Serikali iachane na chaguzi ndogo - Mtatiro

Serikali iachane na chaguzi ndogo - Mtatiro

Naibu Katibu mkuu wa CUF Julius Mtatiro ameitaka serikali kuachana mara moja na chaguzi ndogo kwani ni kutapanya hela za walipa kodi bure.

Mtatiro amesema serikali inapaswa kupitisha sheria kwamba anapokufa mbunge sharti arithiwe kutoka chama kile kile bila kufanya uchaguzi upya.

Akizungumzia uchaguzi wa Arumeru alisema CCM ilipaswa kumteua mrithi bila kufanyika uchaguzi.

Mtatiro alitoa mfano wa nchi za Msumbiji na Ghana kwamba zinafuata mfumo huo.

Source: MWANANCHI

haya ndiyo mawazo Viongozi wa Karne hii... Ndiyo maana kaiuwa CUF... CDM itabidi iandalie watu kama hawa hata kuwa wanachama wa kawaida hawafai maana kwa akili hii atakuwa anaharibu kura tu...
 
Mbunge ni mwakilishi wa wananchi siyo Chama. Chama ni ngazi tu ya kugombea uwakilishi wa wananchi. Nafikiri Mtatizro ameona kuwa chaguzi ndogo ndizo zinazoua au kujenga chama na kwa upande wao CUF chaguzi ndogo zinaua chama. Anajua madhara ya kutaka chama kiteue mbunge badala ya wananchi kuchagua?

  1. Itafikia mahali watu katika chama kimoja wanaogombea nafasi za ubunge wataanza kuviziana ili kutoana dunia kwa lengo la kuwa huenda atateuliwa yeye.
  2. Itaondoa uwajibikaji wa mbunge kwa wananchi wa jimbo lake na kuweka kwa chama zaidi which is bad for development of our democracy

Nafikiri Mtatiro asubiri mchakato wa katiba mpya atoe maoni yake badala ya kutungia sheria, maana haiwezekani mbunge jimbo asipatikane kwenye sanduku la kura. Uchaguzi ndiyo njia pekee ya kupata mwakilishi wa wananchi na yeyote anayetoa mawazo mbadala ni kutaka kulirejesha Taifa miaka 30 nyuma. Matumizi gani ya pesa ambayo Mtatiro anayaongelea?, je ni yale ya kununua shahada za kura au kuhonga wapiga kura?. Kama ni kuandaa uchaguzi kupitia Tume sidhani kama kuna gharama ya kutisha. Gharama zinaletwa na vyama vyenyewe kwa hela zao kama chama hakina hela kinakaa pembeni.

Constituent MP must be decided by the ballot boxes. Hiyo ndiyo demokrasia.

tume inatumia zaidi ya milioni miambili kuandaa uchaguzi kwa mtindo alio usema mtatiro ni sahihi hizo milioni miambili ktk jimbo moja zingetumika kujenga bwawa la mifugo hapo vp. Tuwe jamani wabunifu kupunguza gharama za matumizi ili tujenge nchi kama cdm inaunga mpango wa kurudia uchaguzi basi hawana tofauti na ccm. Kuna baadhi ya wa bunge wa cdm wameliona hili na walikwisha litolea kauli. Nikweli gharama nyingi toka igunga, arumeru, chaguzi za madiwani na sasa zenj kuna chaguzi una kuja baada wa ule mwingine wa uzini tuacheni uvivu wa kufikira jambo zuri sio tu mpaka litoke kwa mbunge wa cdm hapana jamani komaeni kiakili
 
Nakubaliana na hoja kwamba serikali inaingia gharama kubwa kushughurikia chaguzi ndogo, wazo langu ni achukuliwe aliyekuwa mshindi wa pili bila kujali chama alichotoka maana anakuwa alipigiwa kura na wananchi wote. Kumchukuwa mtu kutoka chamani mmmh!?

Watauana watu balaa, mtu anaona yeye mshindi wa pili na mbaya hata zaidi anahisi kuchakachuliwa .... ni kum-BWM tu aurithi ubunge. Hiyo itamaanisha Insecurity to MPs.
 
