Serikali, hiki mnachokifanya hakikubaliki!

Serikali, hiki mnachokifanya hakikubaliki!

Zee la madawa

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2022
Posts
1,744
Reaction score
4,091
Hii nchi wananchi wake ni wajinga na hovyo wa kiwango cha lami inakuaje FBI, CIA na m16 watu wao hawana kinga kabisa ila hili li nchi la kimasikini mnataka kuwawekekea kinga kisa ni .... Kwahiyo wasiojukikana bila shaka wanapewa kinga zaidi wa kufanya uovu wao si ndiyo?

Ila shangaa na wewe wananchi hawajajua chochote kuhusu hii sheria mpya hii nchi ya ajabu sana na itaendelea kuwa masikini milele! Umagufulification.

FB_IMG_1685456862441.jpg

FB_IMG_1685457519628.jpg
FB_IMG_1685457514891.jpg
 
Nimeona na mpimbafu mwenzako Yeriko Nyerere amesema Magufulification...

How magufulification katika utawala wa Mh Samia?

Mnataka kutwambia mh samia hana uwezo wa kutafakari na kuamua tofauti na kilichopendekezwa?
Mkuu samahani labda Mimi nina tongo tongo!
Ninachojua mimi kwenye mchakato wa kutunga Sheria bunge halitungi Sheria bali linajadili muswada wa sheria na kushauri kipi kiongezwe na kipi kipunguzwe!

Wizara husika hukaa na kuona mahitaji ya kisheria katima wizara au Idara husika!
Wataalamu wa sheria wa wizara wanadraft mapendekezo kwa kishirikina na mwanasheria mkuu wa serikali.

Draft husika huwasilishwa kwenye kikao cha Baraza la mawaziri ambapo Rais ndiye mwenyekiti, baada ya Baraza la mawaziri kuijadili na kukubalika juu ya Hiyo Draft inaandikwa Kama Billl of law au muswada wa sheria.

Wakati wa vikao vya Bunge waziri huwasilishwa muswada huo Bungeni ili wabunge waweze kuusikia na kuujadili kwa pamoja huku wakitoa mapendekezo na marekebisho mbalimbali.

Serikali hurudi na kukaa na kupitia mapendekezo yaliyotolewa na wabunge pamoja na wadau wa swala husika.

Baada ya hapo hurudihswa tena bungeni ili kupigiwa kura na kupitishwa ili kuwa Sheria.
Aidha baada ya kupitishwa muswada huo hurudishwa kwa rais ili atie saini kuwa Sheria hiyo imeanza kutumika.
Kwa mujibu wa katiba yetu na mtiririko huo ni dhahiri kwamba sheria au mapendekezo ya Sheria yanaanza na Rais na sio wabunge unless mbunge aje na hoja binafsi katika sheria husika.

Na inapotokea Bunge na serikali wakashindwa kuelewana katika Sheria husika Rais anaweza kulivunja Bunge na tukarejea kwenye uchaguzi!

Kwa Sheria hii iliyoletwa na Waziri Simba chawene Ni Sheria inayoenda kulinda Maslahi ya Viongozi wa CCM ikiwemo Rais wabunge mawaziri na viongozi waandamizi wa serikali ambao kwa nafasi zao wanaweza kuwatumia watu wa usalama wa taifa katika kutimiza majukumu yao au kutimiza matarajio yao kisiasa.

Kufungua kinacholalamikiwa Ni kuwaongezea kinga za kijinai maafisa wa usalama wa taifa au wafanyakazi wa idara ya usalama wa taifa wanapokua wanatimiza majukumu yao.
Swali je Nani anajua mstari wa majukumu ya afisa wa usalama wa taifa kiusalama au binafsi!? Kwamba anaweza kuutwaa uhai wa mtu lakini katika Mazingira ambayo hayana uhusiano na usalama wa taifa lakini sheria itamlinda! (Kinga ya kutishtakiwa) kwa makosa ya kijinai.


Sheria inaenda kubadilishwa kwamba Idara ya usalama wa taifa haitakua Tena chini ya waziri Bali Rais!

