mwakajingatky
JF-Expert Member
- May 30, 2018
- 555
- 909
SERA MPYA YA KUSIMAMIA AJIRA YA WALIMU IFIKAPO SEPTEMBA 2023
Wasalaamu wapendwa, natumaini tuwazima wa afya!
Nimesikia chama cha Walimu kimepinga vikali. Mimi nadhani kuna mambo tunachanganya. Tuna haja ya kuwa na chombo maalum cha kusimamia taaluma ya ualimu. Nikimanisha Bodi ya Ualimu.
Hii imekuwa danadana muda mrefu na siasa zimeingia na hata walimu walio wengi wanapinga kwa kigenzo cha eti kutakuwa na kulipia ada ya bodi. Wenzetu madaktari wanalipia ada ya bodi wenzetu manesi na mafamasia wanalipia ada ya bodi na kupewa lesseni. Hii leseni itasaidia kuleta ubora wa kazi na ndipo leseni zitafanya kazi. Na hakutakuwa na ubabaishaji wa kiendesha mambo kufuata siasa.
Sasa kuna hili la kusema walimu watakao ajiliwa (ajira mpya) kufanya mtihani. Hapo ndipo ubabaishaji mkubwa na siasa zinataka kuchukua mkondo wake. Huo mtihani utatoka wapi?
Huo mtihani utatungwa na nani?
Huo mtahani utapima nini?
Huo mtihani nani atagharimia?
Una walimu wa masomo tofauti tofauti. Unaposema wanafanya mtihani una manisha utakuwa na mtihani kila somo kila mwalimu?
Vyuo ndivyo vyenye mamlaka ya ku-train walimu na kujiridhisha pasipo shaka walimu wameiva na vyuo vimeenda mbali zaidi zimewapa mitihani wakafaulu na hata waliofeli wakarudia mpaka wafaulu.
Leo hii wanataka kuajiliwa wanaambiwa wafanye mtihani. Hapo kuna shida. Ina maana vyuo ndivyo vyenye ubovu mpaka kuto aminika na waajiri wanataka kuwapa wafanye mtihani.
Leo ukija na hoja ya kuwa walimu wafanye mtihani wanapo ajiliwa kwa kigezo eti hawana uwezo hapo haupo sahihi. Hata kama walikuwa na ufaulu mdogo wakasoma ualimu. Je unapowafanyisha mtihani ufaulu mdogo waliokuwa nao utakuwa umepanda?
Kuna awamu kadhaa Serikali ilisha kuwa na uhaba mkubwa wa walimu wakaazisha program za walimu wa Voda Fasta, mara certificate walimu wasome mwaka mmoja. Mara degree walimu wasome miaka mitatu badala ya minne. Mara kuna uhaba wa walimu wa Sayansi hivyo program maalum zikaanzishwa ili kusaidia upungufu.
SASA LEO
Baada ya kuonekana kuna kasoro nyingi kwenye elimu eti walimu wanaoanza ajira mpya wafanye paper
USHAURI WANGU
1. Mpaka sasa bado haijaeleweka kama kuwafanyisha paper walimu wa ajira mpya kutaongeza ubora wa elimu Labda hoja iwe wahitimu wa ualimu ni wengi mtaani kwa hiyo kuwapunguza ni kuwafanyisha mtihani.
Angalizo je ikitokea kuna uhaba tena hapo badaye tutafanyaje? Tutafuta mitihani?
2. Kama kiwango cha elimu kimeshuka ili kukipandisha kuna mambo mengi ya kufanya. Mojawapo ni kuanzisha chombo maalum cha kusimamia taaluma ya ualimu. YAANI BODI YA UALIMU. NA walimu watakuwa up todate. Watafanya mitihani ya bodi na watakuwa na leseni.
Nje ya hapo tunajidanganya ndiyo maana chama cha walimu CWT kimekuja juu kupinga hilo. Tusitegemee kufanya paper kwa walimu wa ajira mpya kutaondoa matatizo tuliyonayo sisi walimu yaani matatizo ya kitaaluma.
Asante.
