Sasa naanza kuwaelewa walioajiriwa

Sasa naanza kuwaelewa walioajiriwa

Mwisho wako ndio mwanzo wetu.

Pole mkuu.
 
Baada ya kushauriwa na wana kwamba ukitaka kufanikiwa jiajiri.

Basi nikaacha kazi nikauza nyumba kuanza kuwekeza kwenye biashara.

Kilichofuata. Tusidanganyane ngoja niendelee kutumwa maisha yenyewe haya haya.

Nb sio kila binadamu kazaliwa kuwa tajiri wengine tumeubwa kutumwa using'ang'anize mambo
Utajipotezea muda.
Mkuu,njoo tuuze zambarau na matikiti maji.Tutatusua.
 
Usisikilize manano ya watu

Binaadamu tuna tofautiana katika uwezo wa kutatua changamoto zetu

So huwenda uwezo ulionao sio wakutatua changamoto za Kijiajiri

Kujiajiri Kuna taka uwe smart sana + uwe na Uwezo mkubwa sana wa kuhimili changamoto
Sawa mkuu nikizeeka najiajir huu ujana na pindi mtaji shwaa
 
Kuajiriwa raha yake iko tarehe 25 tu ama wakati unasign perdiem. Tofauti na hapo tunajikaza sana..🤣
😂😂😂 Wakujiajiri Watuache 🤸🤸
 
Ulishauliwa ujiajili na sio kuacha kazi na kuuza nyumba
 
Mlikua mnavuta ,ushauri ukakuzidia??
😂😂
Kwahiyo mkuu mpaka unauza nyumba, bado bangi ilikua stim haijakata kichwani!!!
Mkuu wewe acha tu kuna wana wakivuta wanamadini mbona unaweza kuona inachelewa kutoboa kimaisha ila ulisha zama kwisha habari
 
Tatizo lako hujaweka kisa kamili ili tujue umekosea wapi?

Ila kosa lako la kwanza kabisa uliweka mayai yote kwenye tenga moja,biashara lazima iwe na hela zingine pembeni ili kuisupport inapohitajika,

Kingine,Biashara huwezi ukaianza leo na kupata faida leo leo,biashara inahitaji time na kujitoa,

Wafanya biashara wengi tu walipata hasara mwanzoni ila hawakurudi nyuma bali walitafiti chanzo cha hasara kisha wakarekebisha,biashara inahitaji uvumilivu,

Mwisho kabisa,sio kila mtu anaweza kua mfanya biashara.
 
Tatizo lako hujaweka kisa kamili ili tujue umekosea wapi?

Ila kosa lako la kwanza kabisa uliweka mayai yote kwenye tenga moja,biashara lazima iwe na hela zingine pembeni ili kuisupport inapohitajika,

Kingine,Biashara huwezi ukaianza leo na kupata faida leo leo,biashara inahitaji time na kujitoa,

Wafanya biashara wengi tu walipata hasara mwanzoni ila hawakurudi nyuma bali walitafiti chanzo cha hasara kisha wakarekebisha,biashara inahitaji uvumilivu,

Mwisho kabisa,sio kila mtu anaweza kua mfanya biashara.
Umemaliza asante kwa ushauli
 
Serikali ukilipwa M3 wewe ni mtu mzito sio powa hapo wastani wa 36M kwa mwaka niambie hapo unanuna uwanja gani kinyerezi au sehemu ya maana(kwanini uende nje ya mji wewe fisi?)

Katika 36M hapo hatujatoa gharama za maisha na vurugu zengine

Self employed is far better biashara ikikubali.
 
Zote ni tamaa tu, wapi unashawishika zaidi? Kuajiriwa au kujiajiri?. Na ipi Ina kurahisishia wewe kuwa mwizi kwa urahisi, kuwa mdhurumaji, kuwa mwongo, kuwa mnafiki, kudharau wengine, kuwa na hila etc

Vipi kwa kufanya hivyo unapata amani na furaha ya kudumu??.. utajiri umejificha humo, amua Leo...jitihada ndio mafanikio...kutendewa hayo na kutenda hayo yote ni majibu kwa moyo wako....amua!!
 
Mkuu kila kitu lazima liwe na mpango wa majaribio kabla ya kufanyiwa kazi.

hauwezi kuamka tu uka sema naacha kazi nika jiajiri, nope it doesn't work like that labda baba ako awe rostam so uko na un limited resources.

Miaka 2-3 Kabla ya kuacha kazi ili paswa uwe Umesha andaa mpango wako, na kuanza kuufanyia kazi uki angalia maendeleo yake.

Kingine biashara au ajira si kwa kila mtu.

Biashara Zinaweza kufeli.
Kazi unaweza fukuzwa (Rejea vyeti feki).

Hivo solution ni kupita na kila fursa ilioko mbele yako, kwa kuamini kua Tomorrow is not guaranteed.
 
Mwalimu wa bachelor take home 520k ambae anadaiwa na HESLB.
520,000×12= 6,240,000/= kwa mwaka

Uliweka matumizi Ya kila mwezi saving inaweza baki 250,000×12=3,000,000/= kwa mwaka.

Maana yake ili ufikishe 10million kwa saving ufanye kazi mika 4.

Ahahahaha.
Kila mtu ashinde mechi zake.
Kuajiriwa sio vibaya.
Tusio na shaka na maswala ya Rizki acha tufuate kadari za Allah
 
Back
Top Bottom