Lakini pia kuna kuongezewa kwa kiapo Cha kutunza siri hata baada ya kustaafu au kuacha kazi, kwamba kwakua watakua na Kinga ya kijinai I maana hata makosa ya hovyo watakayofanya kwa kutumiwa na watawala hakuna namna watatoa taarifa kwa vyombo vingine vya dola au serikali nyingine!
Kwahiyo Sheria hii inaonekana kujenga Mazingira ya kuminya wakisoaji wa serikali kwa namna ya tofauti kuliko wakati uliopita!
 
Mkuu samahani labda Mimi nina tongo tongo!
Ninachojua mimi kwenye mchakato wa kutunga Sheria bunge halitungi Sheria bali linajadili muswada wa sheria na kushauri kipi kiongezwe na kipi kipunguzwe!

Wizara husika hukaa na kuona mahitaji ya kisheria katima wizara au Idara husika!
Wataalamu wa sheria wa wizara wanadraft mapendekezo kwa kishirikina na mwanasheria mkuu wa serikali.

Draft husika huwasilishwa kwenye kikao cha Baraza la mawaziri ambapo Rais ndiye mwenyekiti, baada ya Baraza la mawaziri kuijadili na kukubalika juu ya Hiyo Draft inaandikwa Kama Billl of law au muswada wa sheria.

Wakati wa vikao vya Bunge waziri huwasilishwa muswada huo Bungeni ili wabunge waweze kuusikia na kuujadili kwa pamoja huku wakitoa mapendekezo na marekebisho mbalimbali.

Serikali hurudi na kukaa na kupitia mapendekezo yaliyotolewa na wabunge pamoja na wadau wa swala husika.

Baada ya hapo hurudihswa tena bungeni ili kupigiwa kura na kupitishwa ili kuwa Sheria.
Aidha baada ya kupitishwa muswada huo hurudishwa kwa rais ili atie saini kuwa Sheria hiyo imeanza kutumika.
Kwa mujibu wa katiba yetu na mtiririko huo ni dhahiri kwamba sheria au mapendekezo ya Sheria yanaanza na Rais na sio wabunge unless mbunge aje na hoja binafsi katika sheria husika.

Na inapotokea Bunge na serikali wakashindwa kuelewana katika Sheria husika Rais anaweza kulivunja Bunge na tukarejea kwenye uchaguzi!

Kwa Sheria hii iliyoletwa na Waziri Simba chawene Ni Sheria inayoenda kulinda Maslahi ya Viongozi wa CCM ikiwemo Rais wabunge mawaziri na viongozi waandamizi wa serikali ambao kwa nafasi zao wanaweza kuwatumia watu wa usalama wa taifa katika kutimiza majukumu yao au kutimiza matarajio yao kisiasa.

Kufungua kinacholalamikiwa Ni kuwaongezea kinga za kijinai maafisa wa usalama wa taifa au wafanyakazi wa idara ya usalama wa taifa wanapokua wanatimiza majukumu yao.
Swali je Nani anajua mstari wa majukumu ya afisa wa usalama wa taifa kiusalama au binafsi!? Kwamba anaweza kuutwaa uhai wa mtu lakini katika Mazingira ambayo hayana uhusiano na usalama wa taifa lakini sheria itamlinda! (Kinga ya kutishtakiwa) kwa makosa ya kijinai.


Sheria inaenda kubadilishwa kwamba Idara ya usalama wa taifa haitakua Tena chini ya waziri Bali Rais!

Lakini pia kuna kuongezewa kwa kiapo Cha kutunza siri hata baada ya kustaafu au kuacha kazi, kwamba kwakua watakua na Kinga ya kijinai I maana hata makosa ya hovyo watakayofanya kwa kutumiwa na watawala hakuna namna watatoa taarifa kwa vyombo vingine vya dola au serikali nyingine!
Kwahiyo Sheria hii inaonekana kujenga Mazingira ya kuminya wakisoaji wa serikali kwa namna ya tofauti kuliko wakati uliopita!
Umenena sahihi mkuu...

Mimi nilikua namkosoa mtoa mada kwa kuyahusisha mabadiliko haya na umagufulification.
 
