Serikali isikubali mtafaruku wa Bandari kuchukua mkondo wa kidini, ni ngumu kuidhibiti

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,341
51,907
SERIKALI ISIKUBALI MTAFARUKU WA BANDARI KUCHUKUA MKONDO WA KIDINI, NI NGUMU KUIDHIBITI.

Anaandika, Robert Heriel.
Mtibeli.

Haya mambo yanayoendelea ndani ya nchi Kwa kweli hayavutii na kuna Wakati yanatia wasiwasi. Serikali inahitaji kutiiwa lakini nayo inaowajibu wa kusikiliza kile wananchi(wengi) wanachokitaka. Serikali isiyosikiliza Watu wake kamwe haiwezi kutiiwa.

Sakata la Bandari limezua mengi. Pia limeibua Pande mbili, wanaokubali Mkataba na kundi la pili ni wale wanaokataa mkataba. Kundi la wanaoukataa mkataba wao wanasema wanataka mkataba huo uboreshwe na kufanyiwa mabadiliko kwenye baadhi ya vifungu. Na kama Hilo halifanyiki basi automatically hawataki huo mkataba(huo mkataba haufai).

Wote wanajinasibu kuwa wanaipenda Nchi. Wote wanashutumiana na kutupiana maneno Makali na mengine ni machafu.

Swali moja muhimu ambalo litaleta tija na kuwaunganisha Watu hawa ni hili?

" Kwa nini hivyo vifungu au hayo madai yanayotolewa kuhusu vifungu ambavyo ni Tata visitolewe au kurekebishwa kwenye huo Mkataba?"

Yaani ni kipi serikali inashindwa kuufanyia marekebisho huo mkataba?

Hapo ndipo hata Sisi tusio na upande tunaona kuna tatizo. Kama madai ya wanaoukataa mkataba Kwa kigezo cha baadhi ya vifungu kuwa na dosari ni Kwa nini hizo dosari au mapungufu yasifanyiwe kazi ili kuwaleta Watu wote pamoja?

Je ni kiburi?

Je ni kukosa Uzalendo?

Au je ni kweli Bandari imeuzwa(Jambo ambalo binafsi najua haijauzwa).

Serikali tuseme imakataa kusikiliza Maoni ya wanasiasa wa upinzani labda Kwa kuhofia kuwa watawapa bichwa.

Haya vipi kuhusu Chama cha Wanasheria TLS. Ikiwa hao waliowataalamu wa sheria wameona mkataba unakasoro na unahitaji marekebisho kadhaa iweje serikali ikatae.

Serikali haioni umuhimu wa kufikiria Jambo hili licha ya wataalamu WA Kada husika kushauri.

Ni kweli Katiba inampa mamlaka Rais kuamua Jambo lolote pasipo kuomba ushauri lakini Jambo Hilo lisivunje Katiba Kwa sababu ya kiapo cha kuilinda Katiba.

Lakini kuyapuuza mawazo ya wataalamu wa Kada husika kimakusudi ni kujaribu kuiweka rehani nchi kimakusudi.

Haiwezekani Umeenda hospitalini umeshauriwa na Madaktari kuwa utumiaji wa Dawa Fulani Mpya ambayo hujawahi Kutumia, Kwa jinsi mwili wako ulivyo kuanzia kinga na mifumo ya mwili, itakuletea shida alafu Kwa Makusudi utake Kutumia Dawa hizo Mbaya zaidi unataka familia nzima itumie. Kwa kweli hiyo haina maana nzuri.

Msimamo wangu ni kuwa, serikali Ione haja ya kusikiliza Maoni ya msingi hasa Kwa wataalamu wa sheria kuhusu huo Mkataba. Kama haitaki kusikiliza wanasiasa wenzao basi wasikilize Wanasheria wenye utaalamu wa sheria.

Kipi kinashindikana kuboresha kwenye Huo mkataba? Kwa nini kisiboreshwe ikiwa Watanzania wengi hasa wataalamu WA sheria wameona kuna dosari?

