Njoo nikuhadithie
Dr Lizzy kuhusu kima (nyama ya kusaga.
Ndio nimefika fika enzi hizo Kaskazini π
Mgeni mgeni mitaa siijui, kwanza navyoongea tu najulikana nimevamia mkoa.
Kuna sehemu Town- around CCM mkoa walikuwa wanauza chapati nzuri, basi naagiza kwa kumtuma mtu.
Sasa huyo mtu siku akaniambia jaribu kula chapati-kima, utaifurahia.
Kichwani mie si akaja kima kama kima mnyama. ππ
Nikamuuliza kima ndio manini hayo? Kima analiwa? Nyie watu wa huku mkoje ππ
Akanambia we jaribu, ikiwa mbaya nitalipia.
Deal ikawa β
Woi mzigo si unakuja ni kima nyama ya kusaga? Nikashtuka ππ ndio kuniambia kima ni nyama iliyosagwa.
Sasa sielewi ni jina la huku tu au? Dar, Dom & Moro sijawahi lisikia