Serikali iache kiburi kulazimisha mfumo wa Digital

Serikali iache kiburi kulazimisha mfumo wa Digital

Mkuu,
Ni mikoa ipi ambayo umetembea na ukaona asilimia kubwa wanatumia analogy? Nimekupa mfano wa mikoa ambayo mimi nina uhakika nayo kuwa analogy huko haijawa succsesful. Mfano Iringa, Mbeya, Mwanza, Kagera na Mara. Huko watu wanatumia zaidi satellite dish na cable tv, wewe unachobisha ni nini. Iringa asilimia kubwa ni dish uwe mjini au kijijini. Mbeya nako vivyo hivyo. Mwanza wanatumia dish na cable tv. Kuna watu kama Mwanza Satellite, Barmedas Tv, Ghana Tv wanasupply sehemu kubwa ya jiji la Mwanza, halafu wewe unasema eti makubaliano ya watu watatu, si kweli mkuu hujafanya research na ndio maana nasema yawezekana wewe anaiangalia DSM ukahisi na mikoani ni hivyo hivyo.

Kigoma pekee sijatia mguu wala kunusa hewa yake, hali kadhalika Tanzania visiwani, lakini mikoa mingine yote iliyobaki hakuna pakunidanganya nimekoroga kote.

Kwa mtazamo wa huduma za jamii hatuhesabu mtaa au kitongoji fulani nani ana dish network au kutumia converter box, tunachoangalia huduma hiyo imesambaa kwa wananchi wote. Kinachoendelea hapa ni kuangalia huduma iliyofikiwa kwa wachache wakati walio wengi pengine uwezo huo hawana, na zaidi waliojitahidi kuanza kuitumia sasa mfumo huo mpya unafanya warudie maisha ya zamani kupata habari kwa kutumia redio tu.
 
800px-HFC_Network_Diagram.svg.png

Umesema kuna watumiaji wa Cable Television, kwa uelewa wangu Tanzania hatuna kitu kama hicho, hivyo kama kipo kwa mtazamo wangu ni pale tu mwenye Dish television kushare kwa jirani si kigezo cha kwamba tuna Cable Television Tanzania. Kielelezo nilichoambatanisha ndio mfumo wa Cable television ambapo waya wa cable husambazwa sambamba na nguzo za umeme na simu na kuingiza majumbani.

Ndugu cable zipo,sijui wewe upo mkoa gani kwasababu nadhani mikoa karibu yote hapa nchini cable zipo na zinafanya kazi kwa mfumo huohuo uliouweka hapo njuu.
 
Hujanielewa, sipingi uwepo wa digital, ninachoongelea ni kusitishwa mitambo ya analogia. Jambo la msingi serikali ingeruhusu mitambo ya analogia kupata muda zaidi wa kutoa huduma kwa wasio na nafasi ya haraka kuingia kwenye mfumo mpya.

Kumbuka kwa utaratibu wa sasa, wananchi wanalazimika kuweka darini TV za analogia ambazo hazijatengenezwa kwa mfumo wa Digital. Hilo lawezekana na lipo kwa vile walio wengi pengine nafasi kwa sasa haiwaruhusu. Serikali haina huruma kwa watu kama hao ambao ni walipa kodi na wapiga kura?
nakuelewa vizuri sana,tatizo lililopo kwa watanzania ni maneno mengi bila vitendo,nakuhakikishia kuwa hizo tv ulizoziona dalini zitaendelea kuwa dalini hata utakapofika mwaka 2015 ama 2018,ikimaanisha kuwa watanzania hao hata kama wangepewa muda hadi hiyo miaka niliyoitaja hapo bado ungesikia kauli ya "bado hatujajiandaa "
 
Ndugu cable zipo,sijui wewe upo mkoa gani kwasababu nadhani mikoa karibu yote hapa nchini cable zipo na zinafanya kazi kwa mfumo huohuo uliouweka hapo njuu.

Ninachofahamu ni cable sharing si cable system ambayo imesambaza majumbani. Mfumo huo ungekuwepo maana yake mtu angekuwa na nafasi ya kuomba kuunganishiwa kama inavyotokea kwa umeme na simu. Ninachojua ni cable television sharing ambayo haiko rasmi kama Standard Cable Televison system. Nchi zilizoendelea nyumba mpaka ikamilike iwe na hati ya makazi lazima iwe na umeme, simu na Cable television.

Unaweza kunionyesha cable system iliyosambazwa kwenye pole nchini, tuanze na mijini kwamba waya za cable television simesambazwa sambamba na waya wa simu na umeme?

