Malalamiko ya mfumuko wa bei yakizidi maana yake sekta Binafsi sio msaada kwa wananchi! Serikali iingie mzigoni kuleta ushindani!

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Oct 29, 2019
8,432
17,207
We JARIBU kufikiri Eti mafuta juu,vyakula juu kisa sekta Binafsi inatafuta faida kubwa kwa kuwanyonya wananchi!

Una jkt,magereza,watoto wa mitaani wanaokua Panyaroad halafu Eti unashindwa kuwatumia hao kuzalisha na kuwa price regulator wa bidhaa nchini!unaachia sekta Binafsi PEKEE uamue hatma ya nchi!hii haiwezekani!

Mafuta ya kula tu yatushinde,unga nao,mchele na ardhi yote hii plus nguvukazi kibao!!!?

Kama Taifa hatupo serious!serikali na sekta Binafsi zifanye KAZI kwa pamoja ili KILA mmoja amchunge mwenzake kwa faida ya wananchi!

Wafungwa Eti wanafungiwa ndanie masaa kibao, mahabusu? watoto wa mitaani ni janga ambalo hamna anaeliwazia yote nguvukazi hiyo! Kwanini isitumike ipasavyo kuzalisha kuipa upinzani sekta binafsi na wananchi wakafaidika?

Magereza wanaweza kuwa machinga wazuri KABISA wa bidhaa za serikali,maderwva wa mabasi ya mkoani ya serikali na jkt kama mbeba maono ya uzalishaji, watoto wa mitaani kamata wote peleka huko kuzalisha na mafunzo ya uzalendo jkt miezi mitatu kabla ya kuanza uzalishaji,hakuna mitoto itakayo zagaa kitaaa!!

Mungu ibariki Tanzania

NIPO HAPA nasubiri niambiwe na DOLA nichukue fomu ya urais niiweke nchi sawa coz imepinda!!

Asante kwa kusoma.

"Mzee Warioba ajumuishwe Kwenye kikosi kazi mchakato wa Katiba mpya ukamilike mapema!
 
Back
Top Bottom