Salaam, Shalom!
Tamaduni zetu za kiafrika, huwa hatuna utaratibu wa kudai maiti. Mtu akishaaga Dunia huwa tunasamehe.
Bwana bwana, juzi tena TABIA hii isiyofaa imeibuka tena mkutanoni Furahisha Mwanza katika ziara ya Katibu wa Itikadi na Uenezi CCCM,
Kada mmoja wa chama tawala akanyosha mkono kuuliza swali, Mwenezi wa CCM ambaye ni Kijana wa Kanda ya ziwa Kutokea Kijiji Cha Kolomije Misungwi, akampa nafasi Kutoa dukuduku lake, kada huyo akasema yafuatayo.
Ombi/Swali: "Tumepata misiba miwili ya wanachama wa chama chetu, tunadaiwa Tsh. 2,100,000/= Hospitali ya Sekeu Toure Mwanza, ili kutoa miili hiyo hospitalini, tunakuomba utusaidie ili tukazike".
Mwenezi akijua kuwa, ni aibu maiti kudaiwa, akapiga chenga kama ifuatavyo;
Jibu: "Naagiza mpewe ambulance ili mwende mkazike, na ikiwa ambulance haipo, chukueni gari yangu mkazikie".
Pamoja na chenga za kisiasa ulizopiga ndugu Mwenezi, bado tatizo liko pale pale. Najua off kamera, ulitoa pesa hiyo 2,100,000/= Kutoka mfuko wa chama.
Haiwezekani ndugu wauguze mgonjwa, inatokea bahati mbaya, mgonjwa anaaga Dunia halafu Hospitali ya Serikali igome kutoa mwili kwa maziko hadi ndugu watoe pesa zote.
Serikali ni yetu sote walipa Kodi, futeni hii adha kwa wananchi maskini. Serikali ilipe gharama hizi jamani.
Chonde chonde tafadhali, maiti isidaiwe!
Karibuni🙏
Tamaduni zetu za kiafrika, huwa hatuna utaratibu wa kudai maiti. Mtu akishaaga Dunia huwa tunasamehe.
Bwana bwana, juzi tena TABIA hii isiyofaa imeibuka tena mkutanoni Furahisha Mwanza katika ziara ya Katibu wa Itikadi na Uenezi CCCM,
Kada mmoja wa chama tawala akanyosha mkono kuuliza swali, Mwenezi wa CCM ambaye ni Kijana wa Kanda ya ziwa Kutokea Kijiji Cha Kolomije Misungwi, akampa nafasi Kutoa dukuduku lake, kada huyo akasema yafuatayo.
Ombi/Swali: "Tumepata misiba miwili ya wanachama wa chama chetu, tunadaiwa Tsh. 2,100,000/= Hospitali ya Sekeu Toure Mwanza, ili kutoa miili hiyo hospitalini, tunakuomba utusaidie ili tukazike".
Mwenezi akijua kuwa, ni aibu maiti kudaiwa, akapiga chenga kama ifuatavyo;
Jibu: "Naagiza mpewe ambulance ili mwende mkazike, na ikiwa ambulance haipo, chukueni gari yangu mkazikie".
Pamoja na chenga za kisiasa ulizopiga ndugu Mwenezi, bado tatizo liko pale pale. Najua off kamera, ulitoa pesa hiyo 2,100,000/= Kutoka mfuko wa chama.
Haiwezekani ndugu wauguze mgonjwa, inatokea bahati mbaya, mgonjwa anaaga Dunia halafu Hospitali ya Serikali igome kutoa mwili kwa maziko hadi ndugu watoe pesa zote.
Serikali ni yetu sote walipa Kodi, futeni hii adha kwa wananchi maskini. Serikali ilipe gharama hizi jamani.
Chonde chonde tafadhali, maiti isidaiwe!
Karibuni🙏