Naibu Katibu mkuu wa CUF Julius Mtatiro ameitaka serikali kuachana mara moja na chaguzi ndogo kwani ni kutapanya hela za walipa kodi bure.

Mtatiro amesema serikali inapaswa kupitisha sheria kwamba anapokufa mbunge sharti arithiwe kutoka chama kile kile bila kufanya uchaguzi upya.

Akizungumzia uchaguzi wa Arumeru alisema CCM ilipaswa kumteua mrithi bila kufanyika uchaguzi.

Mtatiro alitoa mfano wa nchi za Msumbiji na Ghana kwamba zinafuata mfumo huo.

Source: MWANANCHI

Mie nakubaliana naye kimsingi ya kwamba sio wachague kutoka chama kile kile ila yule aliyekuwa mshindi wa pili a takeover automatically, kama ktk uchaguzi alifikisha kiwango fulani cha kura.
 
Pesa zilizoibwa EPA na wanazoendelea kujichotea, mafuta ya serikali yanayotumiwa na vigogo katika mambo yao binafsi, kina Malima kulala vyumba vya dola 600 kwa siku na kuporwa na maCD, ........kwa kifupi Tz pesa ipo hata kama wabunge wote watakufa au kushindwa kesi....pesa ya kurudia uchaguzi zipo. Ni wewe usiyejua ziko wapi ndiye unayesema hakuna pesa
Tusipoangalia hii hoja imetoka kwa nani, nadhani tunaweza kuijadili vizuri.

Serikali inaingia gharama sana na hizi chaguzi za kila siku. Watanzania tunakufa mno na nafasi za kuchaguliwa ni nyingi mno vile vile. Miaka mitano hii tutafanya chaguzi mpaka tutakinai

Kuna Muakilishi wa CCM kwenye Baraza la Wawakilishi la Zanzibar jimbo la Bububu amekufa mwezi uliopita, mwezi ujao kutakuwa na uchaguzi huko

Tunahitaji kukaa chini kama taifa na kutafakari namna ya kuokoa hizi fedha zinazotumika kwenye chaguzi ndogo
 
mtatiro kifipa maana yake ni ganuki...ww unaona ghalama kubwa kwenye demokrasia wakati kuna watu wanafanya ufisadi wa mabilioni.Naomba Allah aendelea kujaalia chaguzi ndogo zifanyike nyingi kabla ya 2015.Tunaitaji watu wa kupigania matumizi mabaya ya kodi za walala hoi katika nchi hii...
Mungu ibariki Tanzania na atupe chaguzi ndogo nyingi ....
 
Wazo zuri Mkuu Kwani Uzini CHADEMA Walitumia Milioni MIA TATU Waliambulia Kura 285, sasa huku ni kufuja fedha za umma hujawaangalkia CCM walitumia zaidi na Setrikal;i zaidi ni kweli ip[o haja ya kumpa mshindi wa pili nafasi kwani alishapigiwa kura na wqananchi. Taarifa Kutoka kwa Zitto kabwe amesikika Kuwa CHADEMA ARUMERU Wametumia BILIONI MOJA NA MILIONI MIA MBILI Hili ni balaaaaaa

Tatizo letu watanzania tuna tabia ya kutaka kuwa cost conscious kwa vitu ambavyo tunaona tuna faidika navyo na si kama desturi ya kufuata ukweli.Hivi wanademokrasia wa kweli ni haki kuangalia cost au ni ukweli ni kuangalia Demokrasia imesimikwa kwa kiasi gani kwa faida ya wananchi haijalishi wataungana na dhamira ya demokrasia yao waliyoitafuta kuzalisha kiasi gani cha kupita mara dufu ya gharama walizotumia kuinvest demokrasia yao hiyo.

