Selfika na JF: Snap it. Show it



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dona nimewahi kula sana kijijini na mlenda, bahati nzuri kuanzia mwaka 2000 February sijawahi kula tena hadi leo, na sijalimiss 🀣🀣🀣🀣🀣


Sent from my iPhone using JamiiForums
Kijijini mahindi mnalima wenyewe. Hili Dona letu mahindi hujui yamekaa muda gani kwenye ghala au yamewekwa dawa gani
 
Kijijini mahindi mnalima wenyewe. Hili Dona letu mahindi hujui yamekaa muda gani kwenye ghala au yamewekwa dawa gani
Mimi Kijiji nilichozaliwa ilikuwa hakuna Dona Wala sembe.
Iliaminika kwamba mtu anayesaga Dona Ni yule ambaye Ana njaa na ameishiwa mahindi,katika kubana matumizi anajitahidi anasaga Dona..
Ugali wa Dona haumalizi Sana unga.
Na ndivyo ilivyokuwa.

Mahindi yakikobolewa na kupelekwa nyumbani,yanalowekwa Kwenye maji hata siku 2 Hadi 3,yanaoshwa yanaanikwa halafu yanasagwa.
Unga ukitoka mashineni unaanikwa Tena ,unachekechwa tayari kwa matumizi.
Huu unga Ni mweupe Sana na ugali wake mlaini ila unga unaisha haraka Sana.
Safari za mashineni haziishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…