Saudia yaifungia Al Jazeera ya Qatar

Saudia yaifungia Al Jazeera ya Qatar

Adui
Kidudu mtu kaingia., Lakini lakushangaza kwanini nchi za kiislamu zinakubali kirahisi kushawishiwa na Western? Marekani alitaka kuwafarakanisha China na Korea Kaskazini, pia Japan na Korea kaskazini akagonga mwamba sasa ameona aje atikise dola za kiislamu.
Adui mkubwa wa waraabu na waislam ni ufalme wa saudi arabia
 
Qatar wakiona ovyo wanaweza kuamua tena kuhamishia makao makuu ya nchi yao Zanzibar kama alivyo fanya babu yao! Hakuna atayewabugudhi binamu yao yupo kule!
 
7488a586004b0a9c5732734d3c83af9d.jpg



23d6712e3264beb7869cade2a36b8aff.jpg
 
Hao Saudia, Libya, Egypt na Bahrain ndiyo wanafiki, email zilizovuja zinaonyesha mikakati yao yakutaka kuifanya Qatar ionekane ina fadhili magaidi mbele ya Marekani
Wanataka US aamishie base yake UAE ya jeshi la anga
 
Kaka
Bifi baina ya Qatar na Saudia ni ya kimaslahi/influence na inaogopa sana ukoo wa kifalme kupinduliwa kwa kupitia mbinu za colour revolution, utawala wa Kifalme hawajiamini hata kidogo - katika mbinu zake za kutaka kujihami linataka ndiyo liwe Taifa linao wika Mashariki ya kati i.e a mimi Super Power - watumie uwezo wao kijeshi kuwatishia Waarabu wenzake na raia wa Saudia ili wasifurukute, vile vile Saudia inatumia vibaya utajiri wake kuendeleza siasa zake Mashariki ya kati zenye lengo la kutaka kuvuruga amani kwenye Nchi washindani wao notably IRAN na Syria kwa support ma rebels kwa kuwapatia silaha na fedha. Binafsi siamini kama Trump anahusika katika ku-influence mifarakano ya Saudia na Qatar we sema labda Saudia ilitumia ujio wa Trump nchini mwao kuikandia Qatar kwamba ina support Ugaidi wakati kila mtu mwenye akili timamu anajua Sadia ndiye kinara wa kuvurunga nchi za watu hasa Sysria na Iran.

Narudia kusisitiza kwamba Saudia ina wasi wasi na IRAN, Syria na sasa Qatar, kwa akili zao wanafikiri nchi hizo tatu zinaweza kuwapa mafunzo na ku-finance waasi wa kupidua utawala wa Kifalme, ndiyo maana kwa kupitia ushawishi wake wa kifedha inajaribu sana ku-influence mataifa mengine ya Kiarabu yamtenge Qatar na wao wanakubali bila ya kutafakari undani wa tatizo, mwishowe anaweza kuwashawishi waungane kuishambulia Qatar kijeshi kwa madai kwamba wanafunga ugaidi - Saudia hawataki kuchukua jukumu hilo peke yao baada ya enyeshwa na waasi wa Yemeni, huu sijui mwaka wangapi tangu wavamie Yemen pamoja na Saudia kuwa na silaha nyingi za kisasa bado wameshindwa kutimiza malengo yao huko Yemen, wanajua wakijiingiza Qatar mambo yanaweza kuwa mabaya zaidi ni afadhali wajaribu kuwashurutisha Waarabu wenzao ili washirikiane nao kijeshi/uvamizi just in case.
Kaka umeongea point saana , hila nafikiri raia wa saudia ni wajinga saana , kwa nn utawala wa kifalme wa saudi usiondolewe ?
 