Haya ya Mtatiro siitaji hata apewe nafasi ya kusikilizwa kwa kuwa tayari Gagnija akimjibu Angel Msofe anasema "Kama umesoma mawazo yangu. Huu ni wivu tu kwa kuwa wanaumizwa na mafanikio ya CDM." Ukweli CUF kwa Tanzania bara ndio hivyo tia maji tia maji,hivyo anajaribu kuwasituha CCM kuwa kwa kuwa nao hali si shwari na kuwa CDM wanaonekana kwenye kuelekea kwenye ustawi basi wastukie kucheza faul ya kuibua misemo na mambo ya kubuni juu kwa juu kupitia NEC kuwa Serikali ipendekeze ushauri wake huo kwa nia ya kuondoa gharama kwa Serikali, hivyo iwafaidishe wao na ikibidi CCM japo hawakumtuma.

Demokrasia daima itapandikizwa na kujengwa kwa gharama kubwa haijalishi vipi au kiasi gani cha pesa kinatumika,huo ndio ukweli, mfano kupitia uchaguzi wa Aumeru. Sio demokrasia imeingia tu kwa wanaarumeru bali Nchi nzima imefaidika sana kupitia uchaguzi huo wa kidemokrasia na demokrasia imepanuka na watu wamejifunza mambo mengine sana kuhusu uchaguzi,ambayo ni taofauti kama uchaguzi ungekuwa nchi nzima concentration isingekuwepo kama ambavyo TAIFA zima liliweka macho na masikio yake Arumeru na kuona mambo mengi kwa jicho pana na la umakini mkubwa na kuibua mambo ambayo katika chaguzi za kawaida yalikuwa yanaonekana ya kama ya kawaida.

Kwa sasa kupitia uchaguzi wa Arumeru mambo ya kizamani business as usual sasa ukulasa huo umefungwa na kuzikwa.Timu ya mgombeaji ubunge au udiwani haiwezi kupanda kwenye jukwaa wakamwaga tuhuma juu ya mtu zisizo na ushahidi mbele ya wananchi,hapo hapo hawawezi kutukana au matumizi ya lugha mbaya na bado jamii ikakubaliana nao kama ilivyokuwa zamani.Hayo yaliyokuwa yakifanyika zama hizo wakati huo yalikuwa wakati huo lakini sio sasa, na yamekuwa bye bye kwa sasa.Hivyo hiyo ndio faida ya chaguzi ndogo ambazo zinabeba akili ya Taifa zima kimtizamo.

Hayo ya mabilioni mangapi yametumika, kiuchumi,kwanza pesa hizo zimeingia kwenye jimbo husika na kupanua hali ya uchumi ya jimbo husika na kuleta ustawi kwa umma eneo husika. Hakuna cha hofu kwani zimeenda kustawisha nchi tofauti hivyo tuone hofu na mashaka na kuwa kuna umuhimu wa kusitisha uku tukitumia opportunit cost method theory kuwa gharama za uchaguzi zina umuhimu zaidi ya demokarsia kwa kuwa zile gharama zinakwenda kusitawisha Taifa jingine.Hivyo tuone kuwa demokrasia haina maana kwetu kuliko gharama tutakazo serve kupitia chaguzi hizo ambazo bado ni za kwetu wenyewe kwa kuwa jimbo lenyewe ni ndani ya Taifa letu wenyewe na bado kodi italipwa na kuludi kwa Taifa lile na Serikali ile ile.

Kama vipi huyo Mtatiro ni sizitaki mbivu hizi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!Sungura nakuambia aahhhhaa aaahhaaa!!!![Kana nke aghutana Mura atighee urwambeeee!!!]
 
RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA AUMBUKA.
Rais mstaafu ben mkapa ni mmoja kati ya viongozi wa ccm walioumbuka katika kampeni huko arumeru. akiwa katika kampeni mkapa alikwenda mbali na kuanza kutoa maneno ya kejeli kwa vicent nyerere kwa kumwambia kwamba yeye sio mtoto wa nyerere wakati anajua fika sio kweli hata kidogo.
SASA MIMI NAOMBA NIMUULIZE SWALI BEN MKAPA KAMA IFUTAVYO, Najua anakumbuka wakati wa utawala wake aliwatukana wa tz akawaambia kwamba wa tz ni wavivu wa kufikiri,sasa kama hivyo ni kweli hivi yeye haoni na yeye ni mvivu wa kufikiri kwa kusahau kuwa vicent nyerere ni mtoto wa nyerere?
 
