Serikali iwakumbuke wastaafu

kakuruvi

JF-Expert Member
Sep 2, 2009
770
256
Habari Wana JF,

Juzi kwenye hotuba ya bajeti ya Serikali iliyosomwa na Waziri wa fedha, Waziri alitamka kufahamu kwamba kufuatia kutokuwepo kwa ajira za moja kwa moja kwa Wahitimu, Wazazi wamekua wakibeba mzigo mkubwa wa familia zao.

Kwa kulitambua hili naomba Serikali kuwezesha upatikanaji rahisi wa mafao ya Wastaafu ili waweze kuendelea kufurahia maisha yao baada ya kulitumikia Taifa, pamoja na kuendelea kuhudumia familia zao japo kwa mitaji midogo kwa Watoto wao Wahitimu ili wasiwategemee moja kwa moja.

Ili hili liwe rahisi kiinua mgongo cha Wabunge pia kicheleweshwe kama wanavyofanyiwa Wastaafu, Wabunge wakipata machungu wanayoyapata Wastaafu kwa sababu wao ndio wanaotunga hizi Sheria, watabadilisha ili mambo yaende sawa.

Nawasilisha!
 
Swala la kuminya kiinua mgongo cha mstaafu ni kudidimiza mipango yake ya kifamilia, maana kutokana na ukosefu wa ajira mstaafu alitegemea atumie mafao yake kuwekeza kwenye mradi ambao ungeweza kuajiri wanae ambao wamekumbwa na tatizo kubwa la ajira. Hivyo serikali isidhani inajua sana long-term plans za kila mtumishi hadi kumpangia mafao yake ya kustaafu yatumike vipi.
 
Hivi issue ya waliokua wafanyakazi wa EAC imeishia wapi?,au ni lengo la serikali ya CCM kutowalipa hawa wasteful haki yao?,naona wanafanikiwa maana wanatangulia kwa Allah, siwaoni tena pale Railway station, Mungu ni mwenye haki,ipo siku ataamua kwa haki
 
Habari Wana JF,

Juzi kwenye hotuba ya bajeti ya Serikali iliyosomwa na Waziri wa fedha, Waziri alitamka kufahamu kwamba kufuatia kutokuwepo kwa ajira za moja kwa moja kwa Wahitimu, Wazazi wamekua wakibeba mzigo mkubwa wa familia zao.

Kwa kulitambua hili naomba Serikali kuwezesha upatikanaji rahisi wa mafao ya Wastaafu ili waweze kuendelea kufurahia maisha yao baada ya kulitumikia Taifa, pamoja na kuendelea kuhudumia familia zao japo kwa mitaji midogo kwa Watoto wao Wahitimu ili wasiwategemee moja kwa moja.

Ili hili liwe rahisi kiinua mgongo cha Wabunge pia kicheleweshwe kama wanavyofanyiwa Wastaafu, Wabunge wakipata machungu wanayoyapata Wastaafu kwa sababu wao ndio wanaotunga hizi Sheria, watabadilisha ili mambo yaende sawa.

Nawasilisha!
Wabunge wenyewe hata hawana time na mada kama hizi
 
Back
Top Bottom