Naendelea kusisitiza huduma inapotokea kwa watu wachache mtaa fulani kwa wenye standard huwezi kuichukulia kwamba huduma hiyo imesambaa kwa wananchi. Tunatakiwa kuwa wapana katika kupambanua mambo hayo kwa mtazamo wa kitaifa na kuwafikia wananchi walio wengi si tabaka fulani tu kuhalalisha kwamba wananchi wote wanapata huduma hiyo.
 
nakuelewa vizuri sana,tatizo lililopo kwa watanzania ni maneno mengi bila vitendo,nakuhakikishia kuwa hizo tv ulizoziona dalini zitaendelea kuwa dalini hata utakapofika mwaka 2015 ama 2018,ikimaanisha kuwa watanzania hao hata kama wangepewa muda hadi hiyo miaka niliyoitaja hapo bado ungesikia kauli ya "bado hatujajiandaa "

Katika hilo niko kinyume kabisa na mtazamo wako. Watanzania wana tabia ya kasumba ya kupenda kujionyesha wana nini majumbani mwao. Tukiwapa muda watamudu zoezi hili na utashangaa. Kilichofanyika ni zoezi la haraka mno kama ilivyotokea miaka ile kuhamishia watu vijijini bila matayarisho na kuishia kuwachapa viboko wale waliokuwa wazito kuhamia ni kwa sababu tu ya kutowajengea uelewa na kuwaandalia mazingira, nafasi ya kupata dhana hizo. Television converter box si kitu cha kununua leo kama unaenda kununua kalamu ya kuandikia, inahitaji kupangia bajeti na hivyo tunajua pato la walio wengi mahesabu ya daladala tu yanatupa taabu na kushia kuchakaza kandambili.
 
Katika hilo niko kinyume kabisa na mtazamo wako. Watanzania wana tabia ya kasumba ya kupenda kujionyesha wana nini majumbani mwao. Tukiwapa muda watamudu zoezi hili na utashangaa. Kilichofanyika ni zoezi la haraka mno kama ilivyotokea miaka ile kuhamishia watu vijijini bila matayarisho na kuishia kuwachapa viboko wale waliokuwa wazito kuhamia ni kwa sababu tu ya kutowajengea uelewa na kuwaandalia mazingira, nafasi ya kupata dhana hizo. Television converter box si kitu cha kununua leo kama unaenda kununua kalamu ya kuandikia, inahitaji kupangia bajeti na hivyo tunajua pato la walio wengi mahesabu ya daladala tu yanatupa taabu na kushia kuchakaza kandambili.

sawa bwana,ngoja tusubiri la leseni za madreva,sijui watakuwa na nini la kusema,nitarudi tena hapa kuendelea kupiga soga.
ila ingekuwa vyema kama zile chanel za bure zinge endelea kuwa ni bure,hata kama mtu hata lipia kwa mwezi lakini bado awe naweza kupata zile free channels kama kawaida.
 
800px-HFC_Network_Diagram.svg.png

Umesema kuna watumiaji wa Cable Television, kwa uelewa wangu Tanzania hatuna kitu kama hicho, hivyo kama kipo kwa mtazamo wangu ni pale tu mwenye Dish television kushare kwa jirani si kigezo cha kwamba tuna Cable Television Tanzania. Kielelezo nilichoambatanisha ndio mfumo wa Cable television ambapo waya wa cable husambazwa sambamba na nguzo za umeme na simu na kuingiza majumbani.

Hujatembea kiongozi usiwe mbishi. Jf ni sehemu mojawapo ya kujuzana. Kama kuna mtu wa Mwanza humu atukuhakikishia ninachokuambia. Mwanza kuna
Na wengine ambao mimi siwafahamu. Usiconclude kitu bila kuwa na data. Ndio maana mwenzako nimetolea mfano mikoa ambayo nina uhakika nayo tu.
 
Ninachofahamu ni cable sharing si cable system ambayo imesambaza majumbani. Mfumo huo ungekuwepo maana yake mtu angekuwa na nafasi ya kuomba kuunganishiwa kama inavyotokea kwa umeme na simu. Ninachojua ni cable television sharing ambayo haiko rasmi kama Standard Cable Televison system. Nchi zilizoendelea nyumba mpaka ikamilike iwe na hati ya makazi lazima iwe na umeme, simu na Cable television.

