Scientific fact na knowledge Thread

Scientific fact na knowledge Thread

dosho12

JF-Expert Member
Joined
May 6, 2023
Posts
4,228
Reaction score
11,628
‎hii itakuwa thread ya kupost na kujifunza vitu mbali mbali kuhusu sayansi na saikolojia kuhusu mwadamu, viumbe wengine, dunia na ulimwengu kwa ujumla, hivyo kama una fact, qoutes au chochote cha kujifunza unaweza kuweka
 
‎Kuna cell kwenye ubongo wa mwanadamu ambayo haipatikani kwenye kiumbe chochote kile, Neuron ya tofauti kabisa ambayo wanasayansi wameipa jina la Rosehip sababu inataka kufanana sana na kama mmea kuliko kama cell, mwaka 2020 wanasayansi kutoka taasisi ya Allen na chuo kikuu cha Szeged walikuwa wakichunguza tissue za kwenye ubongo wa mwanadamu kwa lengo la kulinganisha au kuangalia utofauti uliopo kwenye ubongo wa mwanadamu na wa panya hapo ndipo walipo ona hiyo cell yenye umbo la tofauti na inaonekana kuwepo kwa mwanadamu tu walifanya majaribio yakutosha kuona kama hiyo cell huenda ikawepo kwenye viumbe wengine ila hawakuona, kitu kinachowashangaza wachunguzi ni kuwa neuron hiyo ipo kwenye layer ya juu kabisa kwenye ubongo sehemu ambapo mawazo,hisia na ufahamu unapo anza kujitengeneza na kama vile zimekaa kwenye mlango wa ufahamu kuangalia nini inachoingia, zinalinda kitu, control kitu au kuzui kitu haijuikani mpaka sasa sababu wanasayansi mpaka sasa hawajui hasa hizo cell ni nini na zinafanya nini
 
‎Unapozuia pumzi yake kwa sekunde 40 utaanza kuhisi ile presha ya kutaka kupumua na karibu wengi hudhani ni sababu unaishia oxygen mwiini ila sio bali ile presha unayohisi ni presha inayotoka kwenye sensor iliyopo kwenye brainstem yako inayokumbusha mwili kutoa hewa chafu kwenye mwili wako { CO2 } carbondioxide inajaa kwenye damu na kuanza kuwa acidic hivyo husababisha alamu ya kuitoa kwenye mwili hata kama bado kuna hewa ya oxygen mwilini, wazamiaji wa kwenye maji wanapewa mafunzo ya kuivumilia hiyo alamu kwenye ubongo kwa dakika kadhaa, ila ubaya unakuja pale unapovumilia zaidi na hewa kweli inaisha mwilini na hapo kinachofata ni kuzima ghafla na ndio maana wanashauriwa wasizamie peke yao
 
Kwa nini ukikaa kimya sana unaanza kusikia mapigo ya moyo wako?

Wengi hudhani kwamba mapigo ya moyo huanza kusikika pale yanapokuwa “makubwa” au yanapoongezeka, lakini kisayansi sivyo.
Mapigo ya moyo na sauti za ndani ya mwili wako zipo muda wote, lakini huzisikii kwa sababu ubongo wako una mfumo wa kuchuja sauti (sensory filtering). Mfumo huu hufanya kazi kama kifaa cha kuzuia kelele zisizo muhimu, ili ubongo usizidiwe na taarifa nyingi kwa wakati mmoja.
Kwa mfano, kila sekunde ubongo hupokea mamilioni ya taarifa sauti, harufu, mwanga, mguso, lakini huchagua ni zipi muhimu na zipi zipuuzwe. Sauti za ndani ya mwili kama mapigo ya moyo, pumzi, na mtiririko wa damu mara nyingi huwekwa kwenye kundi la kelele za kawaida (background noise).

Sasa unapoingia kwenye mazingira ya kimya sana, hakuna tena kelele za nje za kushindana na hizo sauti za ndani. Hapo ndipo ubongo unapoongeza umakini wake kiotomatiki, na zile sauti ndogo ndogo ambazo zilikuwa zikipuuzwa huanza kuingia kwenye ufahamu wako.
Ndiyo maana unaanza kusikia:

Thump ya moyo wako.
Pumzi yako.

Hata mtiririko wa damu kwenye masikio.

Lakini ukweli ni kwamba hazijaanza upya zilikuwepo muda wote. Kilichobadilika ni kile unachoruhusu ubongo wako kukisikia.
Hii inaonyesha jambo la kushangaza zaidi:

Si kila kitu unachokiona au kusikia ni dunia yenyewe… bali ni dunia iliyochujwa na ubongo wako.
 
Jambo la kushangaza kuhusu macho yako na jinsi unavyoiona dunia.

