, imefafanua kuwa kwa mujibu wa Ibara ya 51(3)(c) ya Mkataba wa Kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mbunge wa EALA hukoma kushika nafasi hiyo pindi anapoteuliwa kuwa Mbunge wa Bunge la nchi mwanachama.

Soma: LHRC: Uteuzi wa Angela Kizigha kuwa Mbunge unavunja masharti ya mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Kutokana na masharti hayo ya kisheria, Serikali imebainisha kuwa ubunge wa EALA kwa Mheshimiwa Angela Kizigha, pamoja na Waheshimiwa Dkt. Ngwaru Maghembe na James Milya, ulikoma mara baada ya kuteuliwa au kuchaguliwa kuwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Serikali imeeleza kuwa kwa mujibu wa Ibara ya 50 ikisomwa pamoja na Ibara ya 52 ya Mkataba huo, Bunge la nchi mwanachama lina mamlaka ya kujaza nafasi zilizo wazi katika Bunge la Afrika Mashariki kulingana na ratiba zake na taratibu husika.

Tazama alivyoapishwa: Angela Kizigha na Dkt. Evaline Munisi waapishwa kuwa Wabunge wa Bunge la Tanzania, Aprili 9, 2026

Kwa msingi huo, Bunge la Tanzania linatarajiwa kujaza nafasi tatu zilizoachwa wazi, kwa kuzingatia ratiba ya shughuli za Bunge. Serikali imeongeza kuwa mchakato huo utaanzia katika vyama vya siasa ili kukidhi matakwa ya Ibara ya 50(1) ya Mkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Serikali imesisitiza kuwa hakuna mgongano wowote kati ya uteuzi uliofanywa chini ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na masharti ya Mkataba wa Kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Hivyo basi, wananchi wamehimizwa kupuuza taarifa iliyotolewa na LHRC kuhusu suala hilo, kwa kuwa si tafsiri sahihi ya masharti ya Mkataba huo.

Walitakiwa kutoa ufafanuzi huu kwenye taarifa ya uteuzi kuondoa maswali yote.
 
Walitakiwa kutoa ufafanuzi huu kwenye taarifa ya uteuzi kuondoa maswali yote.
Lakini pia inashangaza LHRC Kama hawakuona hiki kipengele cha mkataba wa EAC kabla ya kuja na zile tuhuma.
 
Watoe ufafanuzi pia silaha za kuuwa watanzania October 29 alizinunua nani
Kweli nimeamini hakuna aijuaye kesho yake!! Etwege uliyekua ukishangilia upotevu na mauaji ya watu enzi za KAYAFA aka JIWE Leo umekua upande wa wanaolia Lia!! Wakati ule tunalia juu ya mateso ya Lissu kupigwa risasi ulikua ukishangilia na kuhanikiza mateso zaidi juu yake Leo Upo unalia Lia!! Ni kilio cha binadamu hiki au ni machozi ya Mamba????
 
Walimteuaje bila kutengeua nafasi yake kwanza?. Kazi na utu tunasonga mbele na mama.
Nani anatengua? Hivi wabongo mnakuaga na audacity hata kidogo ya kutafuta facts before muongee?
 
Alipaswa kujiuzulu kwanza EALA ndipo uteuzi ufate.
Mkataba unasema akiteuliwa au kuchaguliwa mbunge wa nchi mwanachama. “Automatically” huo ubunge wa EALA unakoma! Umeona kipengele cha kumtaka ajiuzulu kwanza???
 
Lakini pia inashangaza LHRC Kama hawakuona hiki kipengele cha mkataba wa EAC kabla ya kuja na zile tuhuma.
LHRC waliitaka serikali kutoa ufafanuzi, kuona au kutoona kile kipengele hakubadilishi kitu kwa sababu taarifa ya uteuzi iliacha ombwe. LHRC imetusaidia kuilazimisha serikali kutoa taarifa kwamba hawa watu hawataendelea kuwa wabunge wa Bunge la Afrika ya Mashariki.

Kwa serikali ya sasa na teuzi za kuzisikia redioni hata kwa wanaoteuliwa, inawezekana watu wa serikali wenyewe walikuwa hawajafuatilia vifungu na kufanya ombwe hili pengine liwepo hata serikalini.

Certainly ombwe hili lilikuwepo katika taarifa ya uteuzi, ambayo kawaida huweka wazi mteule alikuwa na kazi gani kabla ya uteuzi, na pengine hata kueleza kuwa kazi hiyo itajazwa vipi.

Bado taarifa ya uteuzi ilikuwa na ombwe lililoifanya LHRC kutaka ufafanuzi, ukiisoma taarifa ya LHRC utaona imetaka ufafanuzi zaidi.

Ukisoma somo la Public Relations, kitu kimoja muhimu kinachosisitizwa katika kutoa taarifa ni kutoa taarifa itakayojibu maswali yote ya msingi tangu awali.

Taarifa ya uteuzi iliacha ombwe ambalo lilihitaji ufafanuzi kuliziba. Ndicho LHRC walichotaka.
 
Mkataba unasema akiteuliwa au kuchaguliwa mbunge wa nchi mwanachama. “Automatically” huo ubunge wa EALA unakoma! Umeona kipengele cha kumtaka ajiuzulu kwanza???
Taarifa ya uteuzi nayo ilitakiwa kusema kuwa awali huyu alikuwa mbunge wa bunge la Afrika ya Mashariki na baada ya uteuzi wa ubunge kwenye bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ubunge wake wa Bunge la Afrika Mashariki unakoma kwa mujibu wa kifungu hiki.

Moja kati ya kazi za hizi taarifa za teuzi ni kujibu maswali kabla hayajaulizwa.
 
Mkataba unasema akiteuliwa au kuchaguliwa mbunge wa nchi mwanachama. “Automatically” huo ubunge wa EALA unakoma! Umeona kipengele cha kumtaka ajiuzulu kwanza???
Unachanganya matokeo ya kisheria na sifa za Kuteuliwa.

Unaelewa nini kuhusu haya mambo mawili hapa?
 
Kweli nimeamini hakuna aijuaye kesho yake!! Etwege uliyekua ukishangilia upotevu na mauaji ya watu enzi za KAYAFA aka JIWE Leo umekua upande wa wanaolia Lia!! Wakati ule tunalia juu ya mateso ya Lissu kupigwa risasi ulikua ukishangilia na kuhanikiza mateso zaidi juu yake Leo Upo unalia Lia!! Ni kilio cha binadamu hiki au ni machozi ya Mamba????
Hatujashitakiwa MIGA?
 
Back
Top Bottom