Serikali iachane na chaguzi ndogo - Mtatiro

Serikali iachane na chaguzi ndogo - Mtatiro

CUF iambie pia serikali ya swahiba wako CCM inachene na matumizi mengine ambayo ni ya anasa mfano:
- posho za tshs. 200,000 za kikao cha bunge
- magari ya anasa ya serikali aina ya 'mashangingi"
- safari nyingi za mh. Rais ambazo hazihijiwi na bunge, mkaguzi mkuu wa serikali
- uanzushwaji wa mikoa, wilaya kwa ajili ya kuwapatia 'washkaji' wa CCM vyeo
- tiba nje ya nchi badala ya kuwekeza ktk mahospitali yetu nchini ili kila raia apate huduma bora za afya
-mikataba mibovu na 'wawekezaji' toka nje
n.k n.k
 
Nakubaliana na msimamo wa CUF au Mtatiro kwani ni vema wananchi wakachagua chama na sera zake, then ikitokea kifo au sababu nyingine yeyote chama hicho kinaweza kumuweka mbunge au kiongozi mwingine. Hii ina faida kwa Taifa, Vyama na wananchi.

a. Taifa kupunguza gharama na tume kujiandaa kwa uchaguzi mkuu tu

b. Vyama kupunguza gharama na kuuza sera badala ya watu (hivyo kujenga taasisi)

c. Wananchi kuendelea kufanya kazi na kujipanga na uchaguzi baada ya miaka ya mitano kuliko pressure na time consuming efforts ambazo kimsingi hazi badili chochote katika utendaji wa kazi ya serikali iliyoko madarakani.
 
Ni wale waliovulugana CUF, Hakuna cha gharama wala nini..Wewe sema tu labda kwa vile CCM ambayo wewe CUF ni tawi lake mmeangukia gua.. je unajua ni fedha kiasi gani zinaibwa, sdo ni kheli zitumika kwenya kumtafuta mwakilishi wa wananchi kuliko zillizochukuliwa na mafisadi rafiki yako wa CCM pamoja na kichama chako mjikombo-- au CUF.
 
Du wadau kufikiri ni kazi kweli,inakuwa vema kama mtu anafikiri vema kwa kuangalia pande zote na sio kwa hisia zaidi kama huyu ndugu yetu. Sio lazima kila wakati uongee hata unapokuwa huna la msingi kuongea. Binafsi nazidi kuona democrasia ikichukua nafasi yake jambo ambalo naliona kuwa ni endelevu sana.
 
nyinyi wanafiki gharama zinazopotea bure kurudia uchaguzi na kulikuwa na njia nzuri bila kutoa gharama nyingi. Mfano nasari alishika nafasi ya pili basi angepewa akamalizia kipindi kilicho baki. Kisinge haribika kitu
Mkuu wangu Mgongo wa paka,maoni yako yanaonyesha uelewa wako mdogo ktk mambo ya uchaguzi ktk Tanzania!
 
Acha kufa tu, m2 anaweza kushinda na akasinzia bungeni 2yrs. From there akauza ubunge kwa "mjanja" flan hivi. Mambo yakawa sawia.
 
Kwa maoni hayo ya Mtatiro Cuf haitufai watanzania wa leo na hata yeye hapana. Anacopy na kupest kutoka kwa majirani? Mbaya zaidi anacopy majibu hesabu kujibia mtihani wa kiingereza.
 
Ninapinga Mtatiro

1. Hizo pesa zinazotumika kwenye chaguzi husisimua uchumi wa eneo husika. Ajira za muda hupatikana, na hata miradi huanzishwa ambazo huduma hata baada ya chaguzi. Majimbo kama Igunga ni sehemu ambazo zimelala kiuchumi kabisa, Mzunguko wa hela hakuna. Unapoleta chaguzi ndogo, una-stimualte mzunguko wa hela.

2. Ukiweka utaratibu wa; fulani akifa automatically anapewa fulani, utasababisha watu wauane!
 
Mawazo mengine bana,yaani tuanze kurithishana huyo Mtatiro anamawazo ya kizamani sana.
 
Hizo ni gharama za demokrasia, Tatizo letu ni kushindwa kuwa focus, serikali yote ilihamia huko ndio maana hata walisahau kuwalipa Agrekko.
 
Kweli mfa maji haachi kutapatapa, ukichanganya na wivu wa cdm kushinda ARMR MS wataropoka mengi.
Mtatiro kiongozi wa chama cha siasa ni mweupe namna hiyo hata sheria za nchi hii huzijui?
Hayo unayosema si mahala pake, utayasema wakati wajanja watakapo hitaji maoni yako kuhusu katiba mpya!
 