RAIS MSTAAFU BEN MKAPA AUMBUKA.
Rais mstaafu ben mkapa ni mmoja wa viongozi walioumbuka katika uchaguzi uliopita huko arumeru. akiwa katika kampeni mkapa alikwenda mbali na kuanza kutoa maneno ya kejeli kwa vicent nyerere kwa kumwambia kuwa yeye sio mtoto wa nyerere wakati anajua fika kuwa vicent ni mtoto wa nyerere.
sasa mimi naomba nimuuze swali mkapa, NAJUA ANAKUMBUKA WAKATI WA UTAWALA WAKE ALIWATUKANA WATZ KWA KUWAAMBIA KUWA WAO NI WAVIVU WA KUFIKIRI, SASA KAMA NI HIVYO NI KWELI, NA YEYE HAONI KUWA NI MMOJA KATI YA WA TZ AMBAO NI WAVIVU WA KUFIKIRI KWA KUSEMA VICENT SIO MTOTO WA NYERERE WAKATI ANAFAHAMU SIO KWELI.
 
Believe me kama tutaruhusu mshindi wa pili ndiye achukue ubunge automatically mbunge anapofariki ili kuokoa gharama. I swear in the name of GOD Leo Mh. Highness Kiwia na Salvatory MachemliWASINGEKUWA HAI, wangewaua kabisa CCM.

Kwa mantiki hiyo mbunge wa Ilemela angekuwa Anthony Diallo (CCM) na Mbunge wa Ukerewe angekuwa Getrude Mongella (CCM).

Je haya ndiyo anayo pendekeza Mtatiro?

Mimi bado ninashauri kama tumeona kuendesha chaguzi ndogo imekuwa gunia la MISUMARI ili kubana matumizi tuondokane na WABUNGE WA VITI MAALUMU. Ni pesa nyingi sana tuta save tukiachana na hawa wabunge wa viti maalumu na pesa hizo zinaweza kugharamikia by election zote, kuliko kutafuta short cut kwenye democrasy. Mtatiro inabidi uangalie mambo in four dimension not uni-dimension
 
Tusipoangalia hii hoja imetoka kwa nani, nadhani tunaweza kuijadili vizuri.

Serikali inaingia gharama sana na hizi chaguzi za kila siku. Watanzania tunakufa mno na nafasi za kuchaguliwa ni nyingi mno vile vile. Miaka mitano hii tutafanya chaguzi mpaka tutakinai

Kuna Muakilishi wa CCM kwenye Baraza la Wawakilishi la Zanzibar jimbo la Bububu amekufa mwezi uliopita, mwezi ujao kutakuwa na uchaguzi huko

Tunahitaji kukaa chini kama taifa na kutafakari namna ya kuokoa hizi fedha zinazotumika kwenye chaguzi ndogo

See highlighted. Usije ukakuta hofu ni CHADEMA KUSHIKA NAFASI YA PILI KWENYE UCHAGUZI WA BUBUBU!! Kiukweli sidhani Mtatiro kwa usomi wake angeweza kusema hivi bila kuwa na mawanda mazuri na amekuwa misquoted.
 
Nchi yenye Demokrasia ya kweli duniani India hawarithishi; wanafanya Uchaguzi kuchagua Mbunge endapo kiti hicho kinakuwa wazi; unajuwa wasingempata Indira Ghandhi bila kura; kama ni kuridhisha

Aache naona amekosa itikadi ameona jimbo lao limechukuliwa kwa kishindo na CCM na wanachagua maamuzi mengine tuwarithishe mpaka Uchaguzi Mkuu... na kama aliyeridhi kazi yake ni kula na kulala?

Nchi ina pesa za Uchaguzi Ndogo, kama ilivyo na pesa za Madini...
 
