Sehemu nzuri ya kuishi Tanzania

Sehemu nzuri ya kuishi Tanzania

Kama unafanya kazi full time online ina maanisha wewe ni freelancer..

Ningekushauri pia uangalie sehemu ambayo ina tech eco system kubwa ambayo inaweza kukupa fursa za kuuza huduma kwa private companies lakini pia kufanya networking haswa kwa tech events

1.Dar
Fursa za tech ndo zilipo na Unaweza kujichimbia maeneo ya nje ya mji kama kibamba hukoo

2. Mwanza
Hili ni jiji lenye vigezo vyote unavyotaka

3.Arusha, huwa naona kama tech industry ni kubwa pia lakini kuhusu unafuu wa maisha, sijui

Kama ukitaka hiyo lazy life, mikoa mingi ukienda wilayani panakuwa na nafuu zaidi
 
Kwema wakuu!

Mimi ni kijana wa miaka 24 na kazi zangu ni full-time online. Nataka nikimbie nyumbani.

Kwa 2.5M kama pesa ya kuanzia maisha, Je! Ni mkoa/wilaya gani Tanzania nzuri kwa kuishi yenye sifa zifuatazo

  • Unafuu wa maisha
  • Huduma ya maji ya kuaminika*
  • Huduma ya umeme
  • Network nzuri *, 4G imara ( kazi zangu zinategemea mtandao )
  • Urahisi wa kupangisha (room single masters zichezee 50k - 70k)
  • Hali ya hewa safi

Nitashukuru kwa michango yenu yote. Ukiweka jina la mkoa tafadhali taja na wilaya.
Mimi ni mtu wa Mbeya,,ila nipo Njombe kwa sasa , achana na mambo ya Online njoo Njombe tukusanye maharage na mkaa hakika utafurahi ,, maisha yako poa kabisa hiki si kipindi cha baridi .Nafaka ndio hela ilipo kwa sasa...
 
Tanzania nzima Lushoto ni the best
Mkuu dadavua kuhusu Lushoto.... Nimepitia pia uzi nyingi za nyuma na sehemu zinazotajwa sana ni:
1. Mbeya
2. Mwanza
3. Tanga (Lushoto)
4. Moro

Ila sijabahatika kupata maelezo kuihusu Lushoto, unaweza ukaielezea kuhusu:
---> sehem nzuri za kukakaa ndani ya Lushoto
---> Gharama za maisha hasa bei ya vyumba na chakula
---> Huduma za kijamii kama maji na uneme je ni vya uhakika?
 
Njoo mafinga:
-Ni mji unaokuwa kwa kasi kuliko mkoa wenyewe kwa maana ya iringa urban.
-Hali ya hewa ni safi,baridi,jua hata likiwaka huhisi joto.
-Network ni 4G.
-Maji tunatumia ya visima(underground water) pamoja na ya bomba.
-Umeme ni uhakika kwasababu ya uwepo wa viwanda vingi kwahyo Tanesco wameliziingatia hilo.
-Vyumba self container ni kuanzia 40k mpaka 60k.
-Biashara zipo nyingi sana utachagua tu ukifika.
-Vyakula ni bei rahisi kabisa na ni vya kila aina.
-Ni mji ambao umeunganishwa na mikoa yote ya kusini,Morogoro upande wa kaskazini mwa wilaya(Mufindii) kuelekea kihansi,mlimba mpaka mahenge aua ifakara.
-Kufika dodoma au kwenda Dar es salaam ni muda wowote.
 
Njoo mafinga:
-Ni mji unaokuwa kwa kasi kuliko mkoa wenyewe kwa maana ya iringa urban.
-Hali ya hewa ni safi,baridi,jua hata likiwaka huhisi joto.
-Network ni 4G.
-Maji tunatumia ya visima(underground water) pamoja na ya bomba.
-Umeme ni uhakika kwasababu ya uwepo wa viwanda vingi kwahyo Tanesco wameliziingatia hilo.
-Vyumba self container ni kuanzia 40k mpaka 60k.
-Biashara zipo nyingi sana utachagua tu ukifika.
-Vyakula ni bei rahisi kabisa na ni vya kila aina.
-Ni mji ambao umeunganishwa na mikoa yote ya kusini,Morogoro upande wa kaskazini mwa wilaya(Mufindii) kuelekea kihansi,mlimba mpaka mahenge aua ifakara.
-Kufika dodoma au kwenda Dar es salaam ni muda wowote.
Shukrani sana kaka umepaelezea vizuri. Vipi kuhusu hali ya hewa ya Mafinga, huko nako si naskia baridi lake ni kali sana.
 
Shukrani sana kaka umepaelezea vizuri. Vipi kuhusu hali ya hewa ya Mafinga, huko nako si naskia baridi lake ni kali sana.
Yesss barid lipo lakini linazoeleka na pamoja na kwamba ni la muda wote(miezi yote ya mwaka) ila linvumilika
 
Back
Top Bottom