stakehigh
JF-Expert Member
- Aug 9, 2019
- 6,385
- 3,494
Wakati ujenzi wa kipande cha Dar – Morogoro ulitakiwa kukamilika katika kipindi cha miezi 30 baada ya kuzinduliwa, na muda huo umepita, haifahamiki sababu za kuchelewa kwake wala siku ya kuanza kutumika.
CAG Charles Kichere alibainisha katika ripoti yake ya miradi ya maendeleo ya mwaka 2019/20 kwamba Serikali imelipa zaidi ya Sh2.9 bilioni kama riba ya ucheleweshaji wa malipo kwa makandarasi na Sh26 bilioni kama ucheleweshaji wa mradi hadi kufikia Aprili 2020.
Alipotafutwa kuzungumzia maendeleo ya mradi huo na lini majaribio yatafanyika, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC), Masanja Kadogosa hakutaka kulifafanua suala hilo.
“Mbona tulishatoa taarifa kuhusu hilo, niko barabarani, nipigie kesho (leo) tuzungumze,” alijibu Kadogosa na hata alipotafutwa siku iliyofuata hakupokea simu yake wala kujibu ujumbe mfupi wa simu aliotumiwa.
Hata hivyo, Mwananchi lilimtafuta Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa ambaye alisema alipoingia wizarani, aliambiwa majaribio ya reli ya kisasa yatafanyika Desemba inayoanza leo.
soma zaidi: Danadana majaribio treni ya SGR Dar - Moro
CAG Charles Kichere alibainisha katika ripoti yake ya miradi ya maendeleo ya mwaka 2019/20 kwamba Serikali imelipa zaidi ya Sh2.9 bilioni kama riba ya ucheleweshaji wa malipo kwa makandarasi na Sh26 bilioni kama ucheleweshaji wa mradi hadi kufikia Aprili 2020.
Alipotafutwa kuzungumzia maendeleo ya mradi huo na lini majaribio yatafanyika, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli (TRC), Masanja Kadogosa hakutaka kulifafanua suala hilo.
“Mbona tulishatoa taarifa kuhusu hilo, niko barabarani, nipigie kesho (leo) tuzungumze,” alijibu Kadogosa na hata alipotafutwa siku iliyofuata hakupokea simu yake wala kujibu ujumbe mfupi wa simu aliotumiwa.
Hata hivyo, Mwananchi lilimtafuta Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa ambaye alisema alipoingia wizarani, aliambiwa majaribio ya reli ya kisasa yatafanyika Desemba inayoanza leo.
soma zaidi: Danadana majaribio treni ya SGR Dar - Moro