Unaweza kunionyesha cable system iliyosambazwa kwenye pole nchini, tuanze na mijini kwamba waya za cable television simesambazwa sambamba na waya wa simu na umeme?

Naendelea kusisitiza huduma inapotokea kwa watu wachache mtaa fulani kwa wenye standard huwezi kuichukulia kwamba huduma hiyo imesambaa kwa wananchi. Tunatakiwa kuwa wapana katika kupambanua mambo hayo kwa mtazamo wa kitaifa na kuwafikia wananchi walio wengi si tabaka fulani tu kuhalalisha kwamba wananchi wote wanapata huduma hiyo.

Tembea uone mkuu, usipende kuwa mbishi bila data.
 
Bila kujali ni dili la watu au la, lakini tuwe wakweli ni lini watanzania wanakuwa tayari ? hata tusubiri kuzima hiyo analojia 2015 bado wapo watakaolalamika kuwa hawapati tena matangazo......Angalia kwenye suala la leseni leo ndio utaona misururu ya kilometa moja...suala la benki"updating" nalo ni ishu...Naona serikali ibaki na msimamo wake tu....
 
Sifa moja mbaya kabisa ninayoichukia kwa watanzania wanaishi Dar ni tabia ya kujenga hoja bila kufanya utafiti halafu unajaribu ku influence mamlaka zifuate unachoamini!Kwanza kusema watanzania wengi wanatumia analogia sie kweli hata kidogo unless unamaanisha watanzania ni wale pekee waishio Mjini hususan Dar!Nasema hivi kwa sababu tangu mfumo wa analogia uanze duniani,wakazi wa miji midogo ya wilaya karibu zote hawajawahi kutumia mfumo wa analogia bali wanatumia dishes na cable ambayo hulipiwa kila mwezi!na tumezoea!Serikali iko sahihi kabisa iwapo hiyo ni njia ya kuongeza wigo wa mapato.Watu wa Dar acheni ubinafsi na kujifikiria ninyi ndio watanzania kuliko watanzania wengine!Ninaishi Kahama sehemu ilipo migodi mikubwa miwili ya Barick,lakini pamoja na mchango mkubwa wa fedha za kigeni na mapato kutokana na dhahabu,bado huduma za barabara ni mbovu na kijilami cha kisanii ndicho kimewekwa mjini!Umeme kila uchao umekuwa ukikatika katika kwa visingizio visivyo na msingi wowote!Bado wengi wenu mnaoishi Dar na takwimu za kutupumbaza mnajipigia debe kwa visingizio eti Watanzania wengi hawana uwezo wa kununua ving'amuzi!Naipongeza serikali tena ninyi mnaojidai watanzania waliowengi mfunguke akili kwani asilimia kubwa ndio mnaofaidi fedha za ufisadi wa watumishi wa serikali!Wanaiba wilayani wanakuja Dar kuwekeza mijumba na biashara za anasa lakini mwisho wa siku pamoja na kufaidi huko mnalalamika sana!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Hujatembea kiongozi usiwe mbishi. Jf ni sehemu mojawapo ya kujuzana. Kama kuna mtu wa Mwanza humu atukuhakikishia ninachokuambia. Mwanza kuna
Na wengine ambao mimi siwafahamu. Usiconclude kitu bila kuwa na data. Ndio maana mwenzako nimetolea mfano mikoa ambayo nina uhakika nayo tu.
Uko sawa mkuu.Mwanza na wilaya zake zoote na Shinyanga Simiyu na wilaya zake zote wanatumia cable na ma dish!analogia ni wachache sana waliokuwa wanatumia Mwanza jiji pekee!


Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Nimeongelea wengi hapa tuliopoa JF ni wa digital, lakini hatuwafikirii wenzetu ambao nafasi haziwapi uwezo huo mara moja, huku ndiko tunakosema mfumo wa kubebana wenye uwezo na wasio nacho kuachwa walivyo, na pengine kile kidogo walichokuwa wanakitegemea kuwakatia kabisa, huu ni unyama na dalili ya watu tunaotetea kukosa kuonja ubinadamu kwa watanzania walio wengi wanaotegemea huduma hiyo. Kwa vile mimi najitosheleza basi sioni haja kwa maskikini anayelalamika na kusononeka.

