Serikali ifunge ukurasa wa Ben Saanane ukweli ujulikane

Labda kama hata shetani mwenyewe anaweza kutubu akasamehewa...
Kutubu kazi ndugu,badala ya kutubu unaongeza dhambi.
Unapotubu kama uliua,unatakiwa umtaje yule uliemuua ,Kama Ni mmoja wawili au zaidi.ukificha hapo umesema uongo,na hivyo unakua umetenda dhambi zaidi.
Je huyo mtubuji anaweza kumwambia mtubishaji kuwa aliua wangapi?
Halafu fikiria unatubu mbele ya Askofu.
 
Mimi niliumia sana kwa kweli maana alijulikana kabisa kwamba ameuawa na wakatili sema ndio hivyo tena hatuna jinsi yeyote zaidi ya kumuombea Mwenyezi Mungu amrehemu...
 
mwana kulifind mwana kuliget.

harakati zikirenga umaarufu mwisho wake huwa sio mzuri.
sina uhakika kama jamaa aliuawa,lakini kwa kazi aliyokuwa amejipa,hakutumwa na mtu yeyote.hata wazazi wake sidhani kama wangemuunga mkono.
 
Huyu jamaa katika uzi huu post # 44 aliwahi kuandika hivi. Bila ya shaka ni mmoja wa wahusika wa kupotea kwa Ben Saanane

Ben Saanane: Ninatishwa kuuawa kwa kuikosoa Serikali TumainiEl
Ben acha huu upotoshaji kama unajiita wewe kidume basi endelea ila mimi ni shahidi ndani ya mtandao huu umeshaonywa sana.
Ila mimi nataka kukutabiria jambo. Kama kweli hutobadilika nakuendelea na hii mambo basi kifo chako hutopata nafasi kuja kuandika humu na kwa bahati mbaya watu watakuwa wameshasahau sana sana watajuwa umekufa kama binadam wengine ila kumbuka huna uharakati wowote my dia hata punje ya Dr Ulimboka huna sasa jiangalie usitafute umaarufu wakati kifaru kiponjiani unakizuia kisipite kwa mwili wa nyama utakufa na hao unao walaani wala haiwapati... Take care this is a nation kaa mbali
Niseme wazi kuwa sikuwahi kuwa fan wa Ben Saanane Kwa lolote lile lakini Kwa sababu alikuwa member mwenzetu hapa nilimuona kama mtu wa karibu au nnaefahamiana nae hivi sababu ya kushiriki pamoja mijadala mbalimbali hapa Jf..


Alipoanza kuandikia gazeti la Raia mwema na kuanza kuhoji PHD ya Magufuli binafsi sikuwahi kuwa na interest na huo mjadala..
Kwanza niliuona hauna maana sana..
Pili niliona hautaweza badilisha lolote Kwa hiyo ni kama anajisumbua..

Ilipoanza kutangazwa kapotea nilistuka sana..binafsi nilifikiri labda kajificha ili apate attention kubwa akiibuka tena..
Lakin hadi leo hatuna majibu sahihi hasa nini kilimkuta Ben Saanane..

Alipofariki Magufuli nikahisi labda alikuwa amefungwa rumande kimyakimya
Na sasa ataachiliwa lakini hadi sasa naona kimyaa kabisa...

Natamani sasa ukweli ujulikane tuweze funga ukurasa...kama yupo hai aachiwe
Kama alikufa ijulikane alikufaje?
Wahusika kina nani?Mwili upo wapi??
Ilikuwa kusudi au ajali kwenye interogation? ..

Naaamin familia yake inahitaji kujua ukweli..na Sisi wengine tuzungumze kitu kilichothibitishwa....

Nafikiri wakati wa ukweli kujulikana umefika..

Familia na marafiki waombe kumuona Rais asaidie uchunguzi tupate majibu
 
Hilo andiko la PLAGIARISM la Mwendazake alilokopi kwa Dr Y Philip na kusimamiwa na Prof Buchweshaija iliondolewa makataba ever since, huwezi kupewa kwa ajili ya rejea

Katika AIBU za UDSM wanaojipambanua kuwa ndiyo Chuo Kikuu bora Tanzania, na kuviponda vyuo vingine kuwa havina Ma Profesa wenye majina, au sijui vyuo vingine vinatoa degree za kuandikiwa THESIS, basi nao hii ni AIBU yao.

Itafika siku CCM ikiwa nje ya madaraka, tutaweka petition ya UDSM kuifuta PhD ya Mwendazake kama ambavyo LSE walivyofuta PhD ya mtoto wa Gaddafi mwaka 2011. Na hapo tutakuwa timekamiklsha kazi ya Ben Saanane na tutakuwa TUMEMUENZI inavyostahili
Nimesoma huu mchango, nikataka kuandika lakini nikaona nisitie neno.....
 
