Serikali Dar es Salaam yafuatilia kuchanwa mabango ya CCM

PICHA za mgombea wa urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) zilizobandikwa katika eneo baadhi ya maeneo zimechanwa na watu wasiojulikana hali ambayo ofisi ya Mkuu wa Mkoa imesema inafuatilia kubaini wanaofanya vitendo hivyo.

Eneo ambalo gazeti hili limeshuhudia picha hizo zikiwa zimechanwa ni katika chuo cha teknolojia Dar es Salaam.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi alisema, “tutalifanyia kazi suala hilo na ngoja tuanze kulishughulikia kwa kuwa lipo ndani ya mkoa wangu ina maana lipo chini yangu pia,” alisema Lukuvi.


Gazeti hili lilipita katika maeneo hayo na kushuhudia picha za mgombea huyo zilizobandikwa katika mabati na kuta zilizozunguka eneo hilo zikiwa zimechanwa hali iliyoleta maswali mengi kwa watu wengine waliokatisha katika eneo hilo.


Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya watu hao ambao hata hivyo hawakupenda majina yao yaandikwe gazetini walisema kinachotakiwa kufanywa kwa sasa ni kwa mamlaka zinazohusika kuwatafuta waliofanyakitendo hicho ili wafunguliwe mashitaka.

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba alipozungumza na gazeti hili, alisema, “kwa sasa siwezi kusema neno lolote kwa kuwa si mhusika wa mkoa huu, ingekuwa hapo zamani wakati huo mkoa unatambulika kama mkoa wa Mmakamba ningeweza kulisemea suala hilo,” aliongeza katibu huyo.


Maoni
Acheni hizo na nyie bwana mambo ya CCM yaenze kutumia fedha za serikali kuyashughulikia. CCM watafute namna yao watakayoweza kuyalinda mabango yao. Kama zingechanwa za chadema au CUF serikali ingezishughulikia? Mambo ya nchi ndo yanaponichoshaga hapo.
Kwa maoni hayo umesema jambo la maana maana ni ukweli ulio wazi.
 
Kova na Lukuvi wote wanatetea mkate wao wa kila siku wakale wapi jamani.

Iyo ya chama kimeshika hatamu imenifurahishaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Nakumbuka mwaka 2005 Chadema ilibandika posters nchi nzima zenye portraits za Freeman Mbowe (mgombea urais wa chama hicho) zikimuonyesha Mbowe akiwa mbele ya bendera ya taifa (siyo bendera ya Chadema). Lewis Makame wa Tume ya uchaguzi (NEC) alikuja juu na kusema kufanya hivyo ni kwenda kinyume cha kanuni za kampeni!

Makame alishangaza wengi! Kukataza bendera ya taifa ambayo daima nu kitu cha kuonyesha mshikamano wa wananchi pamoja na tofauti zao za kisiasa?

Kule Marekani,mwaka 2008 kampeni za vyama vyote viwili Democrat na Republican walikuwa wanapeperusha bendera za taifa. Kulke Lebanon, wakati wa mikutano wafuasi wa vyama vya siasa wamepgwa marufuku kubeba bendera za vyama, isipokuwa zile za taifa tu!!!!

Lakini baadaye Makame aliona kosa lake na hakufuatilia. Lakini inaonyesha jinsi mtu huyu alivy na reflex action katika dosari zote azionazo katika vyama vya upinzani, kuliko zile za chama tawala, kilichomuweka pale.
 
Nakumbuka mwaka 2005 Chadema ilibandika posters nchi nzima zenye portraits za Freeman Mbowe (mgombea urais wa chama hicho) zikimuonyesha Mbowe akiwa mbele ya bendera ya taifa (siyo bendera ya Chadema). Lewis Makame wa Tume ya uchaguzi (NEC) alikuja juu na kusema kufanya hivyo ni kwenda kinyume cha kanuni za kampeni!

Makame alishangaza wengi! Kukataza bendera ya taifa ambayo daima nu kitu cha kuonyesha mshikamano wa wananchi pamoja na tofauti zao za kisiasa?

