SENGEREMA: Afisa TAKUKURU amlamba mwalimu makofi

SENGEREMA: Afisa TAKUKURU amlamba mwalimu makofi

Wafanyakazi wote wa Umma situliambiwa ni wana ccm, wacha wauane.
 
Taarifa zilizonifikia ni kwamba;

Kama kichwa kinavyo jieleza tukio limetokea leo Halmashauri ya Wilaya ya BUCHOSA wilaya ya SENGEREMA MKOA WA MWANZA ambapo Afisa mmoja wa TAKUKURU amemlamba makofi mwalimu wa kike (jina linaifadhiwa) wa shule ya msingi (jina linahifadhiwa) wakati wa uhakiki wa vyeti kwa watumishi wote wa umma wa Halmashauri hiyo kwa kosa la kusimama nyuma yake wakati zoezi likiendelea.

Afisa huyo anashikiliwa na polisi mpaka sasa, kwenye kituo cha polisi cha KATA YA NYEHUNGE ambapo zoezi hilo linafanyika, wakati mwalimu akiwa hospitali kwa matibabu ya michubuko aliyoyapata.

Hii ni mwendelezo wa vichapo na udhalilishaji kwa waalimu ambao wanaonekana kutokuwa nathamani mbele ya kada zingine za kiutumishi.

Mpaka sasa suala hilo lipo mikononi mwa polisi, wizara usika na vyombo vyenye dhamana mtende haki kulinda heshma ya mwalimu.
hii issue imeishaje!!
 
Tupe update
mrejesho:::

wapendwa wangu taarifa nilizo nazo mpaka sasa ni kwamba...

mhusika alijidhamini siku hiyo hiyo majira ya saa 5 usiku hivyo yuko nje kwa dahamana!!!!

kesi yake imehamishiwa kituo kikubwa cha polisi SENGEREMA kutoka kituo kidogo cha polisi NYEHUNGE!!!

CWT sengerema wamemtaka mkurugenzi halmashauri ya buchosa kumchukulia hatua za kinidhamu afisa takukuru aliyefanya tukio hilo!!! ni baada ya kufika halmashauri ya buchosa kuonana na mkurugenzi siku ya jumamosi ya tarehe 10/09/2016 siku moja baaada ya tukio!!!! ambapo walipata nafasi yakuonana na muathirika watukio hilo pia!!!

mpka sasa mheshimiwa wa takukuru ajafikishwa mahakamani, na hakuna taarifarasmi kuwa atafikishwa lini mahakamani!!!! labda kwakuwa tukio lilitokea weekend na leo jumatatu ni siku kuu!!!

cc Ta kamugisha na Zamaulid
 
mie naunga mkono walimu wasiojielewa waendelee kunyukwa makofi. Mwalimu aliyesoma philosophy hawez kunyukwa vibao akawa anashangaa tu. Huwezi kuwafundisha watu namna ya kudai wakati wew mwenyew huwez
 
[emoji109] [emoji109] [emoji109] hata mimi
 
Avogadro, kwa maelezo yako ni kwamba involuntary ingeweza kumtokea ticha kumtanfika mtaakukuru. Ni
 
It means hakukuwa na hata walimu wa kiume wa kuweza kumthibiti huyo anayepiga mwenzake?

Hii kada isipochukuliwa serious tutashtuka Kenya wametuacha mbali sana. Coz walimu Kenya wakikohoa tu nchi inasimama kwanza.
 
Jiulize;
Alikuwa anachungulia nini nyuma ya huyo mzabua makofi?? Alimfanyaje hadi hasira ikawaka?? Kofi tu mtu afike hospitali. Sawa, kwa sababu ana bima ndo maana anajirusha hivyo, ingelikuwa malipo kwanza, asingeenda huko.
 
Hapo hakuna kesi wala nini huyo mwalimu kunakosa alfanya kubwa. Jamaa si kicha kumpiga tu.Pia sijaelewa kwamba mkurugenz wa halmashauri ndio amchukulie hatua jamaa,swali siku hizi maafisa watakukuru wapo chini ya halmaahauri?
 
Sasa alisimama nyuma yake kwanini? Wanawake bila kupiga viganja vichache akili haziji kabisa
Hivi wewe umezaliwa na mwanamke kweli? Huna hata heshima kwa mama yako mzazi. Tena wewe ni mshamba uliekosa exposure kabisa. Unawezaje kusema wanawake badala ya kusema baadhi ya wanawake?huu u - primitive wako unapiga honi kabisa. Karne ya 21 bado unazungumzia kumpiga mwanamke! Pole weee, naona dunia imekutupa kweli kweli. Stop being so ignorant, have a life!!!.
 
sioni kama kulikuwa na sababu ya kumpiga huyo mwalimu, na hii yote ni ubabe walionao hao jamaa wanaojiita takukuru angekuwa ni kamanda wa zamu (jw) angethubutu kumpiga, hebu tubadilike tusiishi kwa kudharauliana.
 
Back
Top Bottom