Serikali ingewaacha CHADEMA waandamane ingekuwaje?

Serikali ingewaacha CHADEMA waandamane ingekuwaje?

afwe

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2010
Posts
4,080
Reaction score
765
Nimejaribu kufuatilia kwa karibu mambo yanayotokea kufuatia CDM kuamua kuandamana kupinga mwenendo wa BMK nimejikuta ninapata shida kuamini kuwa nchi yetu ina intelijensia iliyo makini. Sidhani kama kuazimia kuandamana ni kosa. Bila shaka ni vibaya kuandamana bila kufuata utaratibu. Nimeshangaa polisi kupiga marufuku maandamano hata kabla ya taarifa za dhamira ya kuandamana kupelekwa katika ofisi zao.

Nimeshawishika kuamini kwamba huenda serikali kupitia jeshi lake la polisi kama wangeamua kushirikianana na CDM kuandaa na hatimaye kuyasimamia maandaano yao huenda impact ya maandamano hayo isingekuwa kubwa kama dhamira ya CDM ilivyokuwa. Kitendo cha kuyazuia kimeifanya CDM kuwa yenye mafanikio makubwa kwani imewafanya watanzania wajue kuwa kuna ufisadi katika serikali na chama tawala. Ni kweli watu wengi wakiwemo watoto wamejua kuwa serikali yao ni dhalimu kwa kuona mabavu yanayotumika.
 
wangemtumia jambazi Lema kulipua mabomu na watu kuuwawa au kujeruhiwa kisha wangelisingizia jeshi la polisi.
 
Wangeiba mali za watu na kusabaisha vitendo vya ubakaji pia kutokea kwavile tabia zao ni chafu.
 
wangemtumia jambazi Lema kulipua mabomu na watu kuuwawa au kujeruhiwa kisha wangelisingizia jeshi la polisi.

Bomu lililolipuliwa kwenye mkutano wa CDM lilitoka kwenye ghala la JWTZ na hii baada ya WM Pinda kuropoka bils kujua madhara yake, swali kwako hivi Lema anafanya kazi kwenye ghala lipi? Tujuze!
 
Bomu lililolipuliwa kwenye mkutano wa CDM lilitoka kwenye ghala la JWTZ na hii baada ya WM Pinda kuropoka bils kujua madhara yake, swali kwako hivi Lema anafanya kazi kwenye ghala lipi? Tujuze!

ina maana hujui kama Lema alikuwa jambazi au unafanya kusudi?
 
Wangeachwa wafanye halafu tuone wangeharibu nini?mpaka imefikia hatua na kuona hiyo nguvu ya polisi ni kutokana na nchi kuwa na amani,kama wangekuwa Nigeria,wangewezaje kuzuia BHOKO HARAMU na MAANDAMANo?polisi acheni unyanyasaji
 
Serikali ilikuwa inaogopa kuaibika kwa kuwa hayo maandamano yangeungwa mkono na watu wengi sana!
 
Na wewe kilaza mbila ni njaa tu inakutesa Sio kingine ila ole wako uthukumiwa kwa kiwango cha uelewa wako
 
Maandamano ni sumu kwa utawala,ipo hivyo toka enzi na enzi,, harakati nyingi duniani zimefanikiwa kwa maandamano.
 
Mwakani wampandishe mtu mmoja sio kila mtu na Chama chake mkifanya hivyo namie nitapiga kura nitahandamana nanyi. Lakini kwa sasa bado naona mnatudanganya tu.
 
Back
Top Bottom