Serikali kujenga Daraja jipya Mto Wami

Serikali kujenga Daraja jipya Mto Wami

Kuna mradi ulipitishwa mwaka juzi kabla JK hajaondoka, huu mradi ulikuwa ni wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa 242km kutoka Tanga mjini kupitia Pangani, Sadani mpaka bagamoyo. Huu mradi upo chini ya Secretariat ya Africa mashariki na ujenzi wake utajumuisha pia ujenzi wa madaraja mawili, daraja la mto Pangani na daraja la mto wami ambalo litaunganisha mkoa wa Tanga na Pwani. Mradi huu ulitarajiwa kuanza mwaka wa fedha 2017/18, serikali ilisema inatafuta sponsor ambapo benki ya maendeleo ya ADB ilishaonesha nia ya kudhamini huo mradi. Sasa hiyo taarifa ya ujenzi wa daraja la mto Wami imekaaje ina maana wameamua kuweka pending mradi mzima wajenge kwanza daraja?
 
Serikali imesema kuwa itajenga daraja jipya mto Wami kwa kuwa Daraja linalotumika sasa ni dogo na limekuwa likisababisha usumbufu iwapo gari itaharibika katikati ya Daraja.
Ujenzi huo utagharimu kiasi cha shilingi za kitanzania Bilioni 3.

Source:The Guardian 02:02:2017
Aisee....miaka yote na risks zote gharama ya ujenzi ni bilioni 3 tu? au kuna sifuri (z)imesahaulika?!!!
 
Kuna mradi ulipitishwa mwaka juzi kabla JK hajaondoka, huu mradi ulikuwa ni wa ujenzi wa barabara yenye urefu wa 242km kutoka Tanga mjini kupitia Pangani, Sadani mpaka bagamoyo. Huu mradi upo chini ya Secretariat ya Africa mashariki na ujenzi wake utajumuisha pia ujenzi wa madaraja mawili, daraja la mto Pangani na daraja la mto wami ambalo litaunganisha mkoa wa Tanga na Pwani. Mradi huu ulitarajiwa kuanza mwaka wa fedha 2017/18, serikali ilisema inatafuta sponsor ambapo benki ya maendeleo ya ADB ilishaonesha nia ya kudhamini huo mradi. Sasa hiyo taarifa ya ujenzi wa daraja la mto Wami imekaaje ina maana wameamua kuweka pending mradi mzima wajenge kwanza daraja?
Kwani wamesema ujenzi wa hili daraja mdhamini ni huyo huyo wa barabara ya tanga-pangani? Au kukiwa na mradi wa barabara miradi mingine kama madaraja sehemu nyingine haiwezi kuendelea?
 
Kwani wamesema ujenzi wa hili daraja mdhamini ni huyo huyo wa barabara ya tanga-pangani? Au kukiwa na mradi wa barabara miradi mingine kama madaraja sehemu nyingine haiwezi kuendelea?
Umeeelewa nilichouliza? Yaani project ya daraja la wami ipo ndani ya project Tanga-Pangani-Bagamoyo, sasa naona wanataka kujenga daraja la wami tu ndo nikauliza project nzima imeishia wapi?
 
Umeeelewa nilichouliza? Yaani project ya daraja la wami ipo ndani ya project Tanga-Pangani-Bagamoyo, sasa naona wanataka kujenga daraja la wami tu ndo nikauliza project nzima imeishia wapi?
Jiografia yangu haiko vizuri, mimi najua daraja la mto Wami lipo kwenye barabara ya chalinze-segera.
 
Na kama inawezekana lihamishiwe pembeni kuondosha zile kona maana ndizo husababisha ajali mara kwa mara
pale ndugu kuna pembeni kweli....? sidhani maana lile eneo ni issue
 
Jiografia yangu haiko vizuri, mimi najua daraja la mto Wami lipo kwenye barabara ya chalinze-segera.
Sasa barabara inayotumika ni Tanga mjini-Segera- Chalinze ambayo inapita mtoto wami( kumbuka mto wami ndo unatenganisha Tanga na mkoa wa Pwani). Sasa serikali inataka kujenga barabara ambayo itakuwa route mpya kwa Tanga dar, hii itapitia Tanga-Pangani-Sadani-Bagamoyo, lakini hii route mpya pia itavuka mto wami na hivyo ujenzi wa daraja ni lazima( sijajua hii route mpya itatokea hapo hapo ilipo wami bridge ya sasa au kwingine, lakini for sure lazima wavuke mto wami)
 
Na kama inawezekana lihamishiwe pembeni kuondosha zile kona maana ndizo husababisha ajali mara kwa mara
Mkuu umeongea vyema.lile daraja sijui waliolibuni kwa nini waliliweka vile.daraja limejaa kona pande zote.wakiweza kutafta paha pamenyook ingekua safi sana.kona zile hatarishi sana.
 
Habari njema hii, Daraja la mto wami lilitakiwa kupanuliwa tangu zama za awamu zote zilizotangulia.Wembamba wa daraja lile linalounganisha mikoa na nchi jirani za kaskazini umebakia kuwa kiashiria cha hatari hadi leo.Natumaini litajengwa daraja kubwa la kisasa linalolingana na hadhi ya barabara hiyo.
 
jambo la maana sana ila awe makini na wale fisi wa pale Lumumba wasipige ulaji
 
Hili nijambo jema sana maana palikuwa na usumbufu mkubwa sana hapo wami,mzigo wakwenda Tanga lazima uzunguke Dodoma garama zinakuwa kubwa sana
 
Safi Sana.Na kama bajeti inatosha iwekwe fly over kutoka ng'ambo moja kwenda ng'ambo nyingine.Ile milima inaleta ajali sana na hasa kwa Malori.Hapa tuipigie makofi serikali kwaa kwaa kwaaa.
Tofauti ya Daraja na Fly over ni nini?
 
Barabara ya Morocco Mwenge ilikuwa Bil 4 ilo Daraja la Wami linajengwa kwa bil 3.. Aya sawa
 
Back
Top Bottom