Serikali katika madai yake inasema, pale bandarini sijui wafanyakazi sio waaminifu, sijui wengine ni Wezi ndio wanaozotesha kazi za bandarini. Nilimsikia Spika akizungumzia Jambo hili.

Unajua kauli kama hizo zinajaribu kueleza kuwa serikali Ipo corrupted. Yaani serikali Kabisa inasema pale bandarini sijui kuna Wezi sijui kuna watendaji wabovu, kwani hakuna Mahakama?

Kwani hakuna vyombo vya kushughulikia wahalifu, au ukifanya kazi bandarini upo juu ya sheria kiasi cha kuepuka kuwajibishwa?

Kusema watanzania milioni 60 hakuna waadilifu wa kuweza kufanya kazi katika vitengo nyeti kama bandarini ni kujaribu kutukana taifa. Serikali inashindwa kupika na kutengeneza Vijana waadilifu ambao watafanya kazi zao Kwa ufanisi?

Haya, mitafafuku kama hii Watu wanakosa hoja na matokeo yake kuingiza dini kwenye Siasa.
Kikawaida dini ikishaingia kwenye Siasa inakuwa na nguvu kuliko serikali.

Ili serikali iwe na nguvu ni sharti iweke dini upande wa pili shilingi. Kwa sababu Dini ni upande wa pili wa serikali, au tuseme ni mkono wa kushoto wa serikali.

Serikali inaweza kupuuzia wataalamu, sayansi na uwekezaji na mapesa lakini kamwe haiwezi kupuuzia suala la Dini, ambayo msingi Mkuu ni Imani.

Imani inanguvu kuliko Kitu chochote Baada ya Upendo.

Njia kuu ya kudhibiti Imani na Dini za Watu ni Upendo. Huwezi Kutumia nguvu kudhibiti dini. Ila upendo unaweza Kutumika kudhibiti Dini.

Najua serikali inajua nini chakufanya muda huu. Lakini Njia Bora ni kuyafanyia kazi Yale yanayotolewa na upande wa pili Kwa sababu sio mambo mabaya.

Kupuuzia Watu sio Njia sahihi. Kuwatisha pia sio Njia sahihi. Na pia ikiwa lengo ni kuiletea Maendeleo nchi yetu, kuufuta kabisa huo mkataba sio Njia Sahihi.

Njia sahihi ni kuurekebisha ili ulinde maslahi ya nchi kama ilivyoshauriwa na Watalaamu.

Angalizo, ikiwa kuna kundi la Watu wameingiza maslahi Yao binafsi katika mkataba huu na kuacha Nyuma maslahi ya Watanzania hao ndio wanaotuletea shida na kutugawanya kama taifa.
Na Siku zote kikombe kikivunjika hata kiungwe hakiwi kilekile tena.

Watu wasitumie Dini kuitisha na kuishinikiza serikali au kumyumbisha Rais aliyepo madarakani. Ila kama Rais au kiongozi atakuwa mkaidi na kutoisikiliza Sauti ya wengi basi Watu nao hawatakuwa na wajibu wa kuitii serikali.

Lakini kama serikali inafanya Yale ambayo wananchi wanataka, wakitokea wakaidi washughulikiwe Kwa mujibu wa sheria.

Tunahitaji tuachane na haya mambo.

Imetosha, Muafaka chanya upatikane.

Tuzingatie kwenye hili hakuna mshindi, Ila mshindi awe ni taifa. Kuzozana kwetu kuwe kwaajili ya maslahi ya Nchi.

Muungwana akivuliwa nguo huchutama. Kurekebisha ulipokosea sio kujiabisha Bali ni uungwana. Na uungwana ni vitendo.

Nawatakia Sabato njema.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es Salaam
 
Kiongozi anapokosa weledi wa kuliongoza taifa, haya ndio matokeo yake. Siku zote tatizo linatakiwa kufanyiwa kazi pale ambapo dalili pekee zinaanza kujionesha juu ya jambo husika, na sio kuamini upepo tu utapita!.

