Selfika na JF: Snap it. Show it

Nionapo amani kama shwari,
Ama nionapo shida;
Kwa mambo yote umenijulisha,
Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.

Ingawa Shetani atanitesa,
Nitajipa moyo kwani;
Kristo ameona unyonge wangu,
Amekufa kwa roho yangu.

Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.

Dhambi zangu zote, wala si nusu,
Zimewekwa Msalabani;
Wala sichukui laana yake,
Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.

Ee Bwana himiza siku ya kuja,
Panda itakapolia;
Utakaposhuka sitaogopa,
Ni salama rohoni mwangu.

Salama, Salama,
Rohoni, Rohoni,
Ni salama rohoni mwangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…