Qatar wakiona ovyo wanaweza kuamua tena kuhamishia makao makuu ya nchi yao Zanzibar kama alivyo fanya babu yao! Hakuna atayewabugudhi binamu yao yupo kule!
Wabongo nafasi ya kuuza ng'ombe Qatar hiyo, wafugaji mjipange
 
Qatar ni ndogo sawa, Qatar ana mkataba na turkey kwa ajili ya ulinzi , mbona saudi wanaipa funds IS , hatusikii kelele ,Qatar wanapenda na kuunga mkono haki popote pale , hao wengine ni wanafiki tu
unajuwa mimi sisemi kuwa Saudia ndio wasafi wana matatizo yao makubwa tu ila lazima ujuwe Turkey na Saudia ni washirika wakubwa hawezi kuingia katika matatizo na Saudia. ila leo nili comment hii ni green light toka kwa Trump baada ya ziara na kusign bid deal na KSA. muda mfupi Trump ame tweet kuwa kila mtu alikuwa ananyosha kidole kwa Qatar na nategemea huu ndio utakuwa mwisho wa ujangili. hii ni statement kubwa ya Trump ndio ujue Qatar anawekwa kati ila ni ukweli Qatar ni sponser mkubwa wa Hezobolla, Hamas na Brotherhood. leo katoa speech kidogo Mfalme wa Qatar ila akakata speech kwa kuombwa na Kuwait ila kaomba waongee yaishe. kwa ufupi Saudi wabaya sana tu ila Qatar ni fitna zote ni yeye ila wakati wake umefika na Trump kasema leo.
 
Mkipita na kwa usafiri wa Ndege mnajifanya mmeishi acha kudanganya Qatar in tishio sana Emirates kaona anazidiwa kete na Qatar air, Saudia kaona mdororo wa mafuta umeumiza sana uwekezaji Qatar anasoko LA uhakika uzuri Qatar siyo land locked nation
 
Hebu acha utani, Saudi Arabia ni super power kiuchumi wakifuatiwa na UAE katika Gulf, Qatar ni nchi ndogo sana kama mji mmoja tu wa Saudia. Lazima ujuwe land border wanategemea wa Saudia na UAE na hii imefungwa. Qatar ni fund mkubwa wa Hezbollah na muslim brotherhood. ziara ya Trump juzi ni big deal na price ni kuget rid ya mfalme wa Qatar na hili lina green light ya USA na utaniambia siku chache utasikia mfalme out na things back to normal. Qatar ni tatizo kubwa ki nchi hata Dar kubwa basi fujo tu ila wakati wao umefika. na kukumbusha tu Qatar ina history ya kufukuzana katika ufalme Baba yao alipindulia na mtoto wake na huyu alimtoa baba yake na hii ni zamu yake. mark my world.
USA wanataka gesi ya Qatar hawana jipya hao Saudia wanaingizwa kwenye ugomvi kipuuzi na watajutia
 
kukosa coverage ya matangazo maana yake ni kukosa eneo la propaganda.........
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Unajua kwamba Qatar ndio nchi ya kwanza duniani kwa kuwa na GDP kubwa.?
Ni per capital gdp na sio nominal.jifunzi kujua izo gdp.ni sawa na norway inaizid ujeruman kwa per caputal lakin nominal ujeruman ipo juu
 
  • Thanks
Reactions: SDG
unajuwa mimi sisemi kuwa Saudia ndio wasafi wana matatizo yao makubwa tu ila lazima ujuwe Turkey na Saudia ni washirika wakubwa hawezi kuingia katika matatizo na Saudia. ila leo nili comment hii ni green light toka kwa Trump baada ya ziara na kusign bid deal na KSA. muda mfupi Trump ame tweet kuwa kila mtu alikuwa ananyosha kidole kwa Qatar na nategemea huu ndio utakuwa mwisho wa ujangili. hii ni statement kubwa ya Trump ndio ujue Qatar anawekwa kati ila ni ukweli Qatar ni sponser mkubwa wa Hezobolla, Hamas na Brotherhood. leo katoa speech kidogo Mfalme wa Qatar ila akakata speech kwa kuombwa na Kuwait ila kaomba waongee yaishe. kwa ufupi Saudi wabaya sana tu ila Qatar ni fitna zote ni yeye ila wakati wake umefika na Trump kasema leo.
Sasa Qatar hao uliowataja anaowasponsor hakuna hata gaidi hapo , wote ni freedom and democracy fighters, Hamas wameshinda uchaguzi Palestine, Muslims brotherhood wameshinda Egypt , sasa WW utasemaje magaidi ? Kinachoendelea sasa wale waovu wakiongozwa Na Saudi wanampa Qatar jina baya hili kujustify uhovu wao , Saudi wants to dictate Qatar, Qatar can't accept that despite being both sunnis of salafi version,Saudi anaona wivu Qatar inakuwa maarufu Na kufanikiwa kwenye eneo hilo
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Back
Top Bottom