Kiongozi mzuri lazima ajue kutazama reaction ya watu wake, agundue tatizo lilipo, na ajue namna ya kulikabili, kabla halijawa kubwa zaidi na kugeuka gumu kulitatua.

Sasa pale ambapo kiongozi katikati ya tatizo anajitokeza hadharani, anasema ametuzibia masikio, huyu anaonesha vile hajielewi binafsi, hawaelewi wale anaowaongoza, na wala hajui namna ya kutatua matatizo yao.

Matokeo yake sasa, wengi zaidi wanaibuka kuupinga mkataba tofauti na mwanzo, na kadri siku zinavyozidi kwenda mambo yanazidi kuwa magumu, asijue tena ahangaike na kundi lipi, matokeo yake anazidi kupotea.

Frankly speaking, Samia anatakiwa kujiuzulu nafasi yake, amepwaya sana, ameiacha nchi ijiendee tu, yupo yupo tu, sasa haaminiwi na wale anaowaongoza, naamini hata nae hana habari nasi, yeye kwa sasa yupo na baraza lake la mawaziri, na waarabu wa Dubai.
 
Kiongozi anapokosa weledi wa kuliongoza taifa, haya ndio matokeo yake. Siku zote tatizo linatakiwa kufanyiwa kazi pale ambapo dalili pekee zinaanza kujionesha juu ya jambo husika, na sio kuamini upepo tu utapita!.

Kiongozi mzuri lazima ajue kutazama reaction ya watu wake, agundue tatizo lilipo, na ajue namna ya kulikabili, kabla halijawa kubwa zaidi na kugeuka gumu kulitatua.

Sasa pale ambapo kiongozi katikati ya tatizo anajitokeza hadharani, anasema ametuzibia masikio, huyu anaonesha vile hajielewi binafsi, hawaelewi wale anaowaongoza, na wala hajui namna ya kutatua matatizo yao.

Matokeo yake sasa, wengi zaidi wanaibuka kuupinga mkataba tofauti na mwanzo, na kadri siku zinavyozidi kwenda mambo yanazidi kuwa magumu, asijue tena ahangaike na kundi lipi, matokeo yake anazidi kupotea.

Frankly speaking, Samia anatakiwa kujiuzulu nafasi yake, amepwaya sana, ameiacha nchi ijiendee tu, yupo yupo tu, sasa haaminiwi na wale anaowaongoza, naamini hata nae hana habari nasi, yeye kwa sasa yupo na baraza lake la mawaziri, na waarabu wa Dubai.

Nafasi aliyoitoa ya Watu kutoa Maoni nafikiri imetosha. Huu ni muda wa kushughulikia Maoni ya msingi ili tuendelee na mambo mengine
 
SERIKALI ISIKUBALI MTAFARUKU WA BANDARI KUCHUKUA MKONDO WA KIDINI, NI NGUMU KUIDHIBITI.

Anaandika, Robert Heriel.
Mtibeli.

Haya mambo yanayoendelea ndani ya nchi Kwa kweli hayavutii na kuna Wakati yanatia wasiwasi. Serikali inahitaji kutiiwa lakini nayo inaowajibu wa kusikiliza kile wananchi(wengi) wanachokitaka. Serikali isiyosikiliza Watu wake kamwe haiwezi kutiiwa.

Sakata la Bandari limezua mengi. Pia limeibua Pande mbili, wanaokubali Mkataba na kundi la pili ni wale wanaokataa mkataba. Kundi la wanaoukataa mkataba wao wanasema wanataka mkataba huo uboreshwe na kufanyiwa mabadiliko kwenye baadhi ya vifungu. Na kama Hilo halifanyiki basi automatically hawataki huo mkataba(huo mkataba haufai).