Naibu Katibu mkuu wa CUF Julius Mtatiro ameitaka serikali kuachana mara moja na chaguzi ndogo kwani ni kutapanya hela za walipa kodi bure.

Mtatiro amesema serikali inapaswa kupitisha sheria kwamba anapokufa mbunge sharti arithiwe kutoka chama kile kile bila kufanya uchaguzi upya.

Akizungumzia uchaguzi wa Arumeru alisema CCM ilipaswa kumteua mrithi bila kufanyika uchaguzi.

Mtatiro alitoa mfano wa nchi za Msumbiji na Ghana kwamba zinafuata mfumo huo.

Source: MWANANCHI

hii ni tz, na huko ni msumbiji na ghana. Yani vinchi viwili tu vinatosha kupigia mstari jambo? Wacheni demokrasia ifanye kazi yake
 
Nadhani huo hautakuwa utaratibu mzuri hata kidogo na hata kama hao Ghana na Msubiji wanafanya hivyo nadhani wanakosea.
Watu hawachagui chama bali mtu kulingana na uwezo wake na mvuto wake kwenye jamii yake na watu ndani a chama kimoja hawana uwezo sawa na hii imethibitishwa huko Arumeru mashariki. kwasababu Msumbiji na nchi nyingine Africa huja kujifunza kwetu nadhani hili ni eneo ambalo wanahitaji kujifunza kwetu na kujiweka sawa
 
Tunaweza kufanya hivyo kama katiba mpya itaundwa na itabana walarushwa wanunua uongozi watatoweka vinginevyo wazo la mtatiro ni mavi ya chooni.namshangaa mtatiro tulipokuwa chuo kikuu cha dar alikuwa mawanaharakati wa kupignia haki za wanachuo leo hii amekuwa gamba la ccm ambalo alilipinga kwa nguvu zote wakati wa madhila ya mikopo na mambo mengine amesahau leo jamini mla ganda hasahau ila mla miwa.
 
mimi nahisi kunakuribisha mauaji kama kutakuwa na kurithishana namna hiyo. maana mtu atajua kuwa kama akimuua mshindani yeye anaingia automatically so we need to discourage such incentives. mtu asimame kwa miguu yake mwenyewe ndio gharama ya demokrasi .
Wengine wanasema, 'aliyekuwa mshindi wa pili ndio akabidhiwe jukumu'. Mimi nasema yote ni mawazo mazuri, lakin inabidi yatekelezwe kwa tahadhari. Ni mpaka tutakapokuwa na Tume Huru ya uchaguzi, uchaguzi huru na wa haki, sheria nzuri za uchaguzi na katiba bora, ndio mambo haya yatakuwa na mashiko zaidi.

Nadhan itakuwa busara kama tutayaangalia mambo haya kwenye mchakato wa katiba MPYA. Na lazima tutayaangalia tu
 
acheni unafiki tamaa za chadema. Cdm fika inajua kata ya vijibweni ina shikiliwa na cuf kulikuwa hakuna haja ya kuweka mgombea na kugawa kura.

Hivi na wewe ni GT? Unawalaumu WAPINZANI CDM waliosimamisha mgombea VIJIBWENI badala ya kuwalaumu WATAWALA wenzako CCM waliosimamisha mgombea wakati wakijua VIJIBWENI ni ya CUF? CCM A = CCM B; CUF = CCM B: CCM + CUF = SMZ

Nenda kajipange upya CUF mlishaolewa na CCM, no wonder sasa hivi CCM wanamutumia Mtatiro kupenyeza hoja ya chama kuteua mbunge mwingine pindu aliyekuwepo anapofariki.
 
Naibu Katibu mkuu wa CUF Julius Mtatiro ameitaka serikali kuachana mara moja na chaguzi ndogo kwani ni kutapanya hela za walipa kodi bure.

Mtatiro amesema serikali inapaswa kupitisha sheria kwamba anapokufa mbunge sharti arithiwe kutoka chama kile kile bila kufanya uchaguzi upya.

Akizungumzia uchaguzi wa Arumeru alisema CCM ilipaswa kumteua mrithi bila kufanyika uchaguzi.

Mtatiro alitoa mfano wa nchi za Msumbiji na Ghana kwamba zinafuata mfumo huo.

Source: MWANANCHI

Kasema haya kwa sababu CCM wameshindwa Arumeru, siku zote alikuwa wapi?
 
Back
Top Bottom