Kilamtu ana haki yakutoa mawazo pasipo kukiuka lakini kuhusiana na hili huyu bwana anataka kuleta Utawala wa kifalme. Chama cha CUF kinge shiriki na kushinda Sidhani kama ange pendekeza hivyo. ''Amakweli Mtoto wa mchawi asipo rithishwa Uchawi Huenda akapewa roho mbaya '' Walio shindwa ni vyama vingine (TLP,CCM,n.k) CUF, maumivu yanatoka wapi? Au ndo' adui muombee njaa? CUF mna kufa taratibu Huenda mazishi yenu yakawa pamoja na CCM. Ukweli ni kwamba, CDM imeshinda tuna amini Ushindi ni Wa waTanzania wote Walioko Arumeru Mtatiro Tuliza mtima Kama ipo ipo tu Usiforce!


<sapal kihavah>
 
Hawa watu wa cuf huwa Akili zao hazijui kufikiria jambo,nakumbuka mwaka jana bunge la Jan,2011 mh,H.Rashidi alileta hoja binfsi ya kutunga sheria ya iwepo kambi ya upinzani isiyo rasmi, ni baada ya yeye kukosa sifa ya kuwa mw/kiti wa kambi ya upinzani ktk bunge. Sasa Mtatiro naye kaja na style yake hiyo..
 
tume inatumia zaidi ya milioni miambili kuandaa uchaguzi kwa mtindo alio usema mtatiro ni sahihi hizo milioni miambili ktk jimbo moja zingetumika kujenga bwawa la mifugo hapo vp. Tuwe jamani wabunifu kupunguza gharama za matumizi ili tujenge nchi kama cdm inaunga mpango wa kurudia uchaguzi basi hawana tofauti na ccm. Kuna baadhi ya wa bunge wa cdm wameliona hili na walikwisha litolea kauli. Nikweli gharama nyingi toka igunga, arumeru, chaguzi za madiwani na sasa zenj kuna chaguzi una kuja baada wa ule mwingine wa uzini tuacheni uvivu wa kufikira jambo zuri sio tu mpaka litoke kwa mbunge wa cdm hapana jamani komaeni kiakili

Wazo nzuri,lakini je hili ni vema likafanyika katika mazingira ya nchi hii?kwa mfano,vipi kuhusu rushwa itaongezeka au itapungua?vipi kuhusu mauaji ya waheshimiwa yatakua kwa kasi au?vipi kuhusu demokrasia itakuzwa au itabanwa?sasa mtoa mada ameangalia matumizi ya pesa ya mlipa kodi kwa upande mmoja tu,je vipi yey akijiuliza'je ujenzi wa demokrasia unagharama?'je budget ya chaguzi ndogo hutengwa na kupitishwa na bunge kila mwaka?je wabunge wa chama chake wamo bungeni?je walitoka nje kupinga maamuzi dhidi ya dhuluma hiyo kwa pesa ya mlipa kodi?NAOMBA TUEPUKE CHEAP POPULARITY.
 
Tuache kuchagua Wazee na Majina yao kuongoza bunge, bungeni hafai kijana aje amuondoe na miaka yao bungeni

Samuel Sitta Miaka 45
Abdallah Kigoda 40
Anna Makinda 42
Stephen Wassira 50
Mzee Ndesamburo 15
Anna Abdalla 48

Na wengi upande wa Unguja na Pemba na zaidi wapo TANGANYIKA

* Kwa Urais; kwa sasa tunahitaji hekima, kijana hapana hafai tuna mali nyungi, tuna matatizo mengi, - rais wa sasa hayajui sababu yeye alibebwa madarakani; asituvunjie nchi kwa neema zake hatutaki kuchaguliwa...
 
Baada ya kushindwa vibaya na mnyika hapa ubungo naona sasa mtatiro anataka aingie bungeni baada ya mbunge mmoja wa cuf kufa ama kuachishwa uanachama. Asubiri hamad aachishwe arafu chama chake kimteue kuwa mbunge kule pemba.Ukiona unafikia hatua unaombea mwinzio afe ili wewe ufanikiwe ujue umeishiwa sera na utakufa maskini. Pole sana mtatiro
 
Sasa nimeshapata picha halisi ni kwanini CUF hawakumsimamisha mgombea!:A S 39:
 
Back
Top Bottom