Wote wanajinasibu kuwa wanaipenda Nchi. Wote wanashutumiana na kutupiana maneno Makali na mengine ni machafu.

Swali moja muhimu ambalo litaleta tija na kuwaunganisha Watu hawa ni hili?

" Kwa nini hivyo vifungu au hayo madai yanayotolewa kuhusu vifungu ambavyo ni Tata visitolewe au kurekebishwa kwenye huo Mkataba?"

Yaani ni kipi serikali inashindwa kuufanyia marekebisho huo mkataba?

Hapo ndipo hata Sisi tusio na upande tunaona kuna tatizo. Kama madai ya wanaoukataa mkataba Kwa kigezo cha baadhi ya vifungu kuwa na dosari ni Kwa nini hizo dosari au mapungufu yasifanyiwe kazi ili kuwaleta Watu wote pamoja?

Je ni kiburi?

Je ni kukosa Uzalendo?

Au je ni kweli Bandari imeuzwa(Jambo ambalo binafsi najua haijauzwa).

Serikali tuseme imakataa kusikiliza Maoni ya wanasiasa wa upinzani labda Kwa kuhofia kuwa watawapa bichwa.

Haya vipi kuhusu Chama cha Wanasheria TLS. Ikiwa hao waliowataalamu wa sheria wameona mkataba unakasoro na unahitaji marekebisho kadhaa iweje serikali ikatae.

Serikali haioni umuhimu wa kufikiria Jambo hili licha ya wataalamu WA Kada husika kushauri.

Ni kweli Katiba inampa mamlaka Rais kuamua Jambo lolote pasipo kuomba ushauri lakini Jambo Hilo lisivunje Katiba Kwa sababu ya kiapo cha kuilinda Katiba.

Lakini kuyapuuza mawazo ya wataalamu wa Kada husika kimakusudi ni kujaribu kuiweka rehani nchi kimakusudi.

Haiwezekani Umeenda hospitalini umeshauriwa na Madaktari kuwa utumiaji wa Dawa Fulani Mpya ambayo hujawahi Kutumia, Kwa jinsi mwili wako ulivyo kuanzia kinga na mifumo ya mwili, itakuletea shida alafu Kwa Makusudi utake Kutumia Dawa hizo Mbaya zaidi unataka familia nzima itumie. Kwa kweli hiyo haina maana nzuri.

Msimamo wangu ni kuwa, serikali Ione haja ya kusikiliza Maoni ya msingi hasa Kwa wataalamu wa sheria kuhusu huo Mkataba. Kama haitaki kusikiliza wanasiasa wenzao basi wasikilize Wanasheria wenye utaalamu wa sheria.

Kipi kinashindikana kuboresha kwenye Huo mkataba? Kwa nini kisiboreshwe ikiwa Watanzania wengi hasa wataalamu WA sheria wameona kuna dosari?

Serikali katika madai yake inasema, pale bandarini sijui wafanyakazi sio waaminifu, sijui wengine ni Wezi ndio wanaozotesha kazi za bandarini. Nilimsikia Spika akizungumzia Jambo hili.

Unajua kauli kama hizo zinajaribu kueleza kuwa serikali Ipo corrupted. Yaani serikali Kabisa inasema pale bandarini sijui kuna Wezi sijui kuna watendaji wabovu, kwani hakuna Mahakama?

Kwani hakuna vyombo vya kushughulikia wahalifu, au ukifanya kazi bandarini upo juu ya sheria kiasi cha kuepuka kuwajibishwa?

Kusema watanzania milioni 60 hakuna waadilifu wa kuweza kufanya kazi katika vitengo nyeti kama bandarini ni kujaribu kutukana taifa. Serikali inashindwa kupika na kutengeneza Vijana waadilifu ambao watafanya kazi zao Kwa ufanisi?

Haya, mitafafuku kama hii Watu wanakosa hoja na matokeo yake kuingiza dini kwenye Siasa.
Kikawaida dini ikishaingia kwenye Siasa inakuwa na nguvu kuliko serikali.