Kule Marekani,mwaka 2008 kampeni za vyama vyote viwili Democrat na Republican walikuwa wanapeperusha bendera za taifa. Kulke Lebanon, wakati wa mikutano wafuasi wa vyama vya siasa wamepgwa marufuku kubeba bendera za vyama, isipokuwa zile za taifa tu!!!!

Lakini baadaye Makame aliona kosa lake na hakufuatilia. Lakini inaonyesha jinsi mtu huyu alivy na reflex action katika dosari zote azionazo katika vyama vya upinzani, kuliko zile za chama tawala, kilichomuweka pale.

Aliamriwa na Mukapa...
 
Wananchi hawana shida na CCM tena hawataki hata kusikia juzi waligomea kupanda madaladala yenye picha za chagua kikwete chagua ccm,njia nzima ya barabara ya uhuru hata karibu na ofisi ya Lukuvi picha za chagua Zungu chagua kikwete zote zimechanwa,manake utatafakari mwenyewe hata wafanye hira za aina gani watu wamewachoka kabisa
 
hahaaaaaa wamechukia mgombea wao kabanduliwaaaaaa.......hahaaaaa hhiiiiiiiiiiii kumbe mkibanduliwa inaumaaa eeeh
 
Chanachana mahali popote ukiikuta, chana tu usirembe chana tu
 
Hata mimi nikikutana nayo nayachana tu, hawana mpya. Uongo tu na kulaghai wadanganyika na wizi wa kura ndo sera zao! Hivi watu hawamjui rais wao mpaka wabandikiwe mabango kumuchagua kama ametekeleza ahadi zake?? Maana wanasema ilani wametekeleza, sasa hofu ya nini na mabango kibao?

Kibaya cha jitembeza na chema chajiuza! Mtajitembeza sana na mabango yenu mwaka huu lakini hatudanganyikiiiiiii!
 
Mwaka 2005 Jaji Lewis Makame alifanya kwa mujibu ya sheria iliyokuwa active: Tendeni basi haki... matatizo ya bunge lenu musiwapelekee wasiohusika.
 
Hizi ndio zile Mzee Ndesamburo anaita 'deals'. Wamebandika mpaka picha ya utoto ya mkwere na mama yake! Wameshachukua cha juu haoooooooooooo wamewahi kugombea ubunge!
 
duuh hii serikali ya ajabu sana,mambo yote ya kipuuzi wanafuatilia kasoro ya maana kama mafisadi kushughulikiwa.

Kuchanwa mabango ya wagombea ni jambo la kawaida duniani hio ni njia moja wapo ya wananchi kuonesha kwamba hawamuungi mkono mgombea muhusika.sasa kama serikali itaamua kufuatilia wananchi wote ambao wanaonesha kuwapinga wagombea fulani kwenye maeneo yao kwa njia yakuchana au kung'oa mabango yao ya kampeni watakua na kazi nzito sana wakati huu wa kampeni.


au mabango ya ccm tu ndio yanafuatiliwa? lol serikali yetu imejaa vikatuni vya kila haina.
 
Upinzani sio kuwa na tabia ya kihuni.

its part of the game,tatizo lenu mmezoea mambo ya kiufalme na kutaka kila kitu muungwe mkono. Maisha hayako hivyo lazima mkubali kupingwa, kama hamkubaliwi na kundi fulani hio ni kawaida kwani maovu mnayofanya ni makubwa wana haki ya kuwapinga.
 
Upinzani sio kuwa na tabia ya kihuni.

Mtu akiwa na tabia kama Viongozi wa CCM, Vibaraka wao (mafisadi aka wanachama), Tume ya Uchaguzi (hasa wasimamizi wa majimbo), Ofisi ya Msajili (Kama ulimsikia Tendwa BBC jana) basi wewe ni SHETANI. Kwa hiyo kuchana mabango ni kuepusha kichefuchefu
 
Back
Top Bottom