Kila kitu unachokiona duniani kinapitia macho yako, lakini kuna jambo moja la kushangaza sana, huwezi kujiona moja kwa moja kwa macho yako bila kutumia kioo au kamera.

Kwa nini?
Macho yako hufanya kazi kama kamera
Mwanga unaingia ndani ya jicho
Unagonga retina
Ubongo hutafsiri kile kilichoonekana kuwa picha
Lakini ili ujione wewe mwenyewe moja kwa moja, macho yako yangelazimika kujigeuza na kujitazama yenyewe , jambo ambalo haliwezekani kimaumbile.

Lakini hapa ndipo jambo linapozidi kushangaza zaidi
Ubongo wako hauoni dunia kama ilivyo moja kwa moja.
Kile unachokiona ni tafsiri ya ubongo wako ya mwanga unaoingia machoni.

Hii ina maana:
Rangi unazoziona si rangi halisi, bali tafsiri ya ubongo.
Umbali unaouona ni makadirio ya akili yako.
Hata mwili wako unaouona ni ,picha iliyojengwa ndani ya ubongo.

Hitimisho
Kwa namna ya kushangaza.
Wewe hauoni dunia moja kwa moja… unaona toleo la dunia lililotengenezwa na ubongo wako.
Na ndiyo maana:
Watu wawili wanaweza kuona kitu kimoja lakini wakakielewa tofauti
Au mtu mmoja akaona kitu kipo, mwingine asione kabisa.
 
Jambo la kushangaza kuhusu Universe ambalo watu wengi hawalijui.

Unachokiona kama anga la usiku lenye nyota si picha ya sasa ya ulimwengu.
Kila nuru unayoiona kutoka angani imechukua muda mrefu sana kusafiri mpaka ifike machoni pako.

Kwa mfano:
Mwanga wa Jua unafika duniani baada ya takribani dakika 8
Nyota zilizo karibu zinaweza kuchukua miaka mingi kufika kwetu
Nyota zilizo mbali zaidi zinaweza kuonekana kama zilivyokuwa miaka milioni au mabilioni iliyopita.

Hii ina maana gani?
Kila unapotazama anga la usiku, huoni universe ya sasa unaona universe ya zamani.

Jambo la kushangaza zaidi
Inawezekana kabisa kwamba:
Nyota unayoiona usiku huenda tayari imezimika.
Lakini mwanga wake bado unasafiri kuelekea duniani na ndiyo unaoufanya uione.

NB
Anga unaloona si sasa ya universe… ni historia yake inayosafiri kufika kwako.
 
Jambo la kushangaza kuhusu Universe ambalo watu wengi hawalijui.

Unachokiona kama anga la usiku lenye nyota si picha ya sasa ya ulimwengu.
Kila nuru unayoiona kutoka angani imechukua muda mrefu sana kusafiri mpaka ifike machoni pako.

Kwa mfano:
Mwanga wa Jua unafika duniani baada ya takribani dakika 8
Nyota zilizo karibu zinaweza kuchukua miaka mingi kufika kwetu
Nyota zilizo mbali zaidi zinaweza kuonekana kama zilivyokuwa miaka milioni au mabilioni iliyopita.

Hii ina maana gani?
Kila unapotazama anga la usiku, huoni universe ya sasa unaona universe ya zamani.

Jambo la kushangaza zaidi
Inawezekana kabisa kwamba:
Nyota unayoiona usiku huenda tayari imezimika.
Lakini mwanga wake bado unasafiri kuelekea duniani na ndiyo unaoufanya uione.

NB
Anga unaloona si sasa ya universe… ni historia yake inayosafiri kufika kwako.
Inshort hata sisi ni historia katika galaxy nyingine wanaona picha ambalo lishachezwa.
 
Jambo la kushangaza kuhusu Universe ambalo watu wengi hawalijui.

Unachokiona kama anga la usiku lenye nyota si picha ya sasa ya ulimwengu.
Kila nuru unayoiona kutoka angani imechukua muda mrefu sana kusafiri mpaka ifike machoni pako.

Kwa mfano:
Mwanga wa Jua unafika duniani baada ya takribani dakika 8
Nyota zilizo karibu zinaweza kuchukua miaka mingi kufika kwetu
Nyota zilizo mbali zaidi zinaweza kuonekana kama zilivyokuwa miaka milioni au mabilioni iliyopita.

Hii ina maana gani?
Kila unapotazama anga la usiku, huoni universe ya sasa unaona universe ya zamani.

Jambo la kushangaza zaidi
Inawezekana kabisa kwamba:
Nyota unayoiona usiku huenda tayari imezimika.
Lakini mwanga wake bado unasafiri kuelekea duniani na ndiyo unaoufanya uione.

NB
Anga unaloona si sasa ya universe… ni historia yake inayosafiri kufika kwako.
Ulisha wahi kuchek movie ya interstellar
 
Back
Top Bottom