Jambo moja ambalo hujamwelewa mleta mada ni maana nchi kuwa na mfumo wa cable TV, sehemu chache sana zipo kama majaribio lakini si mfumo wa Cable at all. Kwa ambao hawajatembea na kufanya ulinganifu wa maana ya cable TV wataelewa tu kwamba unachosema ndio mfumo.
Kwa Taarifa Cable TV unayosema ni mfumo wa kivigongoji kama kwenye mada hii hapo juu. Unaweza nionyesha nyaya za Cable TM ambazo zimetandazwa miji yote hata miji uliyoitaja kwamba kila anayetaka ni kuinua simu kuita wamwunganishie? Kama ni huduma ya kitongoji fulani kama ilivyo Kariakoo, magomeni na Ilala jijini Dar huwezi kusema tuna mfumo wa Cable TV. Tunaweza kusema tuna mfumo wa simu na umeme kwa vile kila sehemu mijini na baadhi ya vijiji huduma huyo imetandazwa eneo karibu lote. Hapa ndipo tunaposhindwa kuelewana.
Dish nalo ni la vibosile wachache wenye uwezo hivyo huwezi kusema wote wanatumia wakati ni wachache.