Niseme wazi kuwa sikuwahi kuwa fan wa Ben Saanane Kwa lolote lile lakini Kwa sababu alikuwa member mwenzetu hapa nilimuona kama mtu wa karibu au nnaefahamiana nae hivi sababu ya kushiriki pamoja mijadala mbalimbali hapa Jf..

Alipoanza kuandikia gazeti la Raia mwema na kuanza kuhoji PHD ya Magufuli binafsi sikuwahi kuwa na interest na huo mjadala..
Kwanza niliuona hauna maana sana..
Pili niliona hautaweza badilisha lolote Kwa hiyo ni kama anajisumbua..

Ilipoanza kutangazwa kapotea nilistuka sana..binafsi nilifikiri labda kajificha ili apate attention kubwa akiibuka tena..
Lakin hadi leo hatuna majibu sahihi hasa nini kilimkuta Ben Saanane..

Alipofariki Magufuli nikahisi labda alikuwa amefungwa rumande kimyakimya
Na sasa ataachiliwa lakini hadi sasa naona kimyaa kabisa...

Natamani sasa ukweli ujulikane tuweze funga ukurasa...kama yupo hai aachiwe
Kama alikufa ijulikane alikufaje?
Wahusika kina nani?Mwili upo wapi??
Ilikuwa kusudi au ajali kwenye interogation? ..

Naaamin familia yake inahitaji kujua ukweli..na Sisi wengine tuzungumze kitu kilichothibitishwa....

Nafikiri wakati wa ukweli kujulikana umefika..

Familia na marafiki waombe kumuona Rais asaidie uchunguzi tupate majibu
FB_IMG_1618748256371.jpg
 
Marehemu Baba Jesca hakuwa tu mtu muovu, hakuwa hata na chembe cha utu. Aliwahi kuwaita watoto wa watu vilaza na kuwatimua vyuoni huku yeye akiwapa vilaza vyeo na kuwafuga wengine nyumbani kwake. Ukweli mchungu ni kwamba huwezi ukapanda mchicha ukavuna nyanya na hakuna namna Baba Jesca angeweza kuzaa kipanga huku yeye ni mtupu kabisa kichwani na cheti feki cha PhD, DNA haikubali!

Kwa sasa wengine tunampa Rais Samia Suluhu Hassan muda wa miezi mitatu kama tulivyompa mwendazake kwa shingo upande. Katika hizo siku 100 tunategemea ataonesha utofauti wake na aliyemtangulia kwa kukitegua kitendawili cha hatma ya Ben Saanane na wengineo. Kwa sasa tupo tunaoendelea kumpa Rais wetu mpya benefit of doubt lakini akae akijua siku hazigandi na kufumba na kufumbua likizo imeisha.
Kule kukariri tarakimu, kuhadaa watu - kiasi cha samaki waliomo ziwani/baharini?
Kilomita za barabara zilizojengwa
Ma-DED wanaoshindwa kutema tarakimu kwenye mkutano wanatumbuliwa hapo kwa hapo - yote hayo kujionyesha usomi!

Mwisho, wakati anaondoka hata hakujua hasara iliyosababishwa na ununuzi wa ndege kiholela!

Huyo bwana alikuwa ni mpenda sifa ambazo hakuzistahili hata kidogo. Matatizo yake yalikuwa yanaanzia hapo, kutafuta sifa.

Sina matumaini makubwa na huyu mama, kwamba anaweza akaleta mabadiliko chanya zaidi ya hali iliyopo sasa. Kwanza tu, hicho chama chake hakieleweki kipo wapi wakati huu. Atahangaika sana na chama chake hata kama atakuwa anataka kufanya mabadiliko nje ya chama hicho, achia mbali ndani ya chama chenyewe.
 
Kule kukariri tarakimu, kuhadaa watu - kiasi cha samaki waliomo ziwani/baharini?
Kilomita za barabara zilizojengwa
Ma-DED wanaoshindwa kutema tarakimu kwenye mkutano wanatumbuliwa hapo kwa hapo - yote hayo kujionyesha usomi!

Mwisho, wakati anaondoka hata hakujua hasara iliyosababishwa na ununuzi wa ndege kiholela!

Huyo bwana alikuwa ni mpenda sifa ambazo hakuzistahili hata kidogo. Matatizo yake yalikuwa yanaanzia hapo, kutafuta sifa.

Sina matumaini makubwa na huyu mama, kwamba anaweza akaleta mabadiliko chanya zaidi ya hali iliyopo sasa. Kwanza tu, hicho chama chake hakieleweki kipo wapi wakati huu. Atahangaika sana na chama chake hata kama atakuwa anataka kufanya mabadiliko nje ya chama hicho, achia mbali ndani ya chama chenyewe.
😆😆😆
 
Back
Top Bottom