Ubinadamu gani unaoongelea hapa mbona sikuelewi?yaani watanzania waliowengi ni wakazi wa Dar pekee?hivi hujui kuwa hao waliowengi ndo hata umeme hawana?Fikiri nje ya box acha kulalama mkuu bila kuitumia a part of your brain for reasoning!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Sifa moja mbaya kabisa ninayoichukia kwa watanzania wanaishi Dar ni tabia ya kujenga hoja bila kufanya utafiti halafu unajaribu ku influence mamlaka zifuate unachoamini!Kwanza kusema watanzania wengi wanatumia analogia sie kweli hata kidogo unless unamaanisha watanzania ni wale pekee waishio Mjini hususan Dar!Nasema hivi kwa sababu tangu mfumo wa analogia uanze duniani,wakazi wa miji midogo ya wilaya karibu zote hawajawahi kutumia mfumo wa analogia bali wanatumia dishes na cable ambayo hulipiwa kila mwezi!na tumezoea!Serikali iko sahihi kabisa iwapo hiyo ni njia ya kuongeza wigo wa mapato.Watu wa Dar acheni ubinafsi na kujifikiria ninyi ndio watanzania kuliko watanzania wengine!Ninaishi Kahama sehemu ilipo migodi mikubwa miwili ya Barick,lakini pamoja na mchango mkubwa wa fedha za kigeni na mapato kutokana na dhahabu,bado huduma za barabara ni mbovu na kijilami cha kisanii ndicho kimewekwa mjini!Umeme kila uchao umekuwa ukikatika katika kwa visingizio visivyo na msingi wowote!Bado wengi wenu mnaoishi Dar na takwimu za kutupumbaza mnajipigia debe kwa visingizio eti Watanzania wengi hawana uwezo wa kununua ving'amuzi!Naipongeza serikali tena ninyi mnaojidai watanzania waliowengi mfunguke akili kwani asilimia kubwa ndio mnaofaidi fedha za ufisadi wa watumishi wa serikali!Wanaiba wilayani wanakuja Dar kuwekeza mijumba na biashara za anasa lakini mwisho wa siku pamoja na kufaidi huko mnalalamika sana!Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
Umelonga mkuu
 
Jaribu kuelewa mleta mada anaongelea nini na jaribu kusoma maudhui ya habari. Sijapinga uwepo wa Digital TV, lakini muda wa kutoka analogia na kuingia dijita ni mfupi mno na ukitilia maani mataifa ya kiafrika maendeleo bado nyuma. Ninachofahamu mataifa ya nchi za magharibi mfumo huo umebadilishwa karibu miaka kama mitatu mpaka mitano iliyopita, pima historia ya maendeleo ya nchi hizo na nchi za kiafrika. Mapema mno kufuta mfumo wa zamani. Tena ingekuwa na maoni yangu binafsi kwa kufikiria wananchi walio wengi wenye kuhitaji huduma hiyo kwa nchi nyingi za kiafrika ingehitaji miaka hata 10. Uwezo wangu wa kuwa na dish network au kutumia converter boxsi kigezo cha kila mtu kufanya.Walio katika utumishi kwa umma wafikirie umma wa watanzania kwa upana zaidi badala ya kujenga mfumo wa kufikiria wachache wenye nafasi na uwezo. Vyote digital and analogy viengeenda sambamba kwa kipindi fulani hadi wengi watakapokuwa tayari. Kujaa kwa magari Dar es Salaam si maana ya kuwa vijijini wengi wana magari.uko sawa kabisa huo mfumo wa digital nikianza na Dar hiyo cable wanayosema imeenea si kweli ipo kariakoo,ilala,baadhi ya maeneo ya magomeni,baadhi ya maeneo ya kinondoni,masaki,baadhi ya maeneo ya msasani maeneo mengine mbagala,airport,gongolamboto,tegeta,mbezi zote mbili,mpigi majoe,kigamboni nk ni maeneo yenye idadi kubwa ya watu hayana cable.Madishi niya kuhesabu 3 kwa nyumba 100 huko mikoani ambako hapakuwa na analogi madishi ya kuhesabu bado tunahitaji kujipanga
 
Hujatembea kiongozi usiwe mbishi. Jf ni sehemu mojawapo ya kujuzana. Kama kuna mtu wa Mwanza humu atukuhakikishia ninachokuambia. Mwanza kuna
Na wengine ambao mimi siwafahamu. Usiconclude kitu bila kuwa na data. Ndio maana mwenzako nimetolea mfano mikoa ambayo nina uhakika nayo tu.

Jambo moja ambalo hujamwelewa mleta mada ni maana nchi kuwa na mfumo wa cable TV, sehemu chache sana zipo kama majaribio lakini si mfumo wa Cable at all. Kwa ambao hawajatembea na kufanya ulinganifu wa maana ya cable TV wataelewa tu kwamba unachosema ndio mfumo.

