Kuna kitu watu lazima tufahamu,ukizungumzia gesi au madini yaliyopo tanzania ni sawa kumsubiri Masihi au yesu kristo kwamba atarudi Duniani,tatizo letu watanzania hatuna fikira huru,wasomi na wasio soma hatujielewi kabisa tumekuwa kundi moja.Hivi leo hii ukisimama nakujipiga kifuani ukisema Tanzania ina madini madini hayo yako wapi? tangia Babu zetu na sisi vizazi hivi madini yametusaidia nini na yana maana gani katika kizazi hiki na kijacho? wewe uliyepo Arusha,Tanga,Mbeya,Shinyanga ,Geita na Mwanza au popote pale ulipo Tanzania hii madini haya unayoyatamka kila siku yamekusaidia nini katika maisha yako ya kila siku? Watanzania tumerogwa au tunaumwa ugonjwa wa kutojitambua maana tunapenda sana kuzungumzia vitu ambavyo havitusaidii hatutafakari na kuchunguza mambo tukila na kushiba baada ya hapo tunaisubiri kesho na tunandoto kubwa na rasilimali zilizopo hapa kwetu,dhahabu tunayoizungumzia au madini kwa ujumla siyo vyetu ijapokuwa vipo katika nchi tuliyozaliwa ni vya wakubwa wa Dunia,mungu aliviweka hivi vitu ili kila mwanadamu katika Tanzania hii avifaidi, wakubwa wa dunia hii wametunyanganya tumebakia kuzungumza tu,Hatuna vitu ambavyo tunaweza kujivunia kwamba madini tuliyonayo yametusaidia tumepiga hatua, wakubwa wa dunia na kiongozi wao mkuu wanatumiliki sisi na hivyo tulivyonavyo kama madini ni vyao na sisi ni mali yao please tujitatambue na tuyafanye tuliyo na mamlaka nayo.