Umenena sahihi mkuu...

Mimi nilikua namkosoa mtoa mada kwa kuyahusisha mabadiliko haya na umagufulification.
Labda hukupata muda wa kutafakari aliposema Magufulication alikua anamaanisha Nini na nadhani ungemuuliza taratibu alikua analenga Sera zipi za Magufuli.
Kama nimemuelewa mimi kwa uchache ni kwamba,
Utawala wa samia yawezekana una nia ya kudhibiti wakisoaji au wapinzani wake kwa namna tofauti na Ile aliyoifanya Magufuli ambayo tunwesa kuita Magufulication I Tanzania politics.

Kwamba kwa uwazi bila kutafuna maneno aliwadhibiti wapinzani wake kisiasa na vyombo vya habari kwa kutumia vyombo vya dola kwa ujumla ikiwemo polisi na Sheria tata.

Sasa yamkini washauri wa Samia wameona njia sahihi ya kudhibiti haki hiyo ni kuifumua sheria ya usalama wa taifa na kuwaongezea kinga maafisa wa usalama wa taifa!
Kwamba makosa yoyote ya kijinai watakayofanya wakiwa wabatekeleza majukumu yao hawatashtakiwa Wala kuitwa watu wasiojulikana Tena Bali kazi ya usalama wa taifa!
Sasa unawezakuona ni umagufulication ulioboreshwa.
Lakini pia ukiangalia Sasa hivi kuna kelele zinapigwa kuutaka utawala wa Mama Samia ufanye uchunguzi juu ya matukio mbali mbali ambayo yanadhaniwa kufanyiwa na watu wa usalama wa taifa wakati wa utawala wa Magufuli.
Sasa katika kuzima kelele hizo watawala wameamua kuja na hii Sheria .
Usiniambie Sheri haifanyi kazi kurudi nyuma, Tanzania kila kitu linawezekana (rejea sheria ya bodi ya mikopo ilirekebishwa lini na matumizi yake)
Kwahiyo naamini ungehojiana nae kabla ya kumtukana.
 
Hii nchi wananchi wake ni wajinga na hovyo wa kiwango cha lami inakuaje FBI, CIA na m16 watu wao hawana kinga kabisa ila hili li nchi la kimasikini mnataka kuwawekekea kinga kisa ni ........kwahiyo wasiojukikana bila shaka wanapewa kinga zaidi wa kufanya uovu wao si ndiyo?

Ila shangaa na wewe wananchi hawajajua chochote kuhusu hii sheria mpya hii nchi ya ajabu sana na itaendelea kuwa masikini milele! Umagufulification

# mods acheni uzi upepe#

Huu mswada haujaja bahati mbaya!
Hakuna mwenye uwezo wa kuupinga, mtapiga bla blah na kuitisha makongamano ambayo kiufupi intelijensia inaweza ikayaratibu kumbe chenga la macho!
Wanaoupinga huu mswada kwa sasa kwenye mitandao ni watu wa system, ili ionekane kuna watetezi!
Huu mswada unakuwa sheria rasmi penda msipende!
Mlipiga kelele kwenye yale masuala ya cyber crime, ni kipi kilibadilika kwenye ule mswada? Si ulisainiwa na sasa ni sheria rasmi? System iliwachezesha sebene mkacheza!
Hii ya sasa linakuja bolingo na mtacheza kisha mswada unasainiwa'
 
Yaliyomo nyuma ya pazia ya maridhiano!
Uzuri ni kuwa, Raisi wa Umoja Party ajaye, anaweza badilisha hayo ili ukweli ujulikane.

This has nothing to do with Magulification, which is advocating for transparency and accountability!
 