Kwa Taarifa Cable TV unayosema ni mfumo wa kivigongoji kama
kwenye mada hii hapo juu. Unaweza nionyesha nyaya za Cable TM ambazo zimetandazwa miji yote hata miji uliyoitaja kwamba kila anayetaka ni kuinua simu kuita wamwunganishie? Kama ni huduma ya kitongoji fulani kama ilivyo Kariakoo, magomeni na Ilala jijini Dar huwezi kusema tuna mfumo wa Cable TV. Tunaweza kusema tuna mfumo wa simu na umeme kwa vile kila sehemu mijini na baadhi ya vijiji huduma huyo imetandazwa eneo karibu lote. Hapa ndipo tunaposhindwa kuelewana.

Dish nalo ni la vibosile wachache wenye uwezo hivyo huwezi kusema wote wanatumia wakati ni wachache.
 
Sifa moja mbaya kabisa ninayoichukia kwa watanzania wanaishi Dar ni tabia ya kujenga hoja bila kufanya utafiti halafu unajaribu ku influence mamlaka zifuate unachoamini!Kwanza kusema watanzania wengi wanatumia analogia sie kweli hata kidogo unless unamaanisha watanzania ni wale pekee waishio Mjini hususan Dar!Nasema hivi kwa sababu tangu mfumo wa analogia uanze duniani,wakazi wa miji midogo ya wilaya karibu zote hawajawahi kutumia mfumo wa analogia bali wanatumia dishes na cable ambayo hulipiwa kila mwezi!na tumezoea!Serikali iko sahihi kabisa iwapo hiyo ni njia ya kuongeza wigo wa mapato.Watu wa Dar acheni ubinafsi na kujifikiria ninyi ndio watanzania kuliko watanzania wengine!Ninaishi Kahama sehemu ilipo migodi mikubwa miwili ya Barick,lakini pamoja na mchango mkubwa wa fedha za kigeni na mapato kutokana na dhahabu,bado huduma za barabara ni mbovu na kijilami cha kisanii ndicho kimewekwa mjini!Umeme kila uchao umekuwa ukikatika katika kwa visingizio visivyo na msingi wowote!Bado wengi wenu mnaoishi Dar na takwimu za kutupumbaza mnajipigia debe kwa visingizio eti Watanzania wengi hawana uwezo wa kununua ving'amuzi!Naipongeza serikali tena ninyi mnaojidai watanzania waliowengi mfunguke akili kwani asilimia kubwa ndio mnaofaidi fedha za ufisadi wa watumishi wa serikali!Wanaiba wilayani wanakuja Dar kuwekeza mijumba na biashara za anasa lakini mwisho wa siku pamoja na kufaidi huko mnalalamika sana!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums

Research ya matumizi makubwa ya TV ni miji mikubwa ambako kuna wakazi wengi na watumiaji wengi ambao kwa uwiano ndio watumiaji wakubwa wa analogia kuliko unaosema wa Dish ambao ni vibosile wenye uwezo wachache. Madishi unaweza kuhesabu labda katia miji mikubwa utaona labda wapo watu 100 wanaotumia dish na walio wengi ndio walio kwenye mfumo wa analogia. Kwa utaratibu ulioanzishwa na serikali kuzima analogia ndio kusema walio wengi ambao ni watumiaji wa analogia ndio wenye kuathirika. Mpaka hapo umeipata point yangu?
 
Tembea uone mkuu, usipende kuwa mbishi bila data.

Kwa taarifa yako natembea sana tu na si Tanzania tu, navuka mabara mara kwa mara. Wenzetu zilikoanzia hiso digital bado analogia inaendelea, sisi na kiherehere tunakurupuka tu kama msemo wa kuiga kunya kwa tembo. Hahaha, inachekesha.

Mimi ujue sifikirii binafsi, naangalia kipana wananchi walio wengi na jinsi wanavyolalamika na kulazimishwa ghafla kuingia kwenye mfumo huo. Elewa mie mtetezi wa masilahi ya umma si kundi la wachakachuaji.
 
Hongera mkuu, kwa maoni na ushauri wako nafikiri vyombo husika na vyenye mamlaka hayo vimeona ushauri wako.
 
Mulikua wapi kabla haijaja hii digital mbona hatukuziona hizi hoja zenu pumba!? Niynyi ndio munaokurupuka sasa.
 
Back
Top Bottom