Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Serikali kutafuta njia mbadala kushindwa kwa shule za kata
na Victor Masangu, Bagamoyo
SERIKALI imesema kwamba haijaridhishwa na matokeo ya shule za sekondari za kata ambazo zimefanya vibaya katika mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka 2010 huku shule binafsi zikiongoza.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Elimu Mafunzo na Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, wakati wa sherehe za mahafali ya tisa ya kidato cha sita yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Shule ya Sekondari Bagamoyo.
Dk. Kawambwa alisema serikali inatakiwa kuangalia kwa makini njia mbadala zinazotumika kufundishia wanafunzi wanaosoma katika shule za seminari.
Aliwataka wanafunzi wanaomaliza kuacha kujiingiza kwenye makundi ya uvutaji wa dawa za kulevya na badala yake watafute njia ya kuendelea na elimu ya juu.
Kawambwa alisema vijana ndiyo nguvukazi ya taifa, hivyo wazazi na walezi wanatakiwa kuhakikisha wanaangalia maendeleo ya watoto wao kila mara.
na Victor Masangu, Bagamoyo
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Elimu Mafunzo na Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, wakati wa sherehe za mahafali ya tisa ya kidato cha sita yaliyofanyika mwishoni mwa wiki katika Shule ya Sekondari Bagamoyo.
Dk. Kawambwa alisema serikali inatakiwa kuangalia kwa makini njia mbadala zinazotumika kufundishia wanafunzi wanaosoma katika shule za seminari.
Aliwataka wanafunzi wanaomaliza kuacha kujiingiza kwenye makundi ya uvutaji wa dawa za kulevya na badala yake watafute njia ya kuendelea na elimu ya juu.
Kawambwa alisema vijana ndiyo nguvukazi ya taifa, hivyo wazazi na walezi wanatakiwa kuhakikisha wanaangalia maendeleo ya watoto wao kila mara.