Ili serikali iwe na nguvu ni sharti iweke dini upande wa pili shilingi. Kwa sababu Dini ni upande wa pili wa serikali, au tuseme ni mkono wa kushoto wa serikali.

Serikali inaweza kupuuzia wataalamu, sayansi na uwekezaji na mapesa lakini kamwe haiwezi kupuuzia suala la Dini, ambayo msingi Mkuu ni Imani.

Imani inanguvu kuliko Kitu chochote Baada ya Upendo.

Njia kuu ya kudhibiti Imani na Dini za Watu ni Upendo. Huwezi Kutumia nguvu kudhibiti dini. Ila upendo unaweza Kutumika kudhibiti Dini.

Najua serikali inajua nini chakufanya muda huu. Lakini Njia Bora ni kuyafanyia kazi Yale yanayotolewa na upande wa pili Kwa sababu sio mambo mabaya.

Kupuuzia Watu sio Njia sahihi. Kuwatisha pia sio Njia sahihi. Na pia ikiwa lengo ni kuiletea Maendeleo nchi yetu, kuufuta kabisa huo mkataba sio Njia Sahihi.

Njia sahihi ni kuurekebisha ili ulinde maslahi ya nchi kama ilivyoshauriwa na Watalaamu.

Angalizo, ikiwa kuna kundi la Watu wameingiza maslahi Yao binafsi katika mkataba huu na kuacha Nyuma maslahi ya Watanzania hao ndio wanaotuletea shida na kutugawanya kama taifa.
Na Siku zote kikombe kikivunjika hata kiungwe hakiwi kilekile tena.

Watu wasitumie Dini kuitisha na kuishinikiza serikali au kumyumbisha Rais aliyepo madarakani. Ila kama Rais au kiongozi atakuwa mkaidi na kutoisikiliza Sauti ya wengi basi Watu nao hawatakuwa na wajibu wa kuitii serikali.

Lakini kama serikali inafanya Yale ambayo wananchi wanataka, wakitokea wakaidi washughulikiwe Kwa mujibu wa sheria.

Tunahitaji tuachane na haya mambo.

Imetosha, Muafaka chanya upatikane.

Tuzingatie kwenye hili hakuna mshindi, Ila mshindi awe ni taifa. Kuzozana kwetu kuwe kwaajili ya maslahi ya Nchi.

Muungwana akivuliwa nguo huchutama. Kurekebisha ulipokosea sio kujiabisha Bali ni uungwana. Na uungwana ni vitendo.

Nawatakia Sabato njema.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es Salaam
 

Attachments

  • 63FA5F55-B29D-4372-ABA0-05207FBE24FE.png
    63FA5F55-B29D-4372-ABA0-05207FBE24FE.png
    84.3 KB · Views: 3
Ndugu mbona wanasheria kibao wametoa ufafanuzi kwa yale yanayopingwa? Wakili Msando akiwa namba moja kwenye kutoa utetezi. Halafu sio kila watu wanaopinga wanamaanisha kuwa wana nia njema. Hao wanaoitwa wanasheria nguli wakati mwingine hutumia sheria hizohizo kuiingiza nchi kwenye shida. Wakati Zitto akiwa mbunge na Idris Rashid akiwa boss Tanesco, alipeleka hoja bungeni kuwa serikali inunue mitambo ya Dowans na kujitengenezea umeme ambapo pia Dowans iliahidi mitambo ikinunuliwa watafuta kesi waliyokuwa wamefungua. Wasomi wakapinga na kudai anachoshauri Zitto ni kinyume na sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004. Kilichofuatia ni Dowans kushinda kesi huku mitambo wakiiuzia Symbions na hao Symbions kutuuzia sisi umeme. Kwahiyo wanasheria kama Shivji wanaweza kutumia sheria hizohizo kwa maslahi binafsi.
 
Back
Top Bottom