Serikali isithubutu kabisa kuingilia kufanya biashara ya kilimo bali ifanye mabadiriko katika sera za kilimo.
Sera hizo zielekeze serikali kupanga bajeti kubwa katika sekta ya kilimo kwa ajili ya kutafuta masoko.
Tuanze ndani tu kwanza kuna unequal distribution of agricultural produce, unakuta mahindi upande fulani wa nchi bei ndogo na kwingine kubwa. Soko la nje ndilo usiseme, lipo wakati wote, ni wajibu tu wa viongozi wa serikali husika kufanya mazungumzo ya kibiashara. Kwa ufupi tu, soko ndio mchawi mkubwa wa kilimo nchini achana na mitaji, machines, pembejeo n. k. Wakulima wenye mitaji wapo ila wamefirisika kwa kushindwa kupata soko zuri.
Mabadiriko ya ki-sera pia yalazimishe serikali kupanga bajeti ya kuboresha miundombinu ya kilimo. Tuna uhaba wa cold warehouses wakati huohuo tuna tuna soko lililo tayari la kitunguu kwa nchi za Zambia, DRC, Kenya, Uganda na Sudan kusini. Shida ni kuwa kuna wakati masoko haya huwa yanafurika kwa kitunguu na kuna wakati yanakuwa tupu, hapa ndipo cold facilities zinapokuja kufanya kazi ili kuimarisha bei angalau kwa 100,000 kwa gunia mwaka mzima bila kushuka. Hizi chanja za kienyeji kuhifadhi kwa muda mrefu ni changamoto. Wakulima walipie wanapohifadhi kwa gunia na serikali ifaidike, chanzo cha mapato.
Bajeti nyingine ielekezwe kwenye miundombinu ya kisasa mikubwa ya umwagiliaji. Yale maji ya ziwa Tanganyika mfano yanaweza kufanya mikoa ya Rukwa, Dodoma, Tabora, Singida izalishe mara kumi zaidi ya mikoa ya nyanda za juu kusini ya mvua nyingi kwa mwaka mzima. Watumwe watu waende mfano Australia wakajifunze kuhusu murrambidge irrigation project n. k na sehemu nyingine zilizoendelea duniani kwa kilimo.
Nina mengi sana ya kuandika labda niandae uzi maalumu siku moja. Kilimo kina pesa endapo kitachukuliwa serious, Australia kwa mfano inaingiza wastani wa usd bilioni 62 kupitia kilimo, USA wastani wa usd 200+ bilioni kwa mwaka. Wakati huohuo benki ya dunia inakadiria kuwa thamani ya kilimo na shughuli za uzalishaji wa bidhaa za kilimo barani afrika itafikia dola trilioni 2 za kimarekani mwaka 2030 kutoka usd 400 bilioni kwa sasa. Kwa hio utaona ni jinsi gani soko la afrika tu lilivyo endapo tutajipanga vyema.