Comments za kujenga tafadhari
By: Mwl Ndangalasi.
Fb: Mtoto wa mkulima.
Wasalaamu wapendwa, natumaini tuwazima wa afya!
Nimesikia chama cha Walimu kimepinga vikali. Mimi nadhani kuna mambo tunachanganya. Tuna haja ya kuwa na chombo maalum cha kusimamia taaluma ya ualimu. Nikimanisha Bodi ya Ualimu.
Hii imekuwa danadana muda mrefu na siasa zimeingia na hata walimu walio wengi wanapinga kwa kigenzo cha eti kutakuwa na kulipia ada ya bodi. Wenzetu madaktari wanalipia ada ya bodi wenzetu manesi na mafamasia wanalipia ada ya bodi na kupewa lesseni. Hii leseni itasaidia kuleta ubora wa kazi na ndipo leseni zitafanya kazi. Na hakutakuwa na ubabaishaji wa kiendesha mambo kufuata siasa.
Sasa kuna hili la kusema walimu watakao ajiliwa (ajira mpya) kufanya mtihani. Hapo ndipo ubabaishaji mkubwa na siasa zinataka kuchukua mkondo wake. Huo mtihani utatoka wapi?
Huo mtihani utatungwa na nani?
Huo mtahani utapima nini?
Huo mtihani nani atagharimia?
Una walimu wa masomo tofauti tofauti. Unaposema wanafanya mtihani una manisha utakuwa na mtihani kila somo kila mwalimu?
Vyuo ndivyo vyenye mamlaka ya ku-train walimu na kujiridhisha pasipo shaka walimu wameiva na vyuo vimeenda mbali zaidi zimewapa mitihani wakafaulu na hata waliofeli wakarudia mpaka wafaulu.
Leo hii wanataka kuajiliwa wanaambiwa wafanye mtihani. Hapo kuna shida. Ina maana vyuo ndivyo vyenye ubovu mpaka kuto aminika na waajiri wanataka kuwapa wafanye mtihani.
Leo ukija na hoja ya kuwa walimu wafanye mtihani wanapo ajiliwa kwa kigezo eti hawana uwezo hapo haupo sahihi. Hata kama walikuwa na ufaulu mdogo wakasoma ualimu. Je unapowafanyisha mtihani ufaulu mdogo waliokuwa nao utakuwa umepanda?
Kuna awamu kadhaa Serikali ilisha kuwa na uhaba mkubwa wa walimu wakaazisha program za walimu wa Voda Fasta, mara certificate walimu wasome mwaka mmoja. Mara degree walimu wasome miaka mitatu badala ya minne. Mara kuna uhaba wa walimu wa Sayansi hivyo program maalum zikaanzishwa ili kusaidia upungufu.
SASA LEO
Baada ya kuonekana kuna kasoro nyingi kwenye elimu eti walimu wanaoanza ajira mpya wafanye paper
USHAURI WANGU
1. Mpaka sasa bado haijaeleweka kama kuwafanyisha paper walimu wa ajira mpya kutaongeza ubora wa elimu Labda hoja iwe wahitimu wa ualimu ni wengi mtaani kwa hiyo kuwapunguza ni kuwafanyisha mtihani.
Angalizo je ikitokea kuna uhaba tena hapo badaye tutafanyaje? Tutafuta mitihani?
2. Kama kiwango cha elimu kimeshuka ili kukipandisha kuna mambo mengi ya kufanya. Mojawapo ni kuanzisha chombo maalum cha kusimamia taaluma ya ualimu. YAANI BODI YA UALIMU. NA walimu watakuwa up todate. Watafanya mitihani ya bodi na watakuwa na leseni.
Nje ya hapo tunajidanganya ndiyo maana chama cha walimu CWT kimekuja juu kupinga hilo. Tusitegemee kufanya paper kwa walimu wa ajira mpya kutaondoa matatizo tuliyonayo sisi walimu yaani matatizo ya kitaaluma.
Asante.
Comments za kujenga tafadhari
By: Mwl Ndangalasi.
Fb: Mtoto wa mkulima.