Huu mswada haujaja bahati mbaya!
Hakuna mwenye uwezo wa kuupinga, mtapiga bla blah na kuitisha makongamano ambayo kiufupi intelijensia inaweza ikayaratibu kumbe chenga la macho!
Wanaoupinga huu mswada kwa sasa kwenye mitandao ni watu wa system, ili ionekane kuna watetezi!
Huu mswada unakuwa sheria rasmi penda msipende!
Mlipiga kelele kwenye yale masuala ya cyber crime, ni kipi kilibadilika kwenye ule mswada? Si ulisainiwa na sasa ni sheria rasmi? System iliwachezesha sebene mkacheza!
Hii ya sasa linakuja bolingo na mtacheza kisha mswada unasainiwa'
Hakuna mswada wowote wa Sheria Tanzania unakuja kwa Bahati mbaya na Kama nilivyoeleza pale juu, utaratibu wetu wa kutunga Sheria huwa unaanzia kwa Rais then unakuja kwa wananchi

Hii Sheria imekuja mahususi kabisa kwa sababu maalum na sababu kubwa Ni ku-maintai status quo! Na kuwalinda wenye madaraka kwa namna ambayo hautaleta ukakasi!
Wala taharuki kwa jamii, hasa ukizingatia matumizi ya Polisi yamekua na changamoto kubwa Sana kwani wanakosa weledi wa baadhi ya Mambo.
Sasa watu wa system wanaenda kutumika na hata kuruhusiwa kukamata na kuweka kizuizini au hata kuua na kuharibu Mali kwani Sheria inawalinda na watakua chini ya ofisi ya Rais!

Polisi watafanya uchunguzi na wahusika watajulikana Ila litakuja swala la kifungu kinachozuia kumshtaki afisa wa Idara ya usalama wa tafa kwa makosa ya JINAI na madai kali zaidi Ni kifungu kinachozuia afisa huyu kutoa taarifa kwa MTU yeyote ama akiwa kazini au baada ya kustaafu au kuacha kazi kwa namna yoyote ile.
 
Labda hukupata muda wa kutafakari aliposema Magufulication alikua anamaanisha Nini na nadhani ungemuuliza taratibu alikua analenga Sera zipi za Magufuli.
Kama nimemuelewa mimi kwa uchache ni kwamba,
Utawala wa samia yawezekana una nia ya kudhibiti wakisoaji au wapinzani wake kwa namna tofauti na Ile aliyoifanya Magufuli ambayo tunwesa kuita Magufulication I Tanzania politics.

Kwamba kwa uwazi bila kutafuna maneno aliwadhibiti wapinzani wake kisiasa na vyombo vya habari kwa kutumia vyombo vya dola kwa ujumla ikiwemo polisi na Sheria tata.

Sasa yamkini washauri wa Samia wameona njia sahihi ya kudhibiti haki hiyo ni kuifumua sheria ya usalama wa taifa na kuwaongezea kinga maafisa wa usalama wa taifa!
Kwamba makosa yoyote ya kijinai watakayofanya wakiwa wabatekeleza majukumu yao hawatashtakiwa Wala kuitwa watu wasiojulikana Tena Bali kazi ya usalama wa taifa!
Sasa unawezakuona ni umagufulication ulioboreshwa.
Lakini pia ukiangalia Sasa hivi kuna kelele zinapigwa kuutaka utawala wa Mama Samia ufanye uchunguzi juu ya matukio mbali mbali ambayo yanadhaniwa kufanyiwa na watu wa usalama wa taifa wakati wa utawala wa Magufuli.
Sasa katika kuzima kelele hizo watawala wameamua kuja na hii Sheria .
Usiniambie Sheri haifanyi kazi kurudi nyuma, Tanzania kila kitu linawezekana (rejea sheria ya bodi ya mikopo ilirekebishwa lini na matumizi yake)
Kwahiyo naamini ungehojiana nae kabla ya kumtukana.
Hapo kuna tatizo...

Hili ni jambo la Samia na kama hakulipenda alikua na uwezo wa kilibadilisha

Mtu anaposema huu ni umagufulification inategemea amesimama ipande upi...

Nijuavyo, muanzilishi wa Magufulification of africa alikua ni Prof Lumumba na maana yake ilikua kuifanya Africa ijikomboe kifikra na ijitegemee kwa kila kitu...

So unaposema mabdiliko ya sheria hii nayo ni magufulification nashindwa kuelewa...

Kwanini tusiseme hili ni la Mheshimiwa Samia?

Au tunahisi yeye hawezi kuamua hayo?
 
Yaliyomo nyuma ya pazia ya maridhiano!
Uzuri ni kuwa, Raisi wa Umoja Party ajaye, anaweza badilisha hayo ili ukweli ujulikane.

This has nothing to do with Magulification, which is advocating for transparency and accountability!
Which one is advocating for transparency and accountability hebu fafanua mkuu..

This has a lot to do with Magufulication, yeye ndio alijenga msingi wa kutumia vyombo vya dola kuwadhibiti wakosoaji wake, kwahiyo hii Ni maboresho In a more sophisticated way!
Unajua aliwahi kusema I WISH I I COULD BE AIJIIPI?

WAFUKUZE HUKO BUNGENI WAKIJA HUKU NITAWASHIGHULIKIA SABABU HUKU HAWANA KINGA?
.AKALIAMBIA GAZETI LA MWANANCHI KUWA "YOU ARE NOT FREE TO THAT EXTENT" Sasa kwa Sheria hii mpya hutaskia sehemu hayo yakisemwa mkuu! Unless umekua pro-magufuli kupitiliza hutaona Hilo! And umoja party haitasajiliwa nimekaa hapa utaniambia
 
Hapo kuna tatizo...

Hili ni jambo la Samia na kama hakulipenda alikua na uwezo wa kilibadilisha

Mtu anaposema huu ni umagufulification inategemea amesimama ipande upi...

Nijuavyo, muanzilishi wa Magufulification of africa alikua ni Prof Lumumba na maana yake ilikua kuifanya Africa ijikomboe kifikra na ijitegemee kwa kila kitu...

So unaposema mabdiliko ya sheria hii nayo ni magufulification nashindwa kuelewa...

Kwanini tusiseme hili ni la Mheshimiwa Samia?

Au tunahisi yeye hawezi kuamua hayo?
Hakulipenda kwa namna lilivyokua linatekelezwa kwa utashi wa mtu mmoja na sio swlaa la kimfumo Sasa amelileta kwa njia ya mfumo! No one will ponit finger at her.

Sahihi Sana unaposema MTU anaposem umagufulication inategemea amesimama upande you! Hii inasadifu hulka yake ya Sheria za hati za dharura na intention ya kuwadhibiti wakosoaji wake ili kulinda madaraka take na political popularity!

Kuhusu swala la Africa kujitegemea yenyewe ilikua Ni nadharia tu ya mdomo na sio in practical sense na hakua na Sera zozote za kiuchumi ambazo Ni feasible. Hakuna basis yoyote ya kifikra aliyoijenga kwa waafrica Bali alinstill fear and intimidation hakuna fikra mpya aliyoijenga tofauti na kuwafanya watu wajione wanyonge na yeye kujiona ndio mkombozi.

Mabadiliko ya Sheria hii ni Magufulication kwa sababu he was the founder of Sheria tata. Na Samia anaweza kuamua hayo na a.eamua kwa msingi huo wa Magufulication!
 
Hakulipenda kwa namna lilivyokua linatekelezwa kwa utashi wa mtu mmoja na sio swlaa la kimfumo Sasa amelileta kwa njia ya mfumo! No one will ponit finger at her.

Sahihi Sana unaposema MTU anaposem umagufulication inategemea amesimama upande you! Hii inasadifu hulka yake ya Sheria za hati za dharura na intention ya kuwadhibiti wakosoaji wake ili kulinda madaraka take na political popularity!

Kuhusu swala la Africa kujitegemea yenyewe ilikua Ni nadharia tu ya mdomo na sio in practical sense na hakua na Sera zozote za kiuchumi ambazo Ni feasible. Hakuna basis yoyote ya kifikra aliyoijenga kwa waafrica Bali alinstill fear and intimidation hakuna fikra mpya aliyoijenga tofauti na kuwafanya watu wajione wanyonge na yeye kujiona ndio mkombozi.

Mabadiliko ya Sheria hii ni Magufulication kwa sababu he was the founder of Sheria tata. Na Samia anaweza kuamua hayo na a.eamua kwa msingi huo wa Magufulication!
Naomba nikubali Kutokubaliana mkuu.
 
Back
Top Bottom