Serikali ipo katika mchakato kuhakikisha mahabusu wanafanya kazi magerezani kama wafungwa

mkiluvya

JF-Expert Member
May 23, 2019
802
725
1590846237631.png

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene amesema Serikali ipo katika mchakato wa kuhakikisha Mahabusu waliopo katika Magereza mbalimbali nchini wanaanza kufanya kazi kama ilivyokuwa kwa wafungwa.

Amesema mchakato huo ambao tayari umeanza, utakapo kamilika utaleta mapendekezo madhubuti ya jinsi gani ya kuwatumia mahabusu hao pamoja na wafungwa katika kufanya kazi za uzalishaji mali na kuhakikisha Jeshi hilo linajitegemea kikamilifu.

Akizungumza na Maafisa na Askari Magereza katika Magereza ya Segerea, Ukonga na Keko jijini Dar es Salaam, leo, kwa nyakati tofauti alipofanya ziara ya siku moja ya kusisitiza magereza yanajitegemea nchini, alisema ili binadamu ale lazima afanye kazi, na pia vitabu vitakatifu vinasisitiza hilo, hivyo mahabusu wanapaswa kufanya kazi kwa kuwa nao wanakula vyakula magerezani.

“Kuna mjadala mkubwa tunaendelea kuchakata kuhusu mahabusu waweze kufanya kazi, lakini lengo letu sio kuwafanyisha kazi za sulubu, au kazi zinazotweza utu wao, hapana, wao pamoja na wafungwa wana adhabu wanayoitumikia, tunataka kuwatumia katika kuzalisha, kwahiyo watafanya kazi kama watu wengine wanavyofanya kazi, hili naomba lieleweke,” alisema Simbachawene.
 
View attachment 1463576

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene amesema Serikali ipo katika mchakato wa kuhakikisha Mahabusu waliopo katika Magereza mbalimbali nchini wanaanza kufanya kazi kama ilivyokuwa kwa wafungwa. Amesema mchakato huo ambao tayari umeanza, utakapo kamilika utaleta mapendekezo madhubuti ya jinsi gani ya kuwatumia mahabusu hao pamoja na wafungwa katika kufanya kazi za uzalishaji mali na kuhakikisha Jeshi hilo linajitegemea kikamilifu.

Akizungumza na Maafisa na Askari Magereza katika Magereza ya Segerea, Ukonga na Keko jijini Dar es Salaam, leo, kwa nyakati tofauti alipofanya ziara ya siku moja ya kusisitiza magereza yanajitegemea nchini, alisema ili binadamu ale lazima afanye kazi, na pia vitabu vitakatifu vinasisitiza hilo, hivyo mahabusu wanapaswa kufanya kazi kwa kuwa nao wanakula vyakula magerezani.

“Kuna mjadala mkubwa tunaendelea kuchakata kuhusu mahabusu waweze kufanya kazi, lakini lengo letu sio kuwafanyisha kazi za sulubu, au kazi zinazotweza utu wao, hapana, wao pamoja na wafungwa wana adhabu wanayoitumikia, tunataka kuwatumia katika kuzalisha, kwahiyo watafanya kazi kama watu wengine wanavyofanya kazi, hili naomba lieleweke,” alisema Simbachawene.
Hii nchi sijui tulikosea wapi
 
Aisee kumbe Simbachawene ana mambo ya kipumbavu pia? Nilidhana sasa wizara imepata mtu timamu lakini inaonekana ujinga ni uleule.

Mahabusu hana hatia hadi pale mahakama itakapo mtia hatiani na kuhukumiwa kifungo, hajachagua kukaa gerezani, kama serikali inaona kuna gharama kubwa kumtunza basi imwachie huru aendelee kuhudhuria kesi yake akitokea nyumbani.

Kumlazimisha mtu asiye na hatia kufanya kazi ni kukiuka haki zake za msingi za kikatiba na ni sawa na tu na utumwa.

Screenshot_20200530-165841~2.png
 
Mkoloni mweusi ameanza ukoloni rasmi,na ukoloni wake si kama ule walioujua wazee wetu.

Ni ukoloni mkali na m baya zaidi,ukoloni huu mfano wake ni sawa na ule wakale,ule wa waarabu kuwafanya ama kuwauza wazee wetu watumwani.

Unamtumikishaje mtu ambaye huna uhakika na mashtaka yake?
Mahakama ikimhukumu kwamba huyu ni mkosaji, hapo ndipo unaweza kumfanyisha kazi kama adhabu ya makosa yake.

Mheshimiwa sana Trump aliwahi kusema nchi zetu hizi ni shit hole contry, hii inaonekana ni kweli.
 
Simbachawene alisifiwa sana mwanzoni. Lakini anazidi kuharibikiwa.Unamfanyishaje kazi MTU usiyemuhukumu bado?
 
Kama na mimi nimewekwa mahabusu nione na ambiwa kufanya kazi hiyo ndio itakuwa siku yangu ya mwisho kuishi katika hii sayari. Sitakubali sitakubali.
 
Hili kwa kweli binafsi siliungi mkono kabisa maana askari magereza wanaweza utumia mwanya huo kuwatumikisha kama wafungwa wakati wao hawajahukumiwa. Hili litazamwe kwa namna ya pekee ili lisigeuke mateso kwa wasio na hatia
 
Other countries detention centres are under prosecutors and not prison (correction) services
Kazi ya suspect ni kushtakiwa yaan kuhojiwa na si kutumikishwa kama sehemu ya adhabu au kukosa kazi ya kufanya wakiwa detained.

Watalazimisha
 
Back
Top Bottom