Serikali iachane na chaguzi ndogo - Mtatiro

Hiyo ni hoja ya CCM kupitia kwa acting Secretary wao Mtatiro A.K.A Julius mwenye Sigida.
 
Naibu Katibu mkuu wa CUF Julius Mtatiro ameitaka serikali kuachana mara moja na chaguzi ndogo kwani ni kutapanya hela za walipa kodi bure.

Mtatiro amesema serikali inapaswa kupitisha sheria kwamba anapokufa mbunge sharti arithiwe kutoka chama kile kile bila kufanya uchaguzi upya.

Akizungumzia uchaguzi wa Arumeru alisema CCM ilipaswa kumteua mrithi bila kufanyika uchaguzi.

Mtatiro alitoa mfano wa nchi za Msumbiji na Ghana kwamba zinafuata mfumo huo.

Source: MWANANCHI
Si aingize hayo kwenye katiba mpya inayokuja maana kwa mujibu wa katiba ya sasa mbunge akifa unafanyika uchaguzi wa kutafuta mbunge mpya na hiyo ndiyo Demokrasia "Poti kumbuka mambo mazuri gharama" so kwakuwa tumetaka demokrasia na tuwe tayari kubeba gharama zake pia
 
Demokrasia ina gharama zake brother. Sasa huyo wa kuteuliwa atakuwa na tofauti gani ni kina Vicky Kamata?

Labda tuwe tunachagua kama raisi na makamu wake, at least tunajua tunachagua mtu na atakayemrithi kama kutakuwa na tatizo. Kuteuana, hell no.

Umenena mkuu. ndiowanzao wa kupata wakina Vicky Kamata na Rwakatare
 
Uchaguzi uliomalizika juzi Arumeru Mashariki unatoa soma MOJA, kwamba watanzania wanachagua MTU na sio CHAMA. Ucahguzi wa 2010 Waarumeru walimchagua Jeremiah Sumari (CCM), Lakini juzi tu baada ya miaka 2 Waarumeru hao hao wamemchagua Joshua Nassari wa (CDM).

Hivyo kushauri kwamba mbunge anapofariki basi CHAMA kimuchague mwingine ni kawanyima wananchi haki ya kuongozwa na mtu wanayemtaka.

Ndiyo hizi chaguzi ndogo zinatumia pesa nyingi na ni kutapanya our meagre limited resources. Lakini mimi ningependekeza njia mojawapo ya kupunguza matumizi ya kuwapata na kuwagharamikia wabunge ni KUONDOKANA NA WABUNGE WA VITI MAALUMU. Just imagine tukiondokana na hawa wabunge tutakuwa tume save pesa kiasi gani zinazotumika kuwahudumia hawa wabunge wa VITI MAALUMU.

Democracy ina gharama zake, hivyo tusitafute short cut.
 
Hizi chaguzi ndogo ni muhimu sana zinawapa wananchi nafasi ya kuipelekea ujumbe serkali iliyopo madarakani
 
Wazo zuri Mkuu Kwani Uzini CHADEMA Walitumia Milioni MIA TATU Waliambulia Kura 285, sasa huku ni kufuja fedha za umma hujawaangalkia CCM walitumia zaidi na Setrikal;i zaidi ni kweli ip[o haja ya kumpa mshindi wa pili nafasi kwani alishapigiwa kura na wqananchi. Taarifa Kutoka kwa Zitto kabwe amesikika Kuwa CHADEMA ARUMERU Wametumia BILIONI MOJA NA MILIONI MIA MBILI Hili ni balaaaaaa
 
Ana idea nzuri lakini approach aliyoipendekeza si sahihi sana!!Hili kwakweli ni tatizo,mabilioni ya walalahoi walipa kodi wa bongo yanateketezwa kwenye hizi chaguzi ndogo.Nadhani uwekwe mdahalo kupata suluhisho juu ya hili aisee!!
 
Huyu anataka washiriki katika uchaguzi walogane mpaka wamalizane, huo ustaarabu unawezekana kwenye nchi nyingine lakini kwetu Tanzania naona bado kabisa na hasa pande zetu za mkoa mpya wa Katavi, Kigoma, Tabora na Rukwa ambapo kumuondoa mtu ni dakika, kwa sababu mtu akiwa mshindi wa pili ana uhakika akimuondoa mshindi wa kwanza yeye ndo atakalia kiti iwe isiwe,sasa kwa nini apate taabu ya kumuondoa mshindi wa kwanza ili achaguliwe yeye
 
Uchaguzi uliomalizika juzi Arumeru Mashariki unatoa soma MOJA, kwamba watanzania wanachagua MTU na sio CHAMA. Ucahguzi wa 2010 Waarumeru walimchagua Jeremiah Sumari (CCM), Lakini juzi tu baada ya miaka 2 Waarumeru hao hao wamemchagua Joshua Nassari wa (CDM).

Hivyo kushauri kwamba mbunge anapofariki basi CHAMA kimuchague mwingine ni kawanyima wananchi haki ya kuongozwa na mtu wanayemtaka.

Ndiyo hizi chaguzi ndogo zinatumia pesa nyingi na ni kutapanya our meagre limited resources. Lakini mimi ningependekeza njia mojawapo ya kupunguza matumizi ya kuwapata na kuwagharamikia wabunge ni KUONDOKANA NA WABUNGE WA VITI MAALUMU. Just imagine tukiondokana na hawa wabunge tutakuwa tume save pesa kiasi gani zinazotumika kuwahudumia hawa wabunge wa VITI MAALUMU.

Democracy ina gharama zake, hivyo tusitafute short cut.
Maoni mazuri kabisa mkuu! Gharama za kuhudumia wabunge wa viti maalumu ni kubwa sana,na wengi wao hawana tija. Pili majimbo ya uchaguzi huko Zanzibar yagawanywe upya. Watu Milioni moja na nusu wabunge 70!! Tatu liingizwe sharti muhimu,wagombea wote kupimwa Afya zao kabla ya kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
 
Demokrasia ina gharama zake brother. Sasa huyo wa kuteuliwa atakuwa na tofauti gani ni kina Vicky Kamata?

Labda tuwe tunachagua kama raisi na makamu wake, at least tunajua tunachagua mtu na atakayemrithi kama kutakuwa na tatizo. Kuteuana, hell no.
Mkuu hii ni hatari watu watauana kisa ubunge ni heri tu tuseme wanachama wa chama kilichoshinda ubunge kwenye jimbo wachague mbunge wao kwa gharama za chama
 
Nakubaliana na hoja kwamba serikali inaingia gharama kubwa kushughurikia chaguzi ndogo, wazo langu ni achukuliwe aliyekuwa mshindi wa pili bila kujali chama alichotoka maana anakuwa alipigiwa kura na wananchi wote. Kumchukuwa mtu kutoka chamani mmmh!?

hofu yangu ni kuwa vyama vilivyoshindwa watafanya ujasusi kwa wabunge ili wazichukue nafasi zao, matukio ya mwanza yameniogopesha
 
Naibu Katibu mkuu wa CUF Julius Mtatiro ameitaka serikali kuachana mara moja na chaguzi ndogo kwani ni kutapanya hela za walipa kodi bure.

Mtatiro amesema serikali inapaswa kupitisha sheria kwamba anapokufa mbunge sharti arithiwe kutoka chama kile kile bila kufanya uchaguzi upya.

Akizungumzia uchaguzi wa Arumeru alisema CCM ilipaswa kumteua mrithi bila kufanyika uchaguzi.

Mtatiro alitoa mfano wa nchi za Msumbiji na Ghana kwamba zinafuata mfumo huo.

Source: MWANANCHI

ukisema watu warithishane, ki-democrasia siyo sahihi.

ukisema mshindi wa pili ndo awe achukue kiti, tutawazika wengi.

chaguzi ndogo ziendelee, na kama ccm wanaogopa, waseme wao, siyo kumtumia mtatiro.
 
Wengine wanasema, 'aliyekuwa mshindi wa pili ndio akabidhiwe jukumu'. Mimi nasema yote ni mawazo mazuri, lakin inabidi yatekelezwe kwa tahadhari. Ni mpaka tutakapokuwa na Tume Huru ya uchaguzi, uchaguzi huru na wa haki, sheria nzuri za uchaguzi na katiba bora, ndio mambo haya yatakuwa na mashiko zaidi.

Nadhan itakuwa busara kama tutayaangalia mambo haya kwenye mchakato wa katiba MPYA. Na lazima tutayaangalia tu

Ni kweli, hili linahitaji mjadala mkubwa kwenye Katiba mpya. Mawazo yangu 'achukuliwe mshindi wa pili IWAPO alipata angalau theluthi moja ya kura zote. Vinginevyo uchaguzi urudiwe!
 
Hivi huyu jamaa amekuwaje sikuhizi?
Mbona kipindi kile maandamano ya kupinga ufisadi alikuwa kichwa sana jamaa huyo yaani alivyopanda jukwaani nakumbuka mpaka sasa yaani alikuwa ana mwaga point balaa hivi ni nini kimemsibu huyu ndugu yetu!
 
Back
Top Bottom