Sartanic Verses au Aya za shetani ni kitabu cha Fasihi Simulizi ambacho kimetungwa kwa kuzingatia uhalisia maisha na matukio lakini kwa kumtumia mtume Muhammad na maisha yake.
Kitabu hichi kilitoka mwaka 1988 na TATIZO kubwa ni matumizi ya lugha ya kashfa inayokufuru dini ya kiislam na ambayo mwandishi Salman Rushdie aeleza kuwa ni chanzo cha ghasia, mauaji na misimamo mikali (Islamic fundamentalism).
Moja ya sifa kuu ya mwandishi wa Fasihi SImulizi ni uwezo wa matumizi ya lugha, upangaji wa wahusika aktika simulizi hiyo , mazingira, hisia na hali. Hivyo Rushdie atumia lugha inoonekana (kwa wasomaji wa kijujuu) kama ya mzaha hivi na ndo hapo aonekana ametumia lugha ya kashfa.
Kitabu hichi kilipotoka tu waislamu duniani walilaani na hata kufikia kutishia maisha ya Rushdie na wale wote walokwa wakisaidiana nae kutayarisha kitabu hichi na hata kufikia kupigwa marufuku kuingizwa nchini India.
Mwaka mmoja baadae yaani 1989 kiongozi wa Iran Ruhollah Khomeini ndie alieamuru Salman Rushdie auawe popote alipo agizo liloitwa Fatwa ambalo lilisababisha majaribio kadha wa kadha ya kuondoa uhai wa mwandishi huyo.
Katika simulkizi ya kitabu hichi Rushdie amewatumia wahusika wawili wakuu mwanamme aitwae Gibreel na mkewe aitwae Saladin.
Sasa, katika vitabu vya kiislam hususan Quran Gibreel ni malaika mkuu ambae yu karibu na mtume Muhammad, hivyo huwezi kumfananisha au kuhusisha na matukio ambayo hayamo katika misingi ya dini ya kiislam.
Kwa mfano Saladin amfanananisha Gibreel na shetani kwamba amesababisha uokovu kutoka katika anguko la ndege walokuwa wakisafiria pale ilipotekwa nyara ikiwa angani na kuanguka lakini wao wawili kupona.
Saladin nae akakamatwa na askari wa uhamiaji ambao walinyanyasa kijinsia na kipelekea yeye kupata ukichaa. Hali hiyo ni tofauti kabisa na hali halisi kwamba Gibreel alikuwa ameoa mke.
Kosa jingine ni kumbadilisha jina Mtume Muhammad na kumwita Mahound au mjumbe na kuwa ana wapinzani wawili Hind na Baal na pia kuhusisha mtume Muhammad na danguro ambalo pia humo wamo wanawake malaya ambao watumia majina ya wake za mtume.
Na kosa la tatu linopigila msumari kwenye jeneza ni pale Salman Rushdie katika kitabu chake anapomtumia Ayesha mwanamke wa kihidhi ambae hudai kuwa apewa maono ya malaika Gibreel na kisha kwenda kuaambia wanakijiji wote waende Mecca kuhiji lakini kwa kutembea juu ya bahari ya Arabia kitendo kilichopelekea wanakijiji wote kuingia baharini na kupotea.
Hiuo ndo mwongozo wa makosa yanosemwa ya mwandishi Salman Rushdie na kitabu chake cha Aya za Shetani.