Serikali ikumbuke kuweka bendera kwenye ofisi zake

Nzelu za bwino

JF-Expert Member
Jan 12, 2020
376
450
Salaam wana jamii forum,

Leo nimeona niikumbushe serikali tukufu ya jamhuri ya muungano wa tanzania kuhusu kuweka bendera kwenye ofisi za serikali ngazi ya mtaa,kitongoji,Kijiji Hadi kata.maana imekua kawaida kwa sasa kuzikuta ofisi hizi bila kuwepo bendera ya taifa.

Kuna umuhimu mkubwa sana kwa hizi ofisi kuwa na bendera ya taifa kwani inasaidia kwa mtu mgeni kuitambua ofisi, kuipa hadhi ofisi husika ,kuongeza uzalendo kwa raia kwani kila inapo pandishwa na kushushwa bendera kila raia ukumbuka taifa lake nakuipa heshima bendera ya taifa kwa kusimamia.naomba kuwasilisha.
 
Ni kweli ofisi nyingi hazina bender lakini ukiruhusu mradi huo kuna watu wanaenda kutajirika
 
Back
Top Bottom