Serikali kujenga Daraja jipya Mto Wami

Serikali kujenga Daraja jipya Mto Wami

Sasa barabara inayotumika ni Tanga mjini-Segera- Chalinze ambayo inapita mtoto wami( kumbuka mto wami ndo unatenganisha Tanga na mkoa wa Pwani). Sasa serikali inataka kujenga barabara ambayo itakuwa route mpya kwa Tanga dar, hii itapitia Tanga-Pangani-Sadani-Bagamoyo, lakini hii route mpya pia itavuka mto wami na hivyo ujenzi wa daraja ni lazima( sijajua hii route mpya itatokea hapo hapo ilipo wami bridge ya sasa au kwingine, lakini for sure lazima wavuke mto wami)
Ok ni afadhali wajenge sehemu ingine maanake imagine hili moja likipata hitilafu.
 
Ok ni afadhali wajenge sehemu ingine maanake imagine hili moja likipata hitilafu.
Ni kweli kabisa, yakiwepo mawili ya ukweli watu watapata njia mbadala pindi moja likiwa na hitilafu. Mungu asaidie hizi projects ziwe za uhakika
 
Tofauti ya Daraja na Fly over ni nini?
Mtochoro mimi siyo Civil Engineer lakini nadhani kwa suala la daraja la mto,daraja linaunganisha kingo za mto (river banks) fly over ni aina ya daraja lakini linakuwa juu Zaidi,kwa pale Ruvu fly Over haigusi river banks za mto Ruvu.Fly over niliyomaanisha pale Ruvu ni kwamba magari hayashuki kule bondeni kwenye mto, kinanyooshwa kitu hapo mkeka panakuwa hakuna mteremko wala mlima magari yanapita 180.Civil Engineers wanaweza kusaidia zaidi

A bridge is a structure built to span physical obstacles without closing the way underneath such as a body of water, valley, or road, for the purpose of providing passage over the obstacle

Flyover may refer to: Overpass, a high-level road bridge that crosses over a highway interchange or intersection.
 
Itakuwa poa sana, daraja jembambasanalile magari hayawezi kupishana kirahisi pale.
 
Serikali imesema kuwa itajenga daraja jipya mto Wami kwa kuwa Daraja linalotumika sasa ni dogo na limekuwa likisababisha usumbufu iwapo gari itaharibika katikati ya Daraja.
Ujenzi huo utagharimu kiasi cha shilingi za kitanzania Bilioni 3.

Source:The Guardian 02:02:2017
Safi sana... Naunga mkono hoja.
 
Safi Sana.Na kama bajeti inatosha iwekwe fly over kutoka ng'ambo moja kwenda ng'ambo nyingine.Ile milima inaleta ajali sana na hasa kwa Malori.Hapa tuipigie makofi serikali kwaa kwaa kwaaa.
Watuboreshee na ile njia ya Treni kutoka dar mpaka moshi wallau na sie tusafiri na mbuzi na kuku kwenda kula xmas ma kwetu hii biashara ya kila mwezi wa kumi na mbili kichwa kuuma kwa nauli kuwa juu ajili ya kwenda kujumuika na familia makwetu inatuharibu sana kisaikolojia
 
That's a good news, mwishoni mwa mwaka jana 2016, nilipita hapo wami darajani nikielekea Korogwe, kwa kweli niliogopa sana na niliahirisha safari ya kurudi Dar siku hiyo hiyo kwani muda ulienda sana, nikihofia kupita usiku hapo darajani. Ahsante Serikali kwa kutambua hilo, tunasubiri utekelezaji.
 
Watuboreshee na ile njia ya Treni kutoka dar mpaka moshi wallau na sie tusafiri na mbuzi na kuku kwenda kula xmas ma kwetu hii biashara ya kila mwezi wa kumi na mbili kichwa kuuma kwa nauli kuwa juu ajili ya kwenda kujumuika na familia makwetu inatuharibu sana kisaikolojia
Yaani sehemu ya kutumia masaa 7 uwe unatumia siku 2? umekuja kuwaje aise?
 
Yaani sehemu ya kutumia masaa 7 uwe unatumia siku 2? umekuja kuwaje aise?
Hujaelewa namaanisha waiboreshe iwe hata kama hiyo wanayotaka kujenga reli ya kati unaondoka dar asubuhi jioni upo moshi kwa usafiri wa bei nafuu na